Ninakwenda mafunzo ya JKT...

Status
Not open for further replies.

Mhh.........! "samaki mkunje angali mbichi"@mkeshaji
 
Shemeji wiki 3 jeshi gani hilo,sisi kwata pekee tilipiga miezi 6,ukirudi sidhani hata kulenga shabaha utakua umefuzu.
LAKINI bora umejiwahi maana nasikia huko mjengoni,toka mtuondolee tamthilia ya LIVE, NGUMI ZIMERUHUSIWA,
 
Kwenye hiyo course itapendeza kuwe na mafunzo ya nidhamu kwa viongozi wa umma na maadili: 1.kama kiongozi anavyopaswa kuchagua maneno ya kuongea mbele ya wananchi.
2. namna ya kiongozi anavyopaswa kuonyesha utimamu wake wa akili kwa kila sentensi atakayoongea mbele ya wananchi.

Naamini baada ya wewe kutoka kwenye course husika ndio utakuwa mda muafaka wa wewe kuja hapa na kunena hapa tupime kama course husika inasaidia ama ni matumizi sayiyo na lazima.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 


Uwe unakuja hapa mara kwa mara mkuu kutoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali yahusuyo chama na hata serikali unayoisimamia... viongozi wengi wa chadema wanajitokeza sana hapa lakini nyie CCM hamuonekani na jukwaa la siasa hujadili sana mambo ya ccm.
 
Ila ukumbuke kwamba huko huwa hakuna hayo mambo yenu ya fitna kaka , Ni kurushwa Kichura tu kwa kwenda Mbele ! Usisahau ile Skafu yako mkuu .
 

You Nail it Mkuu!!!
 
Barua imeonesha muda wa kuanza tu ila najua sio mwaka mmoja ni kipindi kisichopungua wiki tatu wala si zaidi ya miezi mitatu

Huo ni MGAMBO na sio JKT........OMBA UPIGE MWAKA UTAKUWA MZALENDO MZURI KAMA SISI......na urudi umepauka kama sisi

 
Nilikuwa nashangaa sana Mbona wewe muonekano wako uko kizarendo lakini matendo yako si hivyo. Unamapenzi sana kwa Chama chako cha CCM na sio Mzarendo kwa taifa lako. Nilishindwa kubainisha kuwa haukupitia JKT.

Nenda kale kwata bwana.

 
Mwigulu,
Unakwenda JKT kwa wiki tatu kwa mujibu wa sheria au kutalii tu! Sheria ya JKT imebadilishwa ili ikidhi hadhi, madaraka na vyeo mlivyonavyo? Zamani aliyekuwa akikwepa kwenda JKT kwa mujibu wa sheria alishtakiwa na kufungwa kisha akimaliza kifungo anapelekwa huko JKT kwa mwaka mmoja. Mmeichakachua sheria hii?
 
Huyu jamaa ni hatari sana, ka engineer kumwagia mtu tindikali sasa anatembea naye kama maonyesho, hajisikii vibaya.

 

Nchemba, kwa kwenda JKT hufanyi kigeni isipokuwa kutekeleza Sheria ya JKT, Ujue kuwa wenzako tushapitia huko miaka mingi iliyopita na wala hatujapitia huko kwaajili ya Chama fulani bali ilikuwa Sheria ya nchi, kumbe wewe kama unaenda kwaajili ya chama chako sidhani kama sera ya JKT ipo katika ccm labda mgambo na chipukizi. Nenda JKT kwavile hukwenda huko baada ya kumaliza Kidato cha sita, na wewe si wa kwanza kuna maofisa kibao tulikuwa nao nyakati hizo ambao hawakupitia JKT waliletwa na walifuata mafunzo ya JKT. Jambo moja nakuhakikishia , kama Jeshi bado liko kama lilivyokuwa nyakati zetu, utarudi ukiwa tofauti kabisa na ulivyo sasa, utabadilika kifikra hata kimtazamo. Nakutakia mema huko ila kumbuka huko hakuna cha kada wala Mbunge, ukuruta ni kwa wote.
 
Ila ukumbuke kwamba huko huwa hakuna hayo mambo yenu ya fitna kaka , Ni kurushwa Kichura tu kwa kwenda Mbele ! Usisahau ile Skafu yako mkuu .

Lakini kama vile PoliCCM jeshi nalo si JeCCM? Hivyo Chemba atabweda tu!!
 
matendo yako haviendani na kisomo chako,nenda kajifunze na uache kuropoka hovyo!!
 
Huo ni MGAMBO na sio JKT........OMBA UPIGE MWAKA UTAKUWA MZALENDO MZURI KAMA SISI......na urudi umepauka kama sisi

Umenikumbusha mbali sana,wiki 52 (mwaka) si mchezo. Na ile miezi sita ya mwanzo mawasiliano ya ubongo na viungo vya siri huwa yanakatika kabisa hata uone nini hushtuki.
 
Umenikumbusha mbali sana,wiki 52 (mwaka) si mchezo. Na ile miezi sita ya mwanzo mawasiliano ya ubongo na viungo vya siri huwa yanakatika kabisa hata uone nini hushtuki.

Imagine jama anaenda kwa wiki tatu kama sio utani na dharau ni nini? Three weeks atapewa "uchele" huyu?
 
Kama kabla ya kwenda ndio wewe huyu hivi ukirudi tena mjeshiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii????????????. Natamani na mimi kwenda ili nipate ukakamavu wa kupokea amri za kijeda. Hongera kwa maamuzi naamini hutarudi kama unavyoenda.
 

Napata hofu kwa mtu kama wewe usiyekuwa na uvumilivu wa kisiasa utakuja kurusha ngumi bungeni na pia utakuwa kero kwenye mikutano ya upinzani na vijana wako wanaitwa green guard....sijui ngoja tusubiri siasa za ulingoni sisi ngoja tuendelee na kung fuu na karate za mtaani hizi zitatuweka salama siku moja for self defence.
 
Huo ni MGAMBO na sio JKT........OMBA UPIGE MWAKA UTAKUWA MZALENDO MZURI KAMA SISI......na urudi umepauka kama sisi

Ni kweli wanakwenda kujifunza mgambo na kuvimaliza visichana vilivyomaliza kidato cha sita mwaka huu kwa posho na mishahara yao ya kibunge. Ikiwezekana mkuu wa JKT awatengee kambi yao wenyewe watalii hawa wa ndani.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…