Ningekuwa sina ajira ningefanya jambo moja ambalo lingenipelekea kuajiriwa haraka na kwa urahisi

Kiboko ya Jiwe

JF-Expert Member
Apr 7, 2020
12,702
36,129
Hii njia ambayo nitaianika hapa si njia rasmi na si njia ya kuweza kutumiwa kichwakichwa. Hakikisha suala la ajira na sifa kedekede unazitupa mbali, let's say vitakuja automatically.

Ningefanya upelelezi kwa kina, ningeweza hata kufanya jambo kwa muda wa mwaka mmoja ili nikusanye taarifa za kweli na uhakika.
Ningefuatilia mtandao mmoja wa ujambazi kwa kina nipate details zao zote.
  • Ningemjua mkuu wao
  • Center yao kuu
  • Wanapoficha silaha
  • Idadi kamili ya genge lao
  • Muda na wakati wanaofanya matukio n.k, n.k
Kisha naandika barua kwa OCD, RC au kwa Afisa usalama wa wilaya au mkoa kuhitaji kuonana naye. Najua katika watu ambao hawakatai meeting na raia ni watu wa ulinzi na usalama.

Unaweza kutaka kuonana na meneja mkoa TANROADS au dawasa ukazungushwa miezi na miezi ila kwa upande wa ulinzi na usalama haiko hivyo.

Siku nikikutana naye namweleza kukereka kwangu na vitendo vya uhalifu nchini hivyo kwa mapenzi ya dhati nimejitolea kuchunguza uhalifu kama jitihada za kusaidia dola.

Nitampa fuul information za hilo genge.

NB: Mweleze hatua hadi hatua ulizopitia katika investigation yako ili kumwondolea mashaka juu yako asije kuhisi ulihusika kwa namna moja au nyingine.
 
Hakuna jambazi mpumbavu kama unavyofikiria.

Ukifanya hivyo utauawa ndani muda mfupi tu.

Hakuna jambazi asiye na connection na viongozi wa polisi.

Ndio maana ukitaka kuzuia ujambazi, waite hao viongozi wa polisi WAPIGE BITI.

Matapeli tu wa magari wana net work mpaka central huko, sembuse jambazi wa bank.

Labda unaongelea vibaka kama panya road
 
Unapoenda kuonana nae hakikisha ndugu zako wanajua mana utawekwa ndani ili kusaidia upelelezi mpaka hao majambazi wapatikane. Lakini pia majambazi sio wajinga kiasi hcho mpaka wakupe details zao zote hzo.
 
Hakuna jambazi mpumbavu kama unavyofikiria.

Ukifanya hivyo utauawa ndani muda mfupi tu.

Hakuna jambazi asiye na connection na viongozi wa polisi.

Ndio maana ukitaka kuzuia ujambazi, waite hao viongozi wa polisi WAPIGE BITI.

Matapeli tu wa magari wana net work mpaka central huko, sembuse jambazi wa bank.

Labda unaongelea vibaka kama panya road
Soma hiki kisa cha ukweli hapa chini ili upate picha ni kwa namna gani hayo majamaa yana OPERATE shughuli zao 👇👇👇
Nimeamua kuandika hii thread kuwatahadharisha mnaonunua magari ktk show rooms kuwa makini yasije kuwakuta kama yaliyonifika mimi .

Nilichukua mkopo Benki moja kwa ajili ya kuendeleza na kukuza kazi yangu.

Nikaenda na pesa ktk showroom moja ipo mtoni kwa Azizi Ally jirani na petrol station na ofisi ya CCM wkt huo nilishakwenda kabla siku 5 nyuma nikachagua gari niliyoridhika nayo nilipochukua mkopo ndipo nikatinga na pesa cash nikiongozana na jamaa zangu 2 nikamkuta mhusika mmoja kati ya 3 nikafuata taratibu za mauziano nikapewa risiti card original na mkataba nikaondoka na gari yangu.

Cha kushangaza yule aliyeniuzia aliniuliza hii gari unaipeleka mkoa gani? Nikamwambia umeniuzia gari hakuna haja ya kujua gari inaenda wapi.

Basi nikaenda na hiyo gari yangu siku hiyo nikaipark nyumbani kwangu. Kesho yake nikatoka nayo saa 7 mchana kwenda nayo Magomeni kuifanyia service ili ianze kazi kweli nikamaliza service nikaenda magomeni Kagera kula.

Nikiwa nakula akaja jamaa mmoja simfahamu akanigusa bega akaniambia wewe ndiwe mwenye ile gari pale nje? Nikamjibu ndio akasema ukimaliza kula nina shida na wewe.

Cha ajabu nilipotoka nje nikakuta pembeni ya gari yangu kuna defender la polisi kuna askari 8 nikapigwa bao la mgongoni nikaambiwa kaa chini tulikuwa tunakutafuta mwizi wewe nikawauliza nimeiba nini?

Hawakutaka kunisikiliza wakaninyanganya funguo ya gari polisi mmoja anaendesha na mimi nimewekwa nyuma nakindwa na polisi 2 mwendo tuliotoka nao pale Kagera kwenda central ni kama jambazi sugu linapelekwa kituoni.

Kufika central nikapandishwa juu ghorofa ya pili kama sikosei kitengo cha magari (siyo trafic) ni central kwenyewe. Tulipoingia ndani juu sasa napelekwa mzobemzobe nikaingizwa ktk chumba ni ofisi kulikuwa na afande mmoja tu hapo ni saa 11:30 jioni, wale askari wakasema afande tumemkamata mwizi wa lile gari ndio huyu.

Nnikaambiwa kaa chini nikatii, yule askari akiyekuwepo ofisini akawaamuru wanipeleke jela shimoni. Mimi nikajitetea siyo mwizi nimenunua hii gari kihalali na documents zote ninazo hapa, wakazichukua nikamwambia lkn kwanini msiende kumkamata aliyeniuzia gari ktk kunitendea haki? Akasema ok nendeni mkamlete aliyemuuzia.

Nikapandishwa ktk defender mpk mtoni kwa Azizi Ally bahati nzuri tunafika tu yule alieniuzia ndio alikuwa anajiandaa kutoka wakamchukua tukarudi tena central .

Yule askari akasema wapeleke jela nikajitetea maana mambo ya jela sijawahi maishani mwangu kuingia kkn wapi. Kufika chini tukajiandikisha nikamsikia askari mmoja anasema wafungie VIP kuna chumba jirani tu na hapo tulipopokelewa kabla ya kuingia jela.

Niligundua yule jamaa na wale maaskari wanafahamiana, tukalala ktk hicho chumba cha vip ilipofika saa 11 alfajiri akaja askari akatufungulia tukapekekwa shimoni ili mkaguzi akija atukute kule, tukakaa mpaka saa sita kasoro mchana majina yakaitwa tukatoka shimoni tukaenda kutoa maelezo.

Mungu mkubwa nikatoka kwa dhamana saa 8 mchana. Tukaambiwa kesho yake tufike pale saa 1:30 asubuhi na ikawa hivyo cha ajabu yule polisi aliyetuamuru mwanzo kabisa nipelekwe jela akamuuliza aliyeniuzia gari umeniletea pesa yangu hakumjibu kitu.

Asubuhi ile nikakuta ile gari yangu haipo pale ilipoegeshwa sijui ilipelekwa wapi mpaka leo kumbe wale jamaa wa ile showroom ktk kujitetea kutokanana na utapeli wao wakasema ile gari kuna mtu alienda pale showroom ana shida ya pesa wakamkopesha akaacha gari yake hiyo niliyoinunua mimi kama bond vile kwa hiyo hiyo gari imekaa siku nyingi wakaamua kuiuza ili warudishe pesa zao.

Wakati nahangaika kwenda pale polisi kila siku kupigania haki yangu kumbe wale jamaa wa showroom walikuwa na kesi nyingine za magari mengine 2 aliyeuziwa gari moja ni askari mwenzao alikuwa Arusha wakawalazimisha wale jamaa wa ile showroom matapeli warudishe pesa za ile gari ya askari mwenzao wa Arusha na wakafanya hivyo mimi wakaniambia nikafungue kesi mahakamani .

Nikafungua kesi Temeke lkn kumbukeni pesa ni ya mkopo bank natakiwa irejeshwe kila mwezi, nikatoa taarifa bank wakaniambia wao hawatambui wanachotaka ni pesa tu.

Nilikuwa na wkt mgumu sana nitarudishaje peza za bank kitendea kazi sina na sijui gari ilienda wapi. Wale matapeli waliposikia nimeenda Mahakamani wakapeleka pesa kiasi polisi Changombe kwa maana wanaanza kunilipa kidogo kidogo sikuwa na jinsi nilipata mateso makubwa mpaka nyumba yangu ikataka kuuzwa kazini nikaingia madeni mamilioni lkn Mungu alinipigania.

Ilifika siku niliamua ninunue petroli lita 30 niweke ktk gari yangu ndg ili nikifika ktk ile showroom niilipue gari ili kama kukosa tukose wote lkn sauti ikaniambia acha kufanya hivyo

Nawashauri kuweni makini na hizi showrooms. Nyingine sizihukumu ila ile ya Mtoni kwa Azizi Ally jirani na ifisi ya CCM mtalizwa.

Hawa jamaa walinisababisha maisha yangu na familia yakawa magumu
 
😀😀 Wazo lako ni zuri lakini halitekelezeki hapa Puerto Rico ninapoishi mimi na wewe, hayo mambo yapo kwenye movies za Magharibi huko.
 
Hakuna jambazi mpumbavu kama unavyofikiria.

Ukifanya hivyo utauawa ndani muda mfupi tu.

Hakuna jambazi asiye na connection na viongozi wa polisi.

Ndio maana ukitaka kuzuia ujambazi, waite hao viongozi wa polisi WAPIGE BITI.

Matapeli tu wa magari wana net work mpaka central huko, sembuse jambazi wa bank.

Labda unaongelea vibaka kama panya road
wa magari umeenda mbali hao wa simu tu wana connection huko huko
 
Back
Top Bottom