Nini Hakijatimia Hapa???

Nini Hakijatimia Hapa???

Hizi picha zinatia simanzi sana ukiondoa ya mhe Deo kama macho yameona vyema,kiukweli hali ya mtanzania wa kawaida si shwari kabisaaa,na hapo ndio kitu wanachojaribu kueleza watoto hawa,kweli hii ni zaidi ya miaka 50 ya uhuru au ni miujiza ya uhuru.Amakweli mwenye shibe hamkumbuki mwenye njaa.
 
Tumepiga hatua na tunasonga mbele CCM OYEEEEEE!!!!

d%206.jpg
[/QUOTE

Safari ni Safari ukiweka picha ya mtu kashika jembe unaburudisha moyo wangu jembe linalipa njaa na uchoyo unausikia kwa majirani tu hahahaha.]
 
Hizi picha zinatia simanzi sana ukiondoa ya mhe Deo kama macho yameona vyema,kiukweli hali ya mtanzania wa kawaida si shwari kabisaaa,na hapo ndio kitu wanachojaribu kueleza watoto hawa,kweli hii ni zaidi ya miaka 50 ya uhuru au ni miujiza ya uhuru.Amakweli mwenye shibe hamkumbuki mwenye njaa.

kikundi+cha+watoto+wa+shule+ya+awali+ya+Kitobo+Misenye+Bukoba+vijijini+wakimkaribisha+Mke+wa+Rais+Mama+SALMA+Kikwete+2-10-2010.jpg
 
Safari_ni_Safari thread kama hizi huwezi kuwaona wala jamaa wanachangia maana wanajua kwa uhalisia hii ni hali ya shle zetu huko mtaani na haya nimaisha ya watu wengi sana huko mtaani ambao hawajui kesho itakuwaje
Mtoto anaenda shule pekupeku na ni kilometa kadhaa kutoka anapoishi wengine kama wale wa Rufiki inabidi wavuke mto kwa mtumbwi wakati wanaenda shule na kurudi hakuna daraja
Mtoto anaenda shule tumboni kweupe hajala chochote na anatakiwa adumu na hiyo hali Mungu saidia kama shuleni wanapewa uji na kama hakuna uji shuleni atashinda na njaa yake mpaka jioni atakaporudi ale mlo mmoja huo ni wa moja kwa moja mpaka kesho yake
Mtoto anaenda shule uniform aliyovaa haijulikani ni nyeupe au ya njano (kwanza kama atabahatika kuwa na uniform) na ina viraka mpaka vingine vinaulizana wewe umekuja lini
Mtoto anaenda shule anakumbana na mwalimu mwenye njaa na yeye ambaye hana mshahara mwezi wa pili na amekopa kwa mangi mpaka amechokwa na mwenye duka na hapo anadaiwa kodi ya nyumba hapo unafikiri anawafundisha watoto nini
Mtoto anaenda shule anakumbana na kukalia jiwe au kwenye vumbi na darasa ambalo ni mbavu za mbwa mvua yake na upepo wake na jua lake unafikiri akifundishwa kinaingia kitu kweli hapo
Mtoto hana kitabu cha kupitia kile alichofundishwa kama hakumwelewa mwalimu imekula kwake
halafu unategemea matokeo makubwa kama sio mwanafunzi anamaliza la saba hajui kusoma na kuandika na mtihani ukija anafaulu kwenda secondary huko sijui ndo ataenda kuelewa nini kama sio zero ya form four inamsubiri ohhh division five samahani
cc BAK
 
Last edited by a moderator:
Nitakuja Mkuu Rocky, ngoja niwajibike kwanza.
 
Last edited by a moderator:
Umenikumbusha mbali jamani, maisha haya, haya bana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom