Imamu wa Msikiti Mkuu wa Ijumaa Mkoa wa Arusha, ametoa tamko kuhusu mgogoro unaofukuta ndani ya Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), mkoani hapa na amewaasa vijana wa Kiislamu wanaojihusisha katika mgogoro huo kujitoa.
Aidha, amewaasa Watanzania kwa ujumla kutokubali kutumiwa na chama cho chote ili kuleta vurugu nchini.
Imamu huyo, Muhammad Said Hambal, alisema hayo kufuatia mgogoro uliopo ndani ya UVCCM ambao umedhihirisha kuwepo kwa makundi mawili yanayotumiwa na baadhi ya mafisadi.
Alisema kuna baadhi ya watu aliowaita kuwa ni mafisadi wanawatumia vijana kuleta vurugu kwa malengo wanayoyajua wao na akaonya kuwa hali hiyo ikielendelea inaweza kuleta machafuko makubwa katika jamii.
Ndani ya CCM kuna vijana wanaonyesha mpasuko wa wazi nawaasa vijana wote wa Kiislamu kuacha, wajitoe katika vurugu hizo mkoani hapa, alisema.
Imamu Hambal alisema vijana hao wanafahamika na akaahidi kwenda kuwaona kila mmoja binafsi kuwaasa wajiondoe katika mgogoro huo.
Alisema hivi karibuni kumekuwa na madai yanayotolewa na baadhi ya vijana ndani ya umoja huo wakitishia kuchoma moto jengo la makao makuu ya CCM mkoa.
Ofisi ya CCM ni mali umma, sasa ikichomwa moto wataleta madhara sisi hatutaki madhara, na ndio maana tunakemea vurugu zozote, alisema.
Alisema wamepata madhara makubwa katika maandamano yaliyoandaliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), yaliyofanyika mapema Januari mwaka huu ambapo watu watatu waliuawa na polisi kwa risasi.
Tumepata madhara makubwa katika maandamano yale ya Chadema, hilo ni funzo na tusingependa mambo haya yatokee tena, wengi walioathitika ni Waislamu, alisema na kuongeza, waathirika wa mabomu walikuwa wa hapa mjini kati ambao pia mali zao ziliharibiwa na nyingine kuibwa.
Akizungumzia hatua ambazo watazichukua iwapo watakaidi, Imamu Hambal, alisema wataenda kuwaona wazazi wao na kama itashindikana wataacha.
Hata hivyo, alionyesha matumaini kuwa vijana hao hawatakaidi tamko lake pale aliposema, kila muumini anatakiwa kuwatii viongozi wake na kama hawatatii sisi tutawaacha.
Alisema CCM ni chama kikubwa na kama kuna kasoro basi wakae chini na kuzitafutia ufumbuzi badala ya kukaa kimya na kuwapa faida mafisadi kuwatumia vijana kwa lengo la kuleta vurugu.
Kwa nini baadhi yenu mnapenda sana kudharau Madrasa au elimu ya Waislaam kwa ujumla?
Kwa nini baadhi yenu mnapenda sana kudharau Madrasa au elimu ya Waislaam kwa ujumla?
madrasa haina mpango,mnasoma kuongea maneno mengi saaaana,kichwani hamna kitu,,imagine watanzania wote tusome madrasa itakuwaje
Mimi sio Mwanachadema na sio chama chochote, ila nimpenda mabadiliko. As far as your thread is concerned, they say "No research, no right to speak". I am not well clear on how you reached your conclusion. Probably you need to tell us, how was that research conducted, including the unit of analysis, sample size and sampling technigues. Was is stratified to make sure that both stratas within CHADEMA in terms of belief taken care? Did you you test the hypothesis also in other parties like CCM, NCCR Mageuzi, CUF, TLP, non part allied, etc such that you also have the feelings how the members perceive Madrasa education and related education, and why do they feel so that you differentiate them from CHADEMA? Again, did you trace the historical situation to understand how has it been the situation before. Remember that, multiparty system and so did CHADEMA came in for the first time in 1992. Now did you trace back to see how was the situation before? I think to have a good conclusion go through the advices I have aired down. It is my personal advice.
Research gani wewe? acha porojo. kila siku hilo neno naliona humu kama ninavyona neno m.kwere na wala hakuna anayebugudhiwa nalo.
Itakuchukua muda kuelewa Mkandara, watu walishaelewa siku nyingi saana. Na ndio maana jitihada ufanyazo za kuhakikisha JF inakuwa balanced hazifanikiwi. Tumeshafika point of no return, sasa next stage hatujajua itakuwaje? Maana impact yake ni kwenye vyama. Na hii hali ipo JF kuliko hata mtaani. Mitaani watu wanaheshimiana na wanajua karibu kila mtu ana nduguye aliyopo upande mwengine kwahiyo heshma inaendelea kuwepo. Yaani strategy ya divide and rule hapa imefanikiwa saana.Kwa nini baadhi yenu mnapenda sana kudharau Madrasa au elimu ya Waislaam kwa ujumla?
Kwa nini baadhi yenu mnapenda sana kudharau Madrasa au elimu ya Waislaam kwa ujumla?
Kwa nini baadhi yenu mnapenda sana kudharau Madrasa au elimu ya Waislaam kwa ujumla?