Nini 787 dreamliner na tugemee nini?

Dharra

JF-Expert Member
Jun 23, 2017
1,661
2,931
Wana Jukwaa. Ni jana tu tumetoka kushuhudia kuwasili kwa ndege yetu inayoitwa Boeing 787 dreamliner. Wengi wetu nadhani bado hatufahamu kwa kina ni nini hasa kimewasili na mategemeo ni yepi katika kukuza uchumi wa Taifa hili.

Hii ni ndege ambayo imeundwa rasmi na kampuni na Boeing kutoka marekani kwa ajili ya kuruka umbali mkubwa (long haul aka long range) na ina uwezo wa kuchukua abiria kuanzia 242 hadi 335 kutegemea na jinsi utakavyopanga viti. Uzinduzi rasmi wa ndege hizi za dreamliner ulifanyika kwa mbwembwe nyingi mnamo July 8 2007. wadau mbali mbali wa safari za ndege duniani nzima walichangia katika ujenzi wa ndege hizi na mpaka kufika December 15, 2009 Dreamliner ilifanya safari yake ya kwanza na ilipofika mwaka 2011, Boeing walitangaza rasmi kuwa sasa Dreamliner zipo tayari kwa mauzo.

Kufikia October 26, 2011 Shirika la ndege la Japan liitwalo ALL NIPPON Airways walitoa oda yao ya kwanza kununua dreamliner, ndege hizi ziliingia kwenye ushindani rasmi wa kibiashara mnamo August 7 2014 na mpaka kufikia mwezi May mwaka huu 2018 Dreamliner tayari walishapokea oda ya ndege 1,377 nyingi zikinunuliwa na shirika la ndege la Marekani liitwalo American Airlines. Tangu kuundwa kwake na kuanza kuruka ndege hizi zimeshuhudia matatizo kadhaa ikiwemo kuripuka kwa battery (on board fire) wakati zinaruka kibishara. Hio ndio historia fupi ya mgeni wetu huyu dreamliner ambapo imewagharimu Boeing kiasi cha dola za Kimarekani billioni 32 kama gharama za matengenezo.

Kama nilivyoainisha kabla Boeing wamepokea oda zipatazo 1,377, lakini hadi sasa ni ndege 691 pekee ambazo tayri zimefika mikononi mwa wateja tokea kuundwa kwake.

January 8 2013 Shirika la ndege la Japana waligundua uvujaji wa mafuta katika moja ya dreamliner zake, na hivyo kusitisha safari ya kuelekea Boston ghafla wakati abiria wakiwa tayari kwa safari.
January 9 Shirika la ndege la Marekani walilalamika kutokea kwa cheche za moto (wiring problem) karibia kabisa na mahala ilipo battry.
January 13, 2013 ilitokea tena kuvuja kwa mafuta katika moja ya dreamliner.
January 14, 2014, Kuonekana kwa moshi wakati ndege ikiwa angani tena karibu kabisa na mahala ilipo battery. Na kasoro nyingi nyenginezo.

Tutegemee mwanzo mgumu sana. Kuwa na ndege moja inayoruka umbali mrefu (long haul) kuna ugumu wake hasa linapojitokeza suala la technical issues na ikalazimika ndege kutokuruka, kitu ambacho ni cha kawaida sana katika mambo ya ndege, na ndio maana wenzetu Ethiopian Airways wakajenga hoteli zao maalum (ziligharimu Dola milioni 91) kwa ajili ya abiria inapojitokeza kuchelewa kwa ndege kwa sababu za kiufundi (delay) kama hizi nilizoainisha hapo juu, inagwa wenzetu wapo na ndege nyingi za kuwasaidia kuhaulisha abiria na haraka inavyowezekana. Hapo tutegemee Delay, na hili lisipofanyiwa kazi linaweza kutugharimu baadae kibiashara, na pia kujiandaa na kipindi cha matengenezo ambapo ni lazima ndege isafiri (labda Ethiopia) kwa matengenezo ambayo nayo huchukua muda.

Ukifikiria hayo na mengine mengi utaona tuna safari ngumu sana ya kwenda kwa mfano mgeni huyu anatumia lita 6,811 kwa saa, piga hesabu Dar/Mwz ni mwendo wa saa moja na robo kwenda na kurudi masaa mawili na nusu utaona ugumu uliopo katika kuendesha ndege hii. Nilitegemea mapokezi ya kimya kimya na badala yake kutumia muda mwingi kuwaza na kuwazua kutafakari ni kwa vipi mgeni huyu ataleta faida. ITS NOT GONNA BE EASY FELLAS!!!
boeing.jpg
 
Dream liner ni ndege mbovu zilizokataliwa duniani kote. Hivyo ni janga litakalotuletea mabalaaaaa
Aliyelinunua atapata taaabu sanaaa...
Kwanza zinaitwa terrible teen yaani kijana-mtoto msumbufu. Achilia mbali kulipuka betri na kuvuja mafuta, pia ni nzito kama fiati.
 
Taratibu za manunuzi zilizingatiwa au?
Kwani lazima wangepata historia yake na utendeaji kazi wake ulivyo.
 
Mtegemee kupata taabu sana kwa umbeya wenu. Mngekuwa na akili za kuangalia financial projections na profitability mngewasaidia dada zenu wanaouza kwa bei ya hasara sasa hivi. Mtapata taabu sana nasema.
 
Dharra ni kweli tuna safari ndefu sana, pia changamoto ulizotuonesha. Sasa nini ushauri wako katika hili la kufufua shirika letu la ndege!!!!???
 
Hizo changamoto ni za kawaida. Ni kama zilivyo kwa Airbus na hata aina nyingine za ndege za abiria!

Liliniumiza ni gharama za ununuzi aisee!

Yani dola Bilioni 32?
Hivi hii ni sawa na Bajeti ya wizara gani?
 
Ndege zinanunuliwa bila kufuata bajeti wala tender process.

Halafu kuna watu wanashangilia.
Tuwe tunaangalia na mazuri pia ya serikali yetu
Ukilitimba unaweza chelewesha maendeleo
Leo hapa ingefuatwa process huenda hadi magu anatoka tusingenunua hata ndege ya abiria kumi
 
Hizo changamoto ni za kawaida. Ni kama zilivyo kwa Airbus na hata aina nyingine za ndege za abiria!

Liliniumiza ni gharama za ununuzi aisee!

Yani dola Bilioni 32?
Hivi hii ni sawa na Bajeti ya wizara gani?
Mzee baba umechemsha unajua dollar hizo ni sh ngapi za madafu?
 
Wana Jukwaa. Ni jana tu tumetoka kushuhudia kuwasili kwa ndege yetu inayoitwa Boeing 787 dreamliner. Wengi wetu nadhani bado hatufahamu kwa kina ni nini hasa kimewasili na mategemeo ni yepi katika kukuza uchumi wa Taifa hili.

Hii ni ndege ambayo imeundwa rasmi na kampuni na Boeing kutoka marekani kwa ajili ya kuruka umbali mkubwa (long haul aka long range) na ina uwezo wa kupakia abiri kuanzia 242 hadi 335 kutegemea na jinsi utakavyopanga viti. Uzinduzi rasmi wa ndege hizi za dreamliner ulifanyika kwa mbwembwe nyingi mnamo July 8 2007. wadau mbali mbali dunia nzima walichangia katika ujenzi wa ndege hizi na kufika December 15, 2009 Dreamliner ilifanya safari yake ya kwanza na ilipofika mwaka 2011, Boeing walitangaza rasmi kuwa sasa Dreamliner zipo tayari kwa mauzo.

Kufikia October 26, 2011 Shirika la ndege la Japan liitwalo ALL NIPPON Airways walitoa oda yao ya kwanza kununua dreamliner, ndege hizi ziliingia kwenye ushindani rasmi wa kibiashara mnamo August 7 2014 na mpaka kufikia mwezi May mwaka huu 2018 Dreamliner tayari wameuza ndege 1,377 nyingi zikinunuliwa na shirika la ndege la Marekani liitwalo American Airlines. Tangu kuundwa kwake na kuanza kuruka ndege hizi zimeshuhudia matatizo kadhaa ikiwemo kuripuka kwa battery (on board fire) wakati zinaruka kibishara. Hio ndio historia fupi ya mgeni wetu huyu dreamliner ambapo imewagharimu Boeing kiasi cha dola za Kimarekani billioni 32 kama gharama za matengenezo.

Kama nilivyoainisha kabla Boeing wamepokea oda zipatazo 1,377, lakini hadi sasa ni ndege 691 pekee ambazo tayri zimefika mikononi mwa wateja tokea kuundwa kwake.

January 8 2013 Shirika la ndege la Japana waligundua uvujaji wa mafuta katika moja ya dreamliner zake, na hivyo kusitisha safari ya kuelekea Boston ghafla wakati abiria wakiwa tayari kwa safari.
January 9 Shirika la ndege la Marekani walilalamika kutokea kwa chichi za moto (wiring problem) karibia kabisa na bettry.
January 13, 2013 uklitokea tena kuvuja kwa mafuta.
January 14, 2014, Kuonekana kwa moshi ndege ikiwa angani tena karibu kabisa na bettery. Na kasoro nyingi nyenginezo.

Tutegemee mwanzo mgumu sana. Kuwa na ndege moja inayoruka umbali mrefu (long haul) kuna ugumu wake hasa linapojitokeza suala la technical issues na ikalazimika ndege kutokuruka, kitu ambacho ni cha kawaida sana katika mambo ya ndege na ndio maana wenzetu Ethiopian Airways wakajenga hoteli zao maalum (ziligharimu Dola milioni 91) kwa ajili ya abiria inapojitokeza delay kama hizi inagwa wenzetu wapo na ndege nyingi za kuwasaidia kuhaulisha haraka inavyowezekana. Hapo tategemee Delay, na hili lisipofanyiwa kazi linaweza kutugharimu baadae kibiashara, na pia kujiandaa na kipindi cha matengenezo ambapo ni lazima ndege isafiri (labda Ethiopia) kwa matengenezo ambayo nao huchukua muda.

Ukifikiria hayo na mengine mengi utaona tuna safari ngumu sana ya kwenda kwa mfano mgeni huyu anatumia lita 6,811 kwa saa, utaona ugumu uliopo katika kuendesha ndege hii. Nilitegemea mapokezi ya kimya kimya na badala yake kutumia muda mwingi kuwaza na kuwazua ni kwa vipi mgeni huyu ataleta faida. ITS NOT GONNA BE EASY FELLAS!!!
View attachment 805866
Watatembea na spana angani kama marubani walioileta walivyofanya! Au tatizo hilo halikutokea? Kama halikujitokeza, itachukua muda gani kujitokeza?
 
"mfano mgeni huyu anatumia lita 6,811 kwa saa" hili jambo unauhakika nalo, kutoka USA mpaka TZ itatumia lita ngapi? kwa muda wa masaa 13 hadi 16? mnapoongea muwe na uhakika. unajua hiyo ni Sh ngapi mafuta tu. hapa kunauongo kabisaaa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom