Kipenzi Chao
Member
- Oct 12, 2010
- 99
- 4
Jamani nimekuwa na my wife, ambaye tumekuwa tukiishi vizuri sana, japo kama ilivyo kawaida katika maisha tumekuwa tukipishana hapa na pale na baadaye tunarudi vema kabisa.... Lakini kikubwa zaidi ni kwamba nimekuwa na nyumba ndogo ambaye my wife hakuwahi kuijua...! Juzi nyumba hii ndogo imenipiga kibuti kikali sana, kitu kilichonipelekea kuumia sana moyoni hadi my wife anashtukia siko sawa....! Sasa nahitaji kupewa faraja juu ya kibuti hiki na wakati mgumu inayonikabili sasa....! Nafahamu fika kuwa ni vigumu mtu kunifariji bila kufahamu vema tatizo linalonikabili....! Sasa nauliza; je hali hii ngumu nimshirikishe my wife, au niitafutie nyumba hii ndogo naye msaidizi?