Salary Slip
Platinum Member
- Apr 3, 2012
- 52,178
- 162,659
Lengo kubwa la kununua hizi ndege hasa hii kubwa inaonekana ilikuwa ni kujijenga kisiasa na ndio maana imeandikwa hapa kazi tu.Kama kawaida yetu watanzania,kama kawaida yetu waafrika tuishio chini ya jangwa na sahara kwakweli Tanzania ilikuwa haina haja ya kununua hii Boeing 787 Dreamliner,tulikuwa tunatakiwa tujikite kwa nguvu zetu zote katika kukabili usafiri wa ndege wa ndani(local) ya nchi,kuliko kujingiza katika kutaka kusafiri nchi ya nchi..
Nimemsikia Raisi akisema hiyo Boeing 787 Dreamliner itafanya safari za kwenda India,Thainland nk,hivi kweli ATC inaweza kushindana na mashirika kama Emirates na Qatar mashirika ambayo yamewagaragaza mashirikamakubwa makubwa kama KLM,Lufthansa nk..
Hao watalii wanao wazungumza tulitakiwa tusubiri akina Emirates,Turkish airline,Qatar,Klm na mashirika mengine watumwagia hapa Tanzania,Halafu ATC inawasambaza watalii ndani ya Tanzania kwa ndege zetu,bomberdia ingelifaa sana kwa kazi hiii,mdogo mdogo baada ya kudhidhibiti safari za ndani,tungelianza kusafirisha wasafiri nchi jirani, baadae ndio tungeliamua kufikiria kuruka nje ya Afrika..
Raisi Kakurupuka,ataitia nchi katika hasara,/////Unajua shirika kubwa kama KLM kwa sasa limejikita Zaidi katika safari za ndani za mji kwa mji kuliko masafari marefu ili kuepusha hasara,kwanini ATC isiigie mfano wa KLM!?
Sidhani kama walijipa muda wa jinsi gani ya kufufua hili shirika kibiashara bali inaonekane waliwaza kulifufua kisiasa zaidi na ndio maana hata hii ndege imepokelewa kisiasa wakiamini wanawakomoa wapinzani na ndio maana pia walielekeza vijembe kwa wapinzani.
Si ajabu sasa ndio wanaumiza vichwa ni namna gani watamudu kuendesha hili shirika na hususani hiyo ndege kubwa na hizo zingine zinazotarajiwa kuwasili siku za usoni.
Wakati wao wanadhani zile mbwembwe zilikuwa ni za kutuma ujumbe kwa upinzani, ni mbwembwe hizo hizo ambazoni wapinzani watakuja kuzitumia kama reference wakati wa kuwasuta na kuwakosoa.
Time will tell.