Nini 787 dreamliner na tugemee nini?

Nini 787 dreamliner na tugemee nini?

Mtegemee kupata taabu sana kwa umbeya wenu. Mngekuwa na akili za kuangalia financial projections na profitability mngewasaidia dada zenu wanaouza kwa bei ya hasara sasa hivi. Mtapata taabu sana nasema.

Maoni murua kabisa kaka Nduka wewe kweli ndio unaakili na hutopata tabu kabisa.
 
Mimi naomba tupeane moyo sio kuvunjana

Mkuu DJ Sepetu hio kupeana moyo ndio ilipolifikisha taifa hapa lilipo. Mwenyewe alienunua ndege sio mtu wa kupeana moyo huwa anaongea kwa jinsi anavyojua, watu wakifa njaa kwa ukame huwa anawaambia kabisa kufeni lakini hapa hakuna chakula cha bure..... hakuna kupeana moyo kaka, tunaangamia kaka
 
Mkuu celinawetu sio mbaya kuanza moja lakini nadhani kwanza wengejikita zaidi katika kutafuta soko la ndani na la kati kabla hawajaamua kuleta fleet kubwa na kutangaza tunaenda London, nenda kwanza Rwanda, Burundi, congo, Bujumbura, Nairobi, south africa na kwengineko Africa, Mungu ana makusudi yake kumfanya binaadamu awe anakuwa kwa stage, kuanzia kichanga kisichojiweza hadi kuwa mtu mzima kamili. Pale kuna funzo kubwa kwa chochote unachotaka kuanzisha katika mfumo wa kimaisha kwa mwanadaamu. Tusikimbilie tu kutaka makubwa.

Mkuu umenena vyema,tatizo hataki kutumia wataalam wamshauri, anatumia ukoo kumshauri,watu kama wewe ni muhimu ila nafasi ya kumshauri huwez kuwa nayo kwa sababu ya ubinafsi,
Hyo ndege hata aseme ataninyonga wallah haitafika popote
 
Dharra ni kweli tuna safari ndefu sana, pia changamoto ulizotuonesha. Sasa nini ushauri wako katika hili la kufufua shirika letu la ndege!!!!???

Mkuu eliakeem mimi nilikuwa humo kwenye airlines kwa miaka kadhaa, ninachokisema hapa ni kuwa tutafakari kwa kina ni vipi vipaumbele kwa shirika hili kabla hatujafanya uwekezaji mkubwa. Ndege ya size ya kati zingefanya vizuri sana kwa sasa. Tungewekeza kwenye zile zile ATRs na ndege aina hio, taratibu tunakuwa na kupevuka kiakili katika biashara ya ndege. Karibuni tu hapa jengo la ATC lilitaka kupigwa mnada kwa sababu ya madeni, tena tukasikia tuna matatizo na IATA, kidogo tunasikia ndege moja imekuwa grounded Mwanza kutokana na hitilafu za kiufundi... tungeanza taratibu kwanza haraka hizi za nini?
 
Wana Jukwaa. Ni jana tu tumetoka kushuhudia kuwasili kwa ndege yetu inayoitwa Boeing 787 dreamliner. Wengi wetu nadhani bado hatufahamu kwa kina ni nini hasa kimewasili na mategemeo ni yepi katika kukuza uchumi wa Taifa hili.
Ningeomba sana uendelee na kazi yako ya biashara ya bodaboda au bajaji na hata daladala lakini mambo ya ndege uachie watu wenye upeo wa kuweza kuelezea mambo! Naona sasa kila mtu aki-google na kusoma vi- mistari viwili vitatu kuhusu aina ya hizi ndege basi hapo hapo anajigeuza mtalaam mshauri!
 
Mkuu eliakeem mimi nilikuwa humo kwenye airlines kwa miaka kadhaa, ninachokisema hapa ni kuwa tutafakari kwa kina ni vipi vipaumbele kwa shirika hili kabla hatujafanya uwekezaji mkubwa. Ndege ya size ya kati zingefanya vizuri sana kwa sasa. Tungewekeza kwenye zile zile ATRs na ndege aina hio, taratibu tunakuwa na kupevuka kiakili katika biashara ya ndege. Karibuni tu hapa jengo la ATC lilitaka kupigwa mnada kwa sababu ya madeni, tena tukasikia tuna matatizo na IATA, kidogo tunasikia ndege moja imekuwa grounded Mwanza kutokana na hitilafu za kiufundi... tungeanza taratibu kwanza haraka hizi za nini?
Kama kweli umewahi kuwa ''humo kwenye airlines'' kwa miaka kadhaa basi bora unyamaze kwani nyie ndiyo mlioua shirika letu. Ingekuwa busara mkakaa kimya na kuachia wengine waje na mawazo yao na wakishindwa wakishindwe kivyao.
 
"mfano mgeni huyu anatumia lita 6,811 kwa saa" hili jambo unauhakika nalo, kutoka USA mpaka TZ itatumia lita ngapi? kwa muda wa masaa 13 hadi 16? mnapoongea muwe na uhakika. unajua hiyo ni Sh ngapi mafuta tu. hapa kunauongo kabisaaa.

mbogo31 tunasimama kwenye kukoselewa tuambie hapa ukweli ni upi? kutoka Seattle Marekani ilipokuwa assembled mpaka dar es salaam ni mwendo wa masaa 22 na dakika 39 kwa ndege za abiria na ni lazima usimame kwa ajili ya kuongeza mafuta njiani. Ndege yetu labda imetumia 13 mpaka 16hrs sababu haikuwa na mizigo wala abiria kwa hio hakukuwa na sababu ya kujaza mafuta. Kama unajua ukweli weka hapa tupate faida kaka hii ni ndege yetu sote watanzania tunachangia mada ili kupata uhalisia wa nini kinaendelea sio siasa hapa.
 
Kama kweli umewahi kuwa ''humo kwenye airlines'' kwa miaka kadhaa basi bora unyamaze kwani nyie ndiyo mlioua shirika letu. Ingekuwa busara mkakaa kimya na kuachia wengine waje na mawazo yao na wakishindwa wakishindwe kivyao.

Kaka sijawahi kufanya kazi ATCL hata mara moja. Nimekuwa nchi jirani na nje kidogo. Nimeona si busara kukaa kimya wakati ninacho cha kuwahabarishia Watz wenzangu. Kama kuna wengine watakuja na mawazo yao ni vizuri ndio kujifunza.
 
Wana Jukwaa. Ni jana tu tumetoka kushuhudia kuwasili kwa ndege yetu inayoitwa Boeing 787 dreamliner. Wengi wetu nadhani bado hatufahamu kwa kina ni nini hasa kimewasili na mategemeo ni yepi katika kukuza uchumi wa Taifa hili.

Hii ni ndege ambayo imeundwa rasmi na kampuni na Boeing kutoka marekani kwa ajili ya kuruka umbali mkubwa (long haul aka long range) na ina uwezo wa kuchukua abiria kuanzia 242 hadi 335 kutegemea na jinsi utakavyopanga viti. Uzinduzi rasmi wa ndege hizi za dreamliner ulifanyika kwa mbwembwe nyingi mnamo July 8 2007. wadau mbali mbali wa safari za ndege duniani nzima walichangia katika ujenzi wa ndege hizi na mpaka kufika December 15, 2009 Dreamliner ilifanya safari yake ya kwanza na ilipofika mwaka 2011, Boeing walitangaza rasmi kuwa sasa Dreamliner zipo tayari kwa mauzo.

Kufikia October 26, 2011 Shirika la ndege la Japan liitwalo ALL NIPPON Airways walitoa oda yao ya kwanza kununua dreamliner, ndege hizi ziliingia kwenye ushindani rasmi wa kibiashara mnamo August 7 2014 na mpaka kufikia mwezi May mwaka huu 2018 Dreamliner tayari walishapokea oda ya ndege 1,377 nyingi zikinunuliwa na shirika la ndege la Marekani liitwalo American Airlines. Tangu kuundwa kwake na kuanza kuruka ndege hizi zimeshuhudia matatizo kadhaa ikiwemo kuripuka kwa battery (on board fire) wakati zinaruka kibishara. Hio ndio historia fupi ya mgeni wetu huyu dreamliner ambapo imewagharimu Boeing kiasi cha dola za Kimarekani billioni 32 kama gharama za matengenezo.

Kama nilivyoainisha kabla Boeing wamepokea oda zipatazo 1,377, lakini hadi sasa ni ndege 691 pekee ambazo tayri zimefika mikononi mwa wateja tokea kuundwa kwake.

January 8 2013 Shirika la ndege la Japana waligundua uvujaji wa mafuta katika moja ya dreamliner zake, na hivyo kusitisha safari ya kuelekea Boston ghafla wakati abiria wakiwa tayari kwa safari.
January 9 Shirika la ndege la Marekani walilalamika kutokea kwa cheche za moto (wiring problem) karibia kabisa na mahala ilipo battry.
January 13, 2013 ilitokea tena kuvuja kwa mafuta katika moja ya dreamliner.
January 14, 2014, Kuonekana kwa moshi wakati ndege ikiwa angani tena karibu kabisa na mahala ilipo battery. Na kasoro nyingi nyenginezo.

Tutegemee mwanzo mgumu sana. Kuwa na ndege moja inayoruka umbali mrefu (long haul) kuna ugumu wake hasa linapojitokeza suala la technical issues na ikalazimika ndege kutokuruka, kitu ambacho ni cha kawaida sana katika mambo ya ndege, na ndio maana wenzetu Ethiopian Airways wakajenga hoteli zao maalum (ziligharimu Dola milioni 91) kwa ajili ya abiria inapojitokeza kuchelewa kwa ndege kwa sababu za kiufundi (delay) kama hizi nilizoainisha hapo juu, inagwa wenzetu wapo na ndege nyingi za kuwasaidia kuhaulisha abiria na haraka inavyowezekana. Hapo tutegemee Delay, na hili lisipofanyiwa kazi linaweza kutugharimu baadae kibiashara, na pia kujiandaa na kipindi cha matengenezo ambapo ni lazima ndege isafiri (labda Ethiopia) kwa matengenezo ambayo nayo huchukua muda.

Ukifikiria hayo na mengine mengi utaona tuna safari ngumu sana ya kwenda kwa mfano mgeni huyu anatumia lita 6,811 kwa saa, piga hesabu Dar/Mwz ni mwendo wa saa moja na robo kwenda na kurudi masaa mawili na nusu utaona ugumu uliopo katika kuendesha ndege hii. Nilitegemea mapokezi ya kimya kimya na badala yake kutumia muda mwingi kuwaza na kuwazua kutafakari ni kwa vipi mgeni huyu ataleta faida. ITS NOT GONNA BE EASY FELLAS!!!
View attachment 805866
Kuna mambo yanaimiza vichwa sana ila wengi hatuoni, naukisema unaonekana huna uzalendo, anyway let's wait and see
 
Hakuna mafanikio yaliyokuja lelemama, ili ufanikiwe lazima uwetayari kukumbana na magumu.

lkn pia lengo hasa si biashara ya ndege bali ni utalii mfano kama ndege italeta hasara ya 300bil huku imekuza utalii na tukavuna mfano tr 7 from let say 1tr hiyo itakuwa ni hasara au faida?

akili za kuambiwa.

Nakubaliana na wewe sana, baadhi ya wataalamu wanahoji kulikoni hadi sasa hawajaweka schedule ya ndege kwenye system ukitegemea wataanza kuruka hivi karibuni? mkuu Umkilo nikuulize umeona popote kwamba ATCL wame merge na Shirika la utalii kujiandaa na kutoa mpango kazi? wapi umeona? tupe data mkuu
 
Kaka sijawahi kufanya kazi ATCL hata mara moja. Nimekuwa nchi jirani na nje kidogo. Nimeona si busara kukaa kimya wakati ninacho cha kuwahabarishia Watz wenzangu. Kama kuna wengine watakuja na mawazo yao ni vizuri ndio kujifunza.
Ulichoandika kwenye post yako hakinishawishi kukubali kweli kuwa wewe unajua undani wa biashara ya ndege! It is too shallow! (Ila siyo kama nasema hakuna mapungufu kwenye ununuzi wa hizi ndege, la hasha. Inaonekana kabisa hakuna maandalizi ya kutosha kwani hata ukiingia kwenye webiste ya shirika bado ni ya kiwango cha chini sana.
 
Routine maintenance huwa inafanyika kila ndege inapotua uwanjani. Si mpaka iharibike, check ups zote zinafanyika kabla ndege haijaondoka na hii inafanyika kila ndege inapotua..
Ni utaratibu wa dunia nzima.

Engineer gani hapa mwenye Ratings za Boeing kutengeneza dreamliner? mtaje. mimi naongelea Check B na Check C siongelei daily preflight checkups mkuu. Hizo ndio za kila siku na zinajuilikana
 
Wana Jukwaa. Ni jana tu tumetoka kushuhudia kuwasili kwa ndege yetu inayoitwa Boeing 787 dreamliner. Wengi wetu nadhani bado hatufahamu kwa kina ni nini hasa kimewasili na mategemeo ni yepi katika kukuza uchumi wa Taifa hili.

Hii ni ndege ambayo imeundwa rasmi na kampuni na Boeing kutoka marekani kwa ajili ya kuruka umbali mkubwa (long haul aka long range) na ina uwezo wa kuchukua abiria kuanzia 242 hadi 335 kutegemea na jinsi utakavyopanga viti. Uzinduzi rasmi wa ndege hizi za dreamliner ulifanyika kwa mbwembwe nyingi mnamo July 8 2007. wadau mbali mbali wa safari za ndege duniani nzima walichangia katika ujenzi wa ndege hizi na mpaka kufika December 15, 2009 Dreamliner ilifanya safari yake ya kwanza na ilipofika mwaka 2011, Boeing walitangaza rasmi kuwa sasa Dreamliner zipo tayari kwa mauzo.

Kufikia October 26, 2011 Shirika la ndege la Japan liitwalo ALL NIPPON Airways walitoa oda yao ya kwanza kununua dreamliner, ndege hizi ziliingia kwenye ushindani rasmi wa kibiashara mnamo August 7 2014 na mpaka kufikia mwezi May mwaka huu 2018 Dreamliner tayari walishapokea oda ya ndege 1,377 nyingi zikinunuliwa na shirika la ndege la Marekani liitwalo American Airlines. Tangu kuundwa kwake na kuanza kuruka ndege hizi zimeshuhudia matatizo kadhaa ikiwemo kuripuka kwa battery (on board fire) wakati zinaruka kibishara. Hio ndio historia fupi ya mgeni wetu huyu dreamliner ambapo imewagharimu Boeing kiasi cha dola za Kimarekani billioni 32 kama gharama za matengenezo.

Kama nilivyoainisha kabla Boeing wamepokea oda zipatazo 1,377, lakini hadi sasa ni ndege 691 pekee ambazo tayri zimefika mikononi mwa wateja tokea kuundwa kwake.

January 8 2013 Shirika la ndege la Japana waligundua uvujaji wa mafuta katika moja ya dreamliner zake, na hivyo kusitisha safari ya kuelekea Boston ghafla wakati abiria wakiwa tayari kwa safari.
January 9 Shirika la ndege la Marekani walilalamika kutokea kwa cheche za moto (wiring problem) karibia kabisa na mahala ilipo battry.
January 13, 2013 ilitokea tena kuvuja kwa mafuta katika moja ya dreamliner.
January 14, 2014, Kuonekana kwa moshi wakati ndege ikiwa angani tena karibu kabisa na mahala ilipo battery. Na kasoro nyingi nyenginezo.

Tutegemee mwanzo mgumu sana. Kuwa na ndege moja inayoruka umbali mrefu (long haul) kuna ugumu wake hasa linapojitokeza suala la technical issues na ikalazimika ndege kutokuruka, kitu ambacho ni cha kawaida sana katika mambo ya ndege, na ndio maana wenzetu Ethiopian Airways wakajenga hoteli zao maalum (ziligharimu Dola milioni 91) kwa ajili ya abiria inapojitokeza kuchelewa kwa ndege kwa sababu za kiufundi (delay) kama hizi nilizoainisha hapo juu, inagwa wenzetu wapo na ndege nyingi za kuwasaidia kuhaulisha abiria na haraka inavyowezekana. Hapo tutegemee Delay, na hili lisipofanyiwa kazi linaweza kutugharimu baadae kibiashara, na pia kujiandaa na kipindi cha matengenezo ambapo ni lazima ndege isafiri (labda Ethiopia) kwa matengenezo ambayo nayo huchukua muda.

Ukifikiria hayo na mengine mengi utaona tuna safari ngumu sana ya kwenda kwa mfano mgeni huyu anatumia lita 6,811 kwa saa, piga hesabu Dar/Mwz ni mwendo wa saa moja na robo kwenda na kurudi masaa mawili na nusu utaona ugumu uliopo katika kuendesha ndege hii. Nilitegemea mapokezi ya kimya kimya na badala yake kutumia muda mwingi kuwaza na kuwazua kutafakari ni kwa vipi mgeni huyu ataleta faida. ITS NOT GONNA BE EASY FELLAS!!!
View attachment 805866
Hii ni ndege maalumu kwa safari za nje na humu nchin zinatumika hizo zilizotangulia acheni kupotosha na kuleta siasa za maji taka,watu wana akili zaidi yako wewe.
 
Nakubaliana na wewe sana, baadhi ya wataalamu wanahoji kulikoni hadi sasa hawajaweka schedule ya ndege kwenye system ukitegemea wataanza kuruka hivi karibuni? mkuu Umkilo nikuulize umeona popote kwamba ATCL wame merge na Shirika la utalii kujiandaa na kutoa mpango kazi? wapi umeona? tupe data mkee.
For sure sijaona na hizi ni vitu za wataalamu wetu sasa kufanya hiyo coodination. ni swala la taaluma
 
Ningeomba sana uendelee na kazi yako ya biashara ya bodaboda au bajaji na hata daladala lakini mambo ya ndege uachie watu wenye upeo wa kuweza kuelezea mambo! Naona sasa kila mtu aki-google na kusoma vi- mistari viwili vitatu kuhusu aina ya hizi ndege basi hapo hapo anajigeuza mtalaam mshauri!

Ni nani huyo mwenye upeo? kama wewe unao upeo weka utaalamu wako hapa. Ndege sio ya watu wenye upeo ni ya Watanzania wote, mimi na wewe pia ni watz kaka, wewe kama huna upeo sawa ila mimi nina upeo na ndo maana nikaweka ninayoyajua bayana hapa. Miaka zaidi ya 10 nipo kwenye biashara ya ndege na nadhani nasema ninacho kijua. wewe sio lazima kuchangia msubiri tu mwenye upeo aje aweke upeo wake.
 
Hii ni ndege maalumu kwa safari za nje na humu nchin zinatumika hizo zilizotangulia acheni kupotosha na kuleta siasa za maji taka,watu wana akili zaidi yako wewe.

Hakuna siasa hapa kaka mfianchi wewe kama una taarifa za kitaalamu kuhusu mauzo na namna ndege hii itakavyotengeneza faida weka hapa. Usi comment tu kuonekana na wewe ume comment weka data hapa tupate faida sote
 
Back
Top Bottom