Nini hasa kinawapumbaza waajiriwa?

Nini hasa kinawapumbaza waajiriwa?

Ni Sawa.
Maana Kunawanaopewa Mishahara Duni Vile Vile Lakini Hawana Favor Hiyo.
Kumwambia mtu ambaye ana mshahara duni kapumbazwa na ajira kwa sababu hajajenga nyumba ni kumtia chumvi katika donda lake la mshahara duni.

Sasa walimu na askari ni watu wa kuwalaumu kwa sababu hawajajenga?

Kwa mshahara gani wanaolipwa?
 
Ndio lkn still decision nafanya mimi...wapo mbele yangu...hakuna mtu nyuma yangu wa kunipelekesha
Hata kama hujaajiriwa na umeanzisha ajira yako mwenyewe basi tambua ya kwamba wateja wako ndo ajira yako na hao ndio waajiri wako ndo maana kila siku unapambana ili kuhakikisha unawaridhisha waajiri/wateja/mabossi wako
 
Unakuta mtu ameajiriwa kila mwisho wa mwezi anapokea mshahara, kila katikati ya mwezi anapokea posho, anaishi kwenye nyumba za serikali.Umeme bure na Maji bure.

Amefanya kazi miaka yote na umebaki mwaka mmoja kustaafu, hana kiwanja wala nyumba alojenga kipindi cha ajira miaka yote Hata nyumba alonunua (maybe kujenga ni process)
Majibu ya kinachosababisha ni mawazo finyu yanayopatikana hapa
 
Vipi kwa walijenga kibamba kazi posta
Bora Mara ya hawa wa Kibamba, wana fursa nyingi na jografia yao ya kufika mjini kati haina shida, kuna option ya kupitia maramba mawili kinyerezi, Tabata unaingia town, hawa pia wana access ya mwendokasi. Kibamba is okey ingawa bado ni parefu.
 
Ndio lkn still decision nafanya mimi...wapo mbele yangu...hakuna mtu nyuma yangu wa kunipelekesha
Naomba niingilie uhuru wako hapa mkuu. Kama alivosema Mr hapo juu kuwa ukiwa umejiajiri, basi jua kuwa wewe muajiri wako hapo ni mteja.
Utasema hakuna wakukupelekesha: lakini kumbuka kwamba ukileta huduma ambayo sio chaguo la mteja kwa vyovyote vile itakufia ofisini, lakini mteja akikwambia nataka hiki basi lazima utekeleze.

Maisha ya ajira sio mabaya ni mazuri pia kwa namna yake sababu yanampa mtumishi mafanikio anayohitaji yeye kulingana na vipaombele vyake na namna gani anaisaidia jamii kwa kile alichojahariwa.

Unapoishi katika ajira na hauna malengo na mipango yako ya kesho ( utakapokuwa nje ya ajira ), namna gani utaweza kutatua matatizo kwa jamii na jamii pia ikauthamini mchango wako! Hata katika vitabu vitakatifu, inatafsiriwa kuwa ni kosa kwasababu utaendelea kutumikishwa na wafalme maisha yako yote badala yakuthubutu kutekeleza kile Mungu alichokupa kwa manufaa ya jamii na taifa kwa ujumla wake.
 
Kumwambia mtu ambaye ana mshahara duni kapumbazwa na ajira kwa sababu hajajenga nyumba ni kumtia chumvi katika donda lake la mshahara duni.

Sasa walimu na askari ni watu wa kuwalaumu kwa sababu hawajajenga?

Kwa mshahara gani wanaolipwa?
Kumbuka hapa tunazungumzia ujenzi wa mahala pa kujihifadhi.

Hatuzungumzii Nyumba za mamilioni
 
Kumbuka hapa tunazungumzia ujenzi wa mahala pa kujihifadhi.

Hatuzungumzii Nyumba za mamilioni
Mamilioni ni milioni mbili na kuendelea.

Nyumba gani utajenga chini ya shilingi milioni mbili?

Hata banda la maana la mbao tu tabu kwa bajeti hiyo.
 
Mamilioni ni milioni mbili na kuendelea.

Nyumba gani utajenga chini ya shilingi milioni mbili?

Hata banda la maana la mbao tu tabu kwa bajeti hiyo.
Jenga Hata "Slope House"

Banda, Then laza Mabati.
 
Jenga Hata "Slope House"

Banda, Then laza Mabati.
Usini address mimi kama mimi sijajenga.

Mimi nimejenga yangu ya kuishi mwenyewe na ya kupangisha watu.

Hao unaowaambia wajenge hata slope house, wengine hawana hata hela ya chakula, kulipia ada watoto wala kulipa kodi ya kupanga nyumba.

Na sio wote waajiriwa.

Unakuwa kama yule malkia Marie Antoinette wa Ufaransa, ambaye kuna uvumi kwamba, siku mija aliambiwa watu wa nchi yake wana haki mbaya, hawawezi hata wa kula mkate.

Yeye akawaambia, kama hawawezi kula mkate, basi wale keki.

Wakati keki ni kitu cha bei kubwa zaidi ya mkate!
 
Tatizo ukijenga hawachelewi kukufata kuwa ni mwizi
True ukiwa mwajiriwa yatakiwa uwe fukara ombaomba ukiwa kinyume lzm uletewe tume,ndo lengo la formu za kujaza mali ulizonazo ukiwa mtumishi utakiwi kuwa na Maisha bora uhujumu uchumi utakuhusu.Uzalendo ni kuwa masikini.
 
Eti wanasema kujenga nyumba yako binafsi ni uoga wa maisha. Kazi ya kujenga nyumba ni ya NHC.
Wanamalizia kwa kusema ''mbinguni kuna makao mazuri sana''.
Finali uzeeni ndo majuto hasa ukikaa mda mrefu baada ya kustaafu ukisubiria kwenda makao mazuri
 
Back
Top Bottom