Ningependa Tundu Lissu apokelewe hivi

Ningependa Tundu Lissu apokelewe hivi

Ingekuwa na faida zaidi angerudi kipindi kile kuwatumikia wananchi wake walipokuwa wanamuhitaji ilihali sasa anarudi kama mzigo!

Sio wakati ule, mpaka sasa wananchi wake wanamkubali na wataendelea kumkubali, hata kama jiwe kwa kumtumia kibaraka wake nduguyai kutaka kumtenga na watu wake. Tuko wananchi kibao tunamkubali na ukitaka kuamini jiwe akosee kufanya uchaguzi huru, hataamini macho yake.
 
Danganyaneni watu wanataka kula hell kwa kisingizio Cha mapokezi ya mtu ambaye haji.Kaomba ukimbizi.Watu mtapigwa pesa kwa kuuziwa T-shirt vitenge nk kea ujio hewa wa mtu. Kila mtu achunge mfuko wake

Nilidhani hizo t-shirt na vitenge watu wananunulishwa kwa lazima kumbe ni mapenzi yako tu. Unatamani asirudi ili Magufuli uchaguzi wa 2020 ashindane na Dovutwa tu?
 
Sipati picha siku anarejea kwani vyombo vya dola vitatumika kufanyia watu ukatili ili kuhakikisha hapati mapokezi yenye kuvuta hisia, kwani wanaamini mwenye ruhusa ya kuvutia watu ni jiwe tu.
Hana issue yoyote mnampa promo isiyomsaidia chochote. Mchovu tu kama wachovu wengine. Muacheni auguze maguu yake
 
Taarifa za kiintelijisia hakutakuwepo na usalama kwa hiyo maandamano ya kumpokea Lissu hayatakuwepo.....kisingizio hicho hakitakwepeka
Watu wataandamana lije jua..ije mvua
 
Kwa mtazamo wangu sidhani kama ni busara sana kwa Lisu kurudi nchini kipindi hiki.Nafikiri ni si wakati sahihi sana kwake kurudi nchini.Ukizingatia aina za viongozi tulio nao wakati huu.Si wakati sahihi kwake kufanya harakati yoyote.
Kwahiyo aendelee kupigwa baridi tu huko ughaibuni?
 
Sipati picha siku anarejea kwani vyombo vya dola vitatumika kufanyia watu ukatili ili kuhakikisha hapati mapokezi yenye kuvuta hisia, kwani wanaamini mwenye ruhusa ya kuvutia watu ni jiwe tu.
Bora hata Oscar Kambona alitinga nchini mwaka 1992 na bahasha iliyojaa makaratasi kibao toka UN kama kinga, baada ya kukaa miaka 25 ya exile.
Sielewi Kama historia itajirudia tena!
 
Atapokelewa na wanamtandao huku mtandaoni... nani apoteze muda wake kwenda kumpokea msaliti wa nchi.
Masikini wa Mungu, kama ungejua wapo watu, pamoja na kuwa na madaraka makubwa na ulinzi wa nguvu, hofu imewajaa na hawalali kwani kila wakijaribu kufumba macho wanamuona Mh. Lissu huyo kawakodolea macho! Wanapanga na kupangua watumie njia gani Mh. Lissu asikanyage ardhi hii na ikitokea kweli akakanyaga wamdhibitije? Watake wasitake, Mh. Lissu atarudi nyumbani na hilo hawawezi kuzuia ila watafanya kila wawezalo kuzuia hiyo tsunami ya ujio wake...swali linalowaumiza kichwa ni namna ya kuzuia tsunami.
 
Bora hata Oscar Kambona alitinga nchini mwaka 1992 na bahasha iliyojaa makaratasi kibao toka UN kama kinga, baada ya kukaa miaka 25 ya exile.
Sielewi Kama historia itajirudia tena!

Kambona na Lisuu ni watu wawili tofauti. Kambona alikimbilia ukimbizini, Lissu kaenda ulaya kwa ajili ya matibabu. Lisu hajawahi kukimbia nchi na hatakaa akimbie.
 
Lissu Msaliti wa nchi

Hivyo ndivyo jiwe anavyotaka tuamini, lakini kwa bahati sana wananchi sasa hivi ni digital tuna ufahamu mpana, yeye na genge lake ndio wamebaki analogue hivyo asidhani tunasubiri yeye ndio atauambie nani ni mzalendo na nani ni msaliti. Kwahili amechemsha maana tulishaamka zamani.
 
Hivyo ndivyo jiwe anavyotaka tuamini, lakini kwa bahati sana wananchi sasa hivi ni digital tuna ufahamu mpana, yeye na genge lake ndio wamebaki analogue hivyo asidhani tunasubiri yeye ndio atauambie nani ni mzalendo na nani ni msaliti. Kwahili amechemsha maana tulishaamka zamani.
Eti digital wakati wewe ni zero brain kwenye digital yenyewe ila ni operator tu wa digital!
 
Vipi Yule dereva?naye anarudi?Au anaendelea na masomo?Akija tunamkamata asaidie upelezi hii kesi haijafungwa
Andaa majibu ya haya maswali 2 tu.

1. Walinzi walikuwa wapi wakati wa shambulio?
2. Kwa nini Kalemani alizitoa CCTV na kuzificha anakojua yeye?
 
Atapokelewa na wanamtandao huku mtandaoni... nani apoteze muda wake kwenda kumpokea msaliti wa nchi.
Na kuconfirm hili,intelijensia iwe kimyaaa,maana wakijaribu tu kuhangaika nae watadroo atension ya watu kumpokea. Mwenyekiti wa ulinzi na usalama mkoa wa Dar abaki kimya ili watu hata wasihangaike na ujio huu.
Kweli kabisa janaa hata hajulikani kwa sasa,kaishaaa kamalizwa na kasi ya namba moja!
 
Back
Top Bottom