Nini 787 dreamliner na tugemee nini?

Nini 787 dreamliner na tugemee nini?

Dream liner ni ndege mbovu zilizokataliwa duniani kote. Hivyo ni janga litakalotuletea mabalaaaaa
Aliyelinunua atapata taaabu sanaaa...


Una matatizo ya akili kama Zitto Kabwe, Tundu Lissu na Nape Nnauye….Dreamliner is the best airplane to date haswa kwa masafa marefu. Haina kelele kama ndege zingine kutokana na sound proof yake kuwa the best na iko smooth kwenye turbulences. Mkuu jaribu kusafiri mara kwa mara then uje uandike ukweli, usiwe mpuuzi tu na kupotosha watu wasiojitambua. Kila nchi duniani inataka kuwa na Dreamliner na mashirika mengi yanamiliki Dreamliners. Kama usemavyo wewe ingekuwa kweli kwanini Boeing wana back orders za kutisha juu ya hizi ndege, ni kwa ajili ya mapambo au? Unatakiwa kupewa ban wewe, wapuuzi na wapotoshaji kama wewe msiruhusiwe kutoa comments humu kamwe.
 
Hakuna siasa hapa kaka mfianchi wewe kama una taarifa za kitaalamu kuhusu mauzo na namna ndege hii itakavyotengeneza faida weka hapa. Usi comment tu kuonekana na wewe ume comment weka data hapa tupate faida sote


Dogo huyo mfianchi has a point. Ngoja nikufumbue macho kidogo tu ili ujitambue kiakili...Fikiria hii ndege ikiwa na routes za kwenda India, Mecca, Marekani, Ulaya na sehemu zingine waendazo watanzania kama zile routes za wauza unga wetu enzi za Kikwete (Pakistan, Afghanstan, Uturuki, Ugiriki, China)….abiria badala ya kununua ticketi kwa mashirika mengine wananunua ATCL unafikiri tutakuwa wapi in a year or so? Mtanzania hata kama unawapeleka wazee wako Marekani hauna wasiwasi wa wao kupotea au lugha gongana kwani wako ndani ya ndege yao na wahudumu wanazungumza lugha yao ya asili. Usiwe mwepesi wa kupenda kufumbuliwa kila kitu, tumia akili yako wewe mwenyewe. Unajihaibisha kijana Dharra mpaka unatia kinyaa. Hawa Zitto, Lissu, Nape na Mange wanawalostisha tu kwa sababu wana agenda zao ambazo haziwasaidii nyinyi bali wao tu na familia zao, jitambue dogo. Ni hayo tu.
 
Wana Jukwaa. Ni jana tu tumetoka kushuhudia kuwasili kwa ndege yetu inayoitwa Boeing 787 dreamliner. Wengi wetu nadhani bado hatufahamu kwa kina ni nini hasa kimewasili na mategemeo ni yepi katika kukuza uchumi wa Taifa hili.

Hii ni ndege ambayo imeundwa rasmi na kampuni na Boeing kutoka marekani kwa ajili ya kuruka umbali mkubwa (long haul aka long range) na ina uwezo wa kuchukua abiria kuanzia 242 hadi 335 kutegemea na jinsi utakavyopanga viti. Uzinduzi rasmi wa ndege hizi za dreamliner ulifanyika kwa mbwembwe nyingi mnamo July 8 2007. wadau mbali mbali wa safari za ndege duniani nzima walichangia katika ujenzi wa ndege hizi na mpaka kufika December 15, 2009 Dreamliner ilifanya safari yake ya kwanza na ilipofika mwaka 2011, Boeing walitangaza rasmi kuwa sasa Dreamliner zipo tayari kwa mauzo.

Kufikia October 26, 2011 Shirika la ndege la Japan liitwalo ALL NIPPON Airways walitoa oda yao ya kwanza kununua dreamliner, ndege hizi ziliingia kwenye ushindani rasmi wa kibiashara mnamo August 7 2014 na mpaka kufikia mwezi May mwaka huu 2018 Dreamliner tayari walishapokea oda ya ndege 1,377 nyingi zikinunuliwa na shirika la ndege la Marekani liitwalo American Airlines. Tangu kuundwa kwake na kuanza kuruka ndege hizi zimeshuhudia matatizo kadhaa ikiwemo kuripuka kwa battery (on board fire) wakati zinaruka kibishara. Hio ndio historia fupi ya mgeni wetu huyu dreamliner ambapo imewagharimu Boeing kiasi cha dola za Kimarekani billioni 32 kama gharama za matengenezo.

Kama nilivyoainisha kabla Boeing wamepokea oda zipatazo 1,377, lakini hadi sasa ni ndege 691 pekee ambazo tayri zimefika mikononi mwa wateja tokea kuundwa kwake.

January 8 2013 Shirika la ndege la Japana waligundua uvujaji wa mafuta katika moja ya dreamliner zake, na hivyo kusitisha safari ya kuelekea Boston ghafla wakati abiria wakiwa tayari kwa safari.
January 9 Shirika la ndege la Marekani walilalamika kutokea kwa cheche za moto (wiring problem) karibia kabisa na mahala ilipo battry.
January 13, 2013 ilitokea tena kuvuja kwa mafuta katika moja ya dreamliner.
January 14, 2014, Kuonekana kwa moshi wakati ndege ikiwa angani tena karibu kabisa na mahala ilipo battery. Na kasoro nyingi nyenginezo.

Tutegemee mwanzo mgumu sana. Kuwa na ndege moja inayoruka umbali mrefu (long haul) kuna ugumu wake hasa linapojitokeza suala la technical issues na ikalazimika ndege kutokuruka, kitu ambacho ni cha kawaida sana katika mambo ya ndege, na ndio maana wenzetu Ethiopian Airways wakajenga hoteli zao maalum (ziligharimu Dola milioni 91) kwa ajili ya abiria inapojitokeza kuchelewa kwa ndege kwa sababu za kiufundi (delay) kama hizi nilizoainisha hapo juu, inagwa wenzetu wapo na ndege nyingi za kuwasaidia kuhaulisha abiria na haraka inavyowezekana. Hapo tutegemee Delay, na hili lisipofanyiwa kazi linaweza kutugharimu baadae kibiashara, na pia kujiandaa na kipindi cha matengenezo ambapo ni lazima ndege isafiri (labda Ethiopia) kwa matengenezo ambayo nayo huchukua muda.

Ukifikiria hayo na mengine mengi utaona tuna safari ngumu sana ya kwenda kwa mfano mgeni huyu anatumia lita 6,811 kwa saa, piga hesabu Dar/Mwz ni mwendo wa saa moja na robo kwenda na kurudi masaa mawili na nusu utaona ugumu uliopo katika kuendesha ndege hii. Nilitegemea mapokezi ya kimya kimya na badala yake kutumia muda mwingi kuwaza na kuwazua kutafakari ni kwa vipi mgeni huyu ataleta faida. ITS NOT GONNA BE EASY FELLAS!!!
View attachment 805866
mwalimu jkn alipofariki aliletwa nchini na ndege ya Atc ile ilienda wapi? nani alishiriki kuuwa shirika la ndege nani analifufua kama kweli? mpango kazi ni upi ama mwanunua kwakuwa rwanda wanazo. mme scan mazingira?
 
Mtoa mada katoa angalizo based on facts ya hizo dream liner, suala la kutiana moyo ni la kwako, ila hixo ndio baadhi ya changamoto zake. Ikifanya kwa mafanikio ni sawa, ila ikizingua sijui Makonda atapiga risasi wangapi kwani hizo kelele zake sipati picha.
waliouza za mwanzo zile za nyerere ndo wananunua hizi za sasa! sitashangaa siku wakijenga nyumba mpya umma
 
"mfano mgeni huyu anatumia lita 6,811 kwa saa" hili jambo unauhakika nalo, kutoka USA mpaka TZ itatumia lita ngapi? kwa muda wa masaa 13 hadi 16? mnapoongea muwe na uhakika. unajua hiyo ni Sh ngapi mafuta tu. hapa kunauongo kabisaaa.

Nadhani waliongezewa mafuta wakiwa huko huko angani kwani full tank wangehitaji kung'oa viti waweke tank. 6811X 16=108.976lt. Jamani tusidharau hizi bidii za viongozi wetu.
 
prices-of-boeing-aircraft-by-type.jpg
 
Watanzania kuweni wazalendo na muwache tabia ya kukatishana tamaa kwa kila jambo linalofanyika ndani ya nchi hii.
 
Sababu kubwa na ya msingi, ambayo hata serikali yetu iliishaikubali na kuitekeleza katika zoezi zima la ubinafsishaji, ni kwamba, serikali kazi yake kubwa ni kuhakikisha nchi ina mazingira mazuri ya kufanya biashara, si serikali kujiingiza katika kufanya biashara.

Hususan kwa makampuni ambayo yanaleta hasara.

Ndiyo maana tukabinafsisha mashirika mengi ya umma, CCM wakasema wanataka kubinafsisha mashirika, hususan yaliyokuwa yanaendeshwa kwa hasara.

Cha ajabu wamebinafsisha yaliyokuwa yanaendeshwa kwa faida (NBC, Container Terminal ya Bandari) wakati makampuni yanayoendeshwa kwa hasara kama ATC serikali bado inayakumbatia mpaka leo.

Serikali ya Marekani ilishagundua kwamba biashara ya mashirika ya ndege ni biashara kichaa, ni biashara ambayo serikali ikijiingiza, inajiingiza zaidi kwa kujionesha "na sisi tupo duniani" zaidi ya kufanya biashara yenye faida.

Ndiyo maana wenzetu wajanja wakajitoa katika biashara hiyo kama serikali, wakaachia sekta binafsi ipambane, serikali ikawa imeweka mazingira mazuri tu ya ushindani.

Sisi kwetu mpaka leo tunapiga mark time ya Vienna Waltz, one step forward, two steps back.

Leo tunataifisha, kesho tunabinafsisha, keshokutwa tunataifisha tena!
Muda utasema. Hesabu hazidanganyi. Faida na hasara ni hesabu. Hizi ndege si za raisi, wala hazijaandikwa jina lake. Labda kuna mahesabu ambayo wameyaona wewe huyaoni. Hivyo muda utaongea. Wasi wasi wangu tu ni kwamba kama upo sahihi basi taifa tutakuwa tumepoteza muda na rasilimali. Hope haupo sahihi. Kwangu mm nadhani ubinafsishaji ulikuwa ni kosa.
 
Muda utasema. Hesabu hazidanganyi. Faida na hasara ni hesabu. Hizi ndege si za raisi, wala hazijaandikwa jina lake. Labda kuna mahesabu ambayo wameyaona wewe huyaoni. Hivyo muda utaongea. Wasi wasi wangu tu ni kwamba kama upo sahihi basi taifa tutakuwa tumepoteza muda na rasilimali. Hope haupo sahihi. Kwangu mm nadhani ubinafsishaji ulikuwa ni kosa.
Hata mimi na hope sipo sahihi, lakini maandishi yapo ukutani.

1. Sekta ya ndege dunia nzima iko tricky sana, inahitaji weledi wa hali ya juu kwenda nao, sisi kwa historia yetu ya ATC hatuwezi kusema tumefika hapo. Tulitakiwa kufanya baby steps, kuimarisha technical capabilities, kuimarisha uongozi, kuimarisha viwanja kabla ya kununua midege mikubwa.

2. Tuchukue uzoefu kwa waliofanikiwa, walifanyaje? Nilikuwa namsikiliza CEO wa Ethiopia Airlines anahojiwa na BBC. Akaulizwa, sekta ya usafiri wa anga ni ngumu sana, Ethiopia mmewezaje kufanikiwa hivyo? Akajibu, sababu ni nyingi, ila moja la msingi ni kwamba wataalam tumeachiwa tufanye maamuzi yetu kitaalamu, serikali na wanasiasa hawajatuingilia katika biashara.

Tanzania serikali ya Magufuli haiwezi kufanya hivyo, inaingilia sana wataalamu.

Kama una wasaa na nafasi msikilize mwenyewe hapa (6 minutes clip and worth the insight) --> BBC World News - Africa Business Report, 11/08/2017 GMT, Why is Ethiopian Airlines so successful?

Sisi Tanzania tunafanya tofauti, biashara inaenda kisiasa, maamuzi yanafanywa kisiasa. Serikali inanunua ndege kisiasa. Hata uzinduzi wa ndege ni shughuli ya kisiasa.

3. Midege mikubwa hii inafaa zaidi kwa routes ndefu za kimataifa. Tanzania soko kubwa sana la safari za ndege ambalo halina ushindani mkubwa sana ni safari za ndani. Kwenye safari ndefu, ATC haina advantage ya "economies of scale". Haiwezi kushindana na Wa Ethiopia, Waturuki, Qatar etc. Hatujafikia hata standards za kimataifa za kurusha direct flight from Dar to New York kwa mfano. We are setting ourselves for failure either way. Tukiitumia ndege kubwa kwa safari za ndani hatuwezi kuitumia ipaswavyo, kwa safari za nje hatuna competitive advantage.

4. Ndege hizi zinakuja na mikataba ya matengenezo. Unaponunua ndege kutoka kampuni tofauti tofauti,unakuwa na mikataba na makampuni tofauti tofauti. Sijaelewa logic ya kununua Bombardier halafu pia tukanunua Dreamliner. Hususan kwa shirikadogokama letu. Maana yake tutalipa charges fulani kwa kampuni mbili wakati tungeweza kuwa na "economies of scale" kubwa zaidi kama tunge stick na kampuni moja.

5.Kama manunuzi ya ndege hayajafuata bajeti wala a transparent tender process, sina imani sana na muendelezo wa mradi huu. Tutaangaliaje "cost benefit analysis" wakati hata manunuzi yalivyofanyika hatujui? Nasikia Zitto anaomba mkataba, akifanikiwa kuupata na kutujulisha atakuwa kafanya jambo la maana sana.

Inaonekana, kiujumla, kwamba serikali hainunui ndege ili kumaliza tatizo la usafiri walakutengeneza faida (sehemu nyingi hazina hata viwanja vya ndege vya kuweza kui accommodate hii ndege). Inaonekana serikali inanunua ndege kubwa kwa ulimbukeni wa kujionesha "na sisi tumo, tuna ndege kubwa", bila hata ya kuwa na mipango mizuri ya kuhakikisha shirikala ndege linaweza kujiendesha vizuri.
 
Kama kawaida yetu watanzania,kama kawaida yetu waafrika tuishio chini ya jangwa na sahara kwakweli Tanzania ilikuwa haina haja ya kununua hii Boeing 787 Dreamliner,tulikuwa tunatakiwa tujikite kwa nguvu zetu zote katika kukabili usafiri wa ndege wa ndani(local) ya nchi,kuliko kujingiza katika kutaka kusafiri nchi ya nchi..

Nimemsikia Raisi akisema hiyo Boeing 787 Dreamliner itafanya safari za kwenda India,Thainland nk,hivi kweli ATC inaweza kushindana na mashirika kama Emirates na Qatar mashirika ambayo yamewagaragaza mashirikamakubwa makubwa kama KLM,Lufthansa nk..

Hao watalii wanao wazungumza tulitakiwa tusubiri akina Emirates,Turkish airline,Qatar,Klm na mashirika mengine watumwagia hapa Tanzania,Halafu ATC inawasambaza watalii ndani ya Tanzania kwa ndege zetu,bomberdia ingelifaa sana kwa kazi hiii,mdogo mdogo baada ya kudhidhibiti safari za ndani,tungelianza kusafirisha wasafiri nchi jirani, baadae ndio tungeliamua kufikiria kuruka nje ya Afrika..

Raisi Kakurupuka,ataitia nchi katika hasara,/////Unajua shirika kubwa kama KLM kwa sasa limejikita Zaidi katika safari za ndani za mji kwa mji kuliko masafari marefu ili kuepusha hasara,kwanini ATC isiigie mfano wa KLM!?
 
Hata mimi na hope sipo sahihi, lakini maandishi yapo ukutani.

1. Sekta ya ndege dunia nzima iko tricky sana, inahitaji weledi wa hali ya juu kwenda nao, sisi kwa historia yetu ya ATC hatuwezi kusema tumefika hapo. Tulitakiwa kufanya baby steps, kuimarisha technical capabilities, kuimarisha uongozi, kuimarisha viwanja kabla ya kununua midege mikubwa.

2. Tuchukue uzoefu kwa waliofanikiwa, walifanyaje? Nilikuwa namsikiliza CEO wa Ethiopia Airlines anahojiwa na BBC. Akaulizwa, sekta ya usafiri wa anga ni ngumu sana, Ethiopia mmewezaje kufanikiwa hivyo? Akajibu, sababu ni nyingi, ila moja la msingi ni kwamba wataalam tumeachiwa tufanye maamuzi yetu kitaalamu, serikali na wanasiasa hawajatuingilia katika biashara.

Tanzania serikali ya Magufuli haiwezi kufanya hivyo, inaingilia sana wataalamu.

Kama una wasaa na nafasi msikilize mwenyewe hapa (6 minutes clip and worth the insight) --> BBC World News - Africa Business Report, 11/08/2017 GMT, Why is Ethiopian Airlines so successful?

Sisi Tanzania tunafanya tofauti, biashara inaenda kisiasa, maamuzi yanafanywa kisiasa. Serikali inanunua ndege kisiasa. Hata uzinduzi wa ndege ni shughuli ya kisiasa.

3. Midege mikubwa hii inafaa zaidi kwa routes ndefu za kimataifa. Tanzania soko kubwa sana la safari za ndege ambalo halina ushindani mkubwa sana ni safari za ndani. Kwenye safari ndefu, ATC haina advantage ya "economies of scale". Haiwezi kushindana na Wa Ethiopia, Waturuki, Qatar etc. Hatujafikia hata standards za kimataifa za kurusha direct flight from Dar to New York kwa mfano. We are setting ourselves for failure either way. Tukiitumia ndege kubwa kwa safari za ndani hatuwezi kuitumia ipaswavyo, kwa safari za nje hatuna competitive advantage.

4. Ndege hizi zinakuja na mikataba ya matengenezo. Unaponunua ndege kutoka kampuni tofauti tofauti,unakuwa na mikataba na makampuni tofauti tofauti. Sijaelewa logic ya kununua Bombardier halafu pia tukanunua Dreamliner. Hususan kwa shirikadogokama letu. Maana yake tutalipa charges fulani kwa kampuni mbili wakati tungeweza kuwa na "economies of scale" kubwa zaidi kama tunge stick na kampuni moja.

5.Kama manunuzi ya ndege hayajafuata bajeti wala a transparent tender process, sina imani sana na muendelezo wa mradi huu. Tutaangaliaje "cost benefit analysis" wakati hata manunuzi yalivyofanyika hatujui? Nasikia Zitto anaomba mkataba, akifanikiwa kuupata na kutujulisha atakuwa kafanya jambo la maana sana.

Inaonekana, kiujumla, kwamba serikali hainunui ndege ili kumaliza tatizo la usafiri walakutengeneza faida (sehemu nyingi hazina hata viwanja vya ndege vya kuweza kui accommodate hii ndege). Inaonekana serikali inanunua ndege kubwa kwa ulimbukeni wa kujionesha "na sisi tumo, tuna ndege kubwa", bila hata ya kuwa na mipango mizuri ya kuhakikisha shirikala ndege linaweza kujiendesha vizuri.
Maelezo umeyapangilia vzr! Na changamoto ulizoorodhesha zina uhalisia. Ila kama sijakosea(correct me if am wrong) maelezo ya raisi ni kwamba shirika la ndege inabidi lifufuke ili kukuza sekta ya utalii. Badala ya watalii kutumia ndege za inchi zingine basi watumie za kwetu. Ndo maana nkasema, hesabu hazidanganyi. Mi suala la muda tu. All in all JPM asingenunua ndege angepoteza nini? Na hizi ndege ni za nchi, yeye ataondoka madarakani ataziacha. Labda shirika lijiendeshe kwa hasara life kama mwanzo. narudia tena, hesabu hazidanganyi. Muda utaongea
 
Maelezo umeyapangilia vzr! Na changamoto ulizoorodhesha zina uhalisia. Ila kama sijakosea(correct me if am wrong) maelezo ya raisi ni kwamba shirika la ndege inabidi lifufuke ili kukuza sekta ya utalii. Badala ya watalii kutumia ndege za inchi zingine basi watumie za kwetu. Ndo maana nkasema, hesabu hazidanganyi. Mi suala la muda tu. All in all JPM asingenunua ndege angepoteza nini? Na hizi ndege ni za nchi, yeye ataondoka madarakani ataziacha. Labda shirika lijiendeshe kwa hasara life kama mwanzo. narudia tena, hesabu hazidanganyi. Muda utaongea
Unasema hesabu hazidanganyi, ni kweli. Mimi pia nakubali hesabu hazidanganyi.Ingawa uhasibu na takwimu vinaweza kudanganya vizuri tu.

Tatizo JPM haheshimu hesabu, uhasibu wala takwimu, anaendekeza siasa.

Angeheshimu hesabu na uhasibu, angenunua ndege kwa hela za bajeti na kwa tenda iliyo wazi.

Ushajiuliza, kwa nini hakununua ndege kwa hela zilizopitishwa kwenye bajeti?

Sasa hivi inawezekana katupiga mamilioni ya dola humo na hakuna anayejua, kwa sababu kama nilivyosema, manunuzi yamefanyika nje ya bajeti na kwa kificho.

Na hata kama hajatupiga, kanunua kwa moyo mzuri tu, that is even worse. Ameacha wanaomsema wapate mwanya wa kusema kanunua ndege bila kufuata bajeti. Kwa sababu gani?

Hutakiwi kusema hesabu hazidanganyi wakati hata bei ya kununulia ndege ni ipi na mikataba ya matengenezo inaendaje hujui.

Ukitaka kuja kuangalia baada ya mwaka kama ndege inaenda kwa hasara au faida na Return On Investment tutarudisha lini, utapigaje hiyo hesabu?


Umeongelea habari nzima ya kufufua utalii.

Tatizo siasa nyingi bila nia ya kweli.

Tanzania tumeweka VAT kwenye utalii, tumewanyanyasa watalii mpaka ambao walishafanya booking na kulipia ikabidi walipe tena, with hardly a weeks notice, wakati wao malipo walishafanya kabla VAT haijawekwa.Juzi nimeona picha moja horrible reviews za airport yetu ina trend instagram. Huwezi kuvutia wataliikwa ndege nzuri halafu uwanja wa ndege choo mgogoro, huduma mbovu

Serikali yenyewe inaharibu utalii kwa kupandisha kodi kwa namna ya ajabu kwa muda mfupi bila hata taarifa nzuri na mpangilio, halafu inatakakupandisha utalii kwa kununua ndege?

Hao watalii wa kimataifa ndege washaziona sana hizo, kitu cha kufanya kuvutia utalii ni kuongeza huduma nzuri kwa watalii na kama kuna kupandisha kodi, kufanyike gradually, sio 185 at a go.

Soma chini hapo uone utekelezwaji mbaya wa VAT kwenye utalii ulivyoharibu utalii Tanzania.

Tanzania VAT hike sends safari industry into pandamoneum

Upheaval in the Safari Industry As the Impact of New Tanzania Vat Tax Starts to Bite – SafariBookings

New tourism tax roils Tanzania safari industry: Travel Weekly

Is VAT causing tourists to pick Kenya over Tanzania? see link --> {{title}} Tourism Update
 
Maelezo umeyapangilia vzr! Na changamoto ulizoorodhesha zina uhalisia. Ila kama sijakosea(correct me if am wrong) maelezo ya raisi ni kwamba shirika la ndege inabidi lifufuke ili kukuza sekta ya utalii. Badala ya watalii kutumia ndege za inchi zingine basi watumie za kwetu. Ndo maana nkasema, hesabu hazidanganyi. Mi suala la muda tu. All in all JPM asingenunua ndege angepoteza nini? Na hizi ndege ni za nchi, yeye ataondoka madarakani ataziacha. Labda shirika lijiendeshe kwa hasara life kama mwanzo. narudia tena, hesabu hazidanganyi. Muda utaongea
Mkuu kweli watalii watapanda ATC waiache Qatar na Emirates na mashirika mengine ya kimataifa,kwanini Raisi asijiimarishe Zaidi katika ndege za matumizi ya ndani ya nchi,ndege zinazokwenda masafa mafupi,..kama vile Bombardier!?
Magufuli akiondoka si na Hiyo Boeing itakuwa iko juu ya mawe,nani atalipia matengenezo ya hiyo ndege kama ndege inatembea kwa hasara..
 
Back
Top Bottom