Hata mimi na hope sipo sahihi, lakini maandishi yapo ukutani.
1. Sekta ya ndege dunia nzima iko tricky sana, inahitaji weledi wa hali ya juu kwenda nao, sisi kwa historia yetu ya ATC hatuwezi kusema tumefika hapo. Tulitakiwa kufanya baby steps, kuimarisha technical capabilities, kuimarisha uongozi, kuimarisha viwanja kabla ya kununua midege mikubwa.
2. Tuchukue uzoefu kwa waliofanikiwa, walifanyaje? Nilikuwa namsikiliza CEO wa Ethiopia Airlines anahojiwa na BBC. Akaulizwa, sekta ya usafiri wa anga ni ngumu sana, Ethiopia mmewezaje kufanikiwa hivyo? Akajibu, sababu ni nyingi, ila moja la msingi ni kwamba wataalam tumeachiwa tufanye maamuzi yetu kitaalamu, serikali na wanasiasa hawajatuingilia katika biashara.
Tanzania serikali ya Magufuli haiwezi kufanya hivyo, inaingilia sana wataalamu.
Kama una wasaa na nafasi msikilize mwenyewe hapa (6 minutes clip and worth the insight) -->
BBC World News - Africa Business Report, 11/08/2017 GMT, Why is Ethiopian Airlines so successful?
Sisi Tanzania tunafanya tofauti, biashara inaenda kisiasa, maamuzi yanafanywa kisiasa. Serikali inanunua ndege kisiasa. Hata uzinduzi wa ndege ni shughuli ya kisiasa.
3. Midege mikubwa hii inafaa zaidi kwa routes ndefu za kimataifa. Tanzania soko kubwa sana la safari za ndege ambalo halina ushindani mkubwa sana ni safari za ndani. Kwenye safari ndefu, ATC haina advantage ya "economies of scale". Haiwezi kushindana na Wa Ethiopia, Waturuki, Qatar etc. Hatujafikia hata standards za kimataifa za kurusha direct flight from Dar to New York kwa mfano. We are setting ourselves for failure either way. Tukiitumia ndege kubwa kwa safari za ndani hatuwezi kuitumia ipaswavyo, kwa safari za nje hatuna competitive advantage.
4. Ndege hizi zinakuja na mikataba ya matengenezo. Unaponunua ndege kutoka kampuni tofauti tofauti,unakuwa na mikataba na makampuni tofauti tofauti. Sijaelewa logic ya kununua Bombardier halafu pia tukanunua Dreamliner. Hususan kwa shirikadogokama letu. Maana yake tutalipa charges fulani kwa kampuni mbili wakati tungeweza kuwa na "economies of scale" kubwa zaidi kama tunge stick na kampuni moja.
5.Kama manunuzi ya ndege hayajafuata bajeti wala a transparent tender process, sina imani sana na muendelezo wa mradi huu. Tutaangaliaje "cost benefit analysis" wakati hata manunuzi yalivyofanyika hatujui? Nasikia Zitto anaomba mkataba, akifanikiwa kuupata na kutujulisha atakuwa kafanya jambo la maana sana.
Inaonekana, kiujumla, kwamba serikali hainunui ndege ili kumaliza tatizo la usafiri walakutengeneza faida (sehemu nyingi hazina hata viwanja vya ndege vya kuweza kui accommodate hii ndege). Inaonekana serikali inanunua ndege kubwa kwa ulimbukeni wa kujionesha "na sisi tumo, tuna ndege kubwa", bila hata ya kuwa na mipango mizuri ya kuhakikisha shirikala ndege linaweza kujiendesha vizuri.