Nina swali kwa WanaChadema

Elimu ya fitna! Unaijua wewe!ULIMLINGANISHA SHEIKH NANI na Padre au Askof yupi? Ila upo shalow hata kimawazo mpwa wangu. Unajua ndo mana Maadil yanaharibika kwakua 2naendesha ulimwengu kwa utash zaidi ndo mana mnapenda ushabiki,ulimwengu unajinsi ya kuuendesha kwa jins aliye tuleta duniani ame2andalia na co mpaka papa atoe kichwani kwake.hauwez kuzitenganisha kanisa chadema hata kwa elimu ya biblia ambayo hujui hata imeundwa na nani na kwanini?soma na wewe kaka inaonekana unakaelim kako hakanamsada sana na wewe matokeo yake unaka2mia vibaya.
 
Heshima mkuu Mkandara.
Nimesoma michango yako kwenye hii thread yako kuna hoja nyingi za ujenzi umeziongea, kuhusu baadha ya wana Chadema kudharau mafundisho ya dini ya Kislam na kutumie neno Madrasa kama kejeli kwa Waislam, kama utasoma Al nuur ukakutana na kitu kimekuudhi halafu ukaja JF, ukaanza kukejeli Waislam wote ukagongewa Thanks ukadhani unawakoga Waislam kumbe ujui hizo kejeli zako zinazidi kukipaka matope Chadema sababu, kuna baadhi ya wana Chadema JF, kila siku wanawatoa Waislam ndani ya Chadema kutokana na kejeli zao dhidi ya Waislam, uwezi kuwakejeli Waislam sababu ya JK, kuna Waislam wengi tu awamkubali JK, ata kama ni Muislam mwenzao
Mkuu wangu imefikia mahala tuzungumze ukweli na sii kuatfuta kuwapendesha Waislaam/ Wakristu CCM au Chadema bali ukweli toka ktk nafsi zetu ndio utahesabika ktk ujenzi wa Taifa hili.

Umezungumzia Redio na gazeti la Alnoor, hivi hawa jamaa wanarusha matangazo yao toka wapi na who owns it..naomba kufahamishwa kabla hatujaendelea maanake ndio utaratibu tunaoutumia hapa JF kuzungumzia magazeti au redio zinginezo..Na mkuu wangu this is not about Chadema bali wanaChadema ambao tumekubali kubeba mabango pasipo kujua chama kinasimamia maswala gani.

Hivi kweli kwa sababu ya JK kuwa Muislaam na redio sijui gazeti la Alnuur ndio sababu ya dharau kwa Waislaam wote! Na kama ulivyosema wapo Waislaam Chadema hivi hawa watu hawaoni kama ni aibu kubwa kuwadharau waislaam kwa ujumla wake kwa sababu tu ya gazeti la Alnuur ambalo halina mahusiano na CCM wala waislaam wote?..
Na labda niwakumbushe tu kwamba wakati JK anaingia madarakani tulihoji sote hapa fedha za misaada toka Iran na Libya mbona hatukuona ubaya wowote hali ni haki yetu ya kimsingi kujua mahusiano baina ya fedha zile..Hatukupewa jibu lakini sidhani kama kuna mtu alijibu kwa dharau ya elimu ya wakristu na kuifanya hii kuwa agenda ya Wakikristu..Leo tunahojiwa sisi, matusi yanatoka kwa wanachadema tena hawana hata uongozi wa kata!... hii hatari kwa chama.
 
Kinachoendelea kwenye thread hii ni porojo tu ili siku iende, ngoja nikachakalike zangu watoto wapate kwenda chooni. mwenye dini inayogawa pesa anijurishe nitasilimu na kujiunga nayo leo leo.
 
Kinachoendelea kwenye thread hii ni porojo tu ili siku iende, ngoja nikachakalike zangu watoto wapate kwenda chooni. mwenye dini inayogawa pesa anijurishe nitasilimu na kujiunga nayo leo leo.

Ingorance is bliss
 
Kinachoendelea kwenye thread hii ni porojo tu ili siku iende, ngoja nikachakalike zangu watoto wapate kwenda chooni. mwenye dini inayogawa pesa anijurishe nitasilimu na kujiunga nayo leo leo.

Kazi njema
 
Wow! ama kweli mimi nina ugonjwa wa kusahau... Hivi JK aliyazungumza haya lini na katika mkutano gani?..Halafu mkuu wangu kuwa na kadi ya Chadema pekee haiwezi kukufanya wewe uwe mwanaChadema isipokuwa kuwa na tumaini la kiimani na itikadi na sera za chama ndio nguvu kubwa ya chama na Wanachadema. Hiyo kadi ni sawa na kuwa na Passport tu haiwezi kuondoa ukweli kama wewe ni Mtanzania.

Halafu mkuu wangu bado hujayajibu maswali yangu hasa kuhusiana na mfumo kristo ni mfumo gani huo? maanake nijuavyo hao waislaam wanaolalamika na mfumo kristu wanailalamikia CCM na JK akiwa kiongozi wao. Hapa kidogo inanitatiza zaidi kuelewa unachojaribu kujenga na hasa kumhusisha JK na Uislaam...Kisha ninakuhakikishia kwamba JK ameyafanya mengi kusaidia makanisa (wakristu) kuliko hao Waislaam na Uislaam wenyewe tofauti na Mwalimu Nyerere ambaye alivunja mkataba na kanisa katoliki mwaka 1967 kwa kutaifisha mali zao..Kisha hao hao Waislaam wasomi wa madrasa alipoingia Mwinyi aliwarudishia wakristu mali zao ktk mkataba wa MoU.. Huyu Muislaam asiyekuwa na Elimu dunia ndiye aliyerudisha mahusiano ya Tanzania na Israel na ndiye pia aliyetuwezesha kuwa na vyama vingi (kuzaliwa kwa Chadema) pamoja na kuchukua mfumo mpya wa kiuchumi kutoka Ujamaa kuingia Utandawazi...Lakini pamoja na kuyafanya yote hayo sijakusikia ukisifia elimu ya madrasa au ndio ktk Ugaidi wa waislaam..

Hizo redio za Masheikh Ubwabwa zinapata nguvu kwa sababu Chadema tumeshindwa kujibu maswali mengi yanayowahusu...Wewe si msomi wa elimu dunia?...kwa nini unarudisha matusi ikiwa mambo mengi yanayozungumzwa na hizi redio ni kuhusu dini na yalikuwepo toka enzi za mwalimu wakifanya mihadhara pale uwanja wa Mnazi mmoja na hatukufika huku iuweje msomi wewe ushindwe kutetea elimu yako unapoitwa kafir kwani kafir maana yake nini msomi?.
Wakristu pia wana mihadhara na mahubiri ya dini ambayo pengine wewe huyasikii. Waislaam wameitwa dini ya shetani, Katukanwa Mtume wao kwa matusi yote unayoweza kufikiria lakini hata siku moja hutamsikia Muislaam akimtukana wala kumdharau Yesu ambaye ndiye DINI na sii waumini wenye kutenda madhambi kila siku na biblia mkononi. Sijui wewe unaishi dunia gani lakini hizi dini zote zipo kughiribu watu waikubaliane na imani yao against dini nyingine na imeanza toka enzi za mitume..

Mkuu wangu nawaombeni sana, na nimeliweka swali hili makusudi kama Mwanakijiji alivyoweza kuwauliza wanaCCM kuhusu Urafiki wake na Uislaam..Na kwa jazba wanna CCM walikuja na kutafsiri hoja nzima wanavyotaka wao ili mradi kudhihirisha chuki zao kwa Chadema na hakika naipatapata picha kwamba haya sii maswala ya CCM na Chadema bali yamefikia ktk UDINI na kwa bahati mbaya chama CCM na Chadema vinatumiwa vibaya na watu kueneza Udini..

Na amini maneno yangu sii wengine isipokuwa viongozi wa dini zetu, waliokufundisha kuwachukia Waislaam kwa sababu ni magaidi na yeyote aliye Muislaam hana elimu dunia... Haaa!Haaa! makubwa haya kama kweli elimu dunia yenyewe ndio hii basi hizo shule sintokwenda hata kwa bakora kwa sababu zinafundisha elimu ya chuki na Ubinafsi..Elimu ya Udini tuloletewa na wazungu kumchukia mpinzani wako ili mradi upate nguvu ya kugawanya na kutawala..

Nitamalizia tu kusema Nyote hapa, wanaCCM na wanaChadema tumeingia mkenge vibaya sana na hizi siasa za chuki. Kufikiria kwamba CCM ni chama cha Waislaam kwa sababu ya JK na Chadema ni chama cha Wakristu kwa sababu ya Dr.Slaa au cha wachagga kwa sababu ya Mbowe...Huu ni Ujinga mkuu wangu hakuna elimu dunia yeyote inayofundisha elimu dunia kwa ufinyu huu.

Na mkuu wangu mnakiweka chama ktk nafasi mbaya sana kuelekea uchaguzi wa mwaka 2015 hasa ikitokea kwamba CUF, NCCR, TLP na vyama vingine vikiungana kwani swala hili lipo mbioni linasukwa na kuna vigogo toka CCM watajiunga huko ili mradi kuiangusha Chadema..Quote my word!
Na sijui kwa elimu yenu ya dunia mliyajua haya....Karagabaho!

Mkuu, Mkandara tupo pamoja, Espouse
 
Rekebisha kichwa cha makala yako kiwe Swali kwa wasio waislam.
Kwa msaada kwa wale wasio ijua madrasat toa ufafanuzi, ukieleze elimu hiyo inalenga nini kwa wanaoisoma na faida wanazopata.
Kuelekeza swali kwa kundi moja la siasa inazidi kuchochea udini bila sababu.
 
Rekebisha kichwa cha makala yako kiwe Swali kwa wasio waislam.
Kwa msaada kwa wale wasio ijua madrasat toa ufafanuzi, ukieleze elimu hiyo inalenga nini kwa wanaoisoma na faida wanazopata.
Kuelekeza swali kwa kundi moja la siasa inazidi kuchochea udini bila sababu.
Mkuu wangu siwezi kubadilisha kichwa cha makala hii kwa sababu naelewa nilichokiandika na sababu zake.
Udini nchini unatokana na siasa hizi chafu za majitaka. Tanzania hatuna Udini isipokuwa kwa kupitia SIASA za vyama na nimeandika haya makusudi baada ya kutambua kwamba CCM walicheza lugha ya Udini kana vile kuwaambia Waislaam kwamba Chadema kinampinga JK kwa sababu ni Muislaam na kwa bahati mbaya BAADHI ya waislaam walivutiwa na hoja hii kutokana na sababu ndogo sana - Dr.Slaa ni mkristu na alikuwa Padre hivyo kuna hatari ya Waislaam kubaguliwa..

Ndipo wakaanza kuhoji uwezo wa Dr.Slaa kabla ya uchaguzi na hakika walikuwa na haki ya kufanya hivyo kwa sababu hakuna mtu anayeweza kumchagua kiongozi wake pasipo kujua vizuri dhamira zake nje ya misingi ya kiutawala, na ndio maana wenzetu hufuatilia marais wao hadi chumbani. CCM walianza ku launch personal attack kwa Dr.Slaa, Chadema na Ukristu wakiwatumia viongozi wa dini na kwa uhakika zipo report za UWT zinazothibitisha jinsi viongozi wa dini walivyoweza kutumiwa kwa FEDHA kuanzisha Udini nchini kupitia mfereji huu wa Siasa za majitaka.

Binafsi sikuona tatizo kubwa zaidi ya kukemea udini tu, lakini athari za matumizi ya misikiti na makania ulifika kiwango kibaya sana cha kuanza kuwatenganisha wananchi wenyewe kwa makundi ya dini. Swala hili halikuwa siasa tena isipokuwa BAADHI Waislaam waliamini Chadema ni chama cha Wakristu na kwa bahati mbaya pia BAADHI ya WanaChadema waliamini kwamba Chadema ni mahala pao bila kujua terms zilizotumika kisiasa. Ikawa kana kwamba Chadema ni chama cha waliokoka na CCM ni chama cha Mafisadi kupitia nadharia ya kiimani ya dini na sio kisiasa tena...

Na ndio maana Mzee Mwanakijiji alipoweka mada ile ya kuhoji Urafiki baina ya CCM na Waislaam umeanza lini, waislaam walikuja juu pasipo kuelewa kwamba kila walivyoshambulia Chadema ndivyo ilivyoonyesha imani yao ya dini kisiasa.. Nikiwa na maana ukiwapinga Chadema ktk hoja ya CCM basi bila shaka unawapa support CCM..Lakini haikuishia hapo kwani hata wale waliokuwa wakibeza urafiki wa CCM na Waislaam nao pia walikuwa ktk mashambulizi ya Waislaam, CCM na Ufisadi wake kuwa kundi moja badala ya kuweka swali la Mwanakijiji kama lilivyo ili Waislaam wapate kujiuliza kwa nini wamevutiwa na kanyanga la CCM kuwatenganisha Waislaam na Wakristu kisiasa...

Vivyo hivyo mimi nimekuja toka upande wa pili baada ya kuwasoma sana wanaChadema wakirusha madogo kwa Waislaam as if CCM ni ya waislaam na hakika kuonyesha chuki yao dhidi ya Waislaam bila kufahamu kwamba sisi wote hapa ni VICTIMS..Na hakika mada hii imedhirisha wazi kwamba sisi wenyewe tumekuwa influences kiasi gani na Udini uliopazwa. Na hakika wapo wakristu na waislaam ambao wameshindwa kutambua kwamba hizi ni siasa za majitaka na hakuna chama kinachoweza kumtumikia bwana mmoja ama upande mmoja isipokuwa tumejazwa ujinga..

Halafu basi hao wote walijaa ujinga huu wanajiita wasomi ili hali wamefunikwa na kiza kikubwa cha kuna mbali. Mkuu wangu, mimi nimepata habari za mbinu zinazojengwa kukiangusha chama Chadema nje ya nguvu ya CCM... Nakama tusipojiweka vema Chadema itakuwa hadithi coming 2015, kwani udini ukishindikana kuivunja Chadema, bado CCM wana plan C, D, E na F ambayo wewe na mimi hatutaifurahia hata kidogo..CCM leo hii hawashughulikina ujenzi wa Taifa tena isipokuwa ni jinsi gani wataweza kuivunja nguvu Chadema na hakika watu wengi hapa JF on both sides wanaisaidia sana CCM kisiasa hali wananchi wakiendelea kulia na maisha magumu..
 
Kwanza swali lako umeliunda vibaya, halafu pia sipendi kujadili mambo ya dini yanayohusisha siasa.

Pili kuna wanachadema wengi waislamu wanaopeleka watoto wao kujifunza maadili ya dini ya kiislamu, kama vile wakristo wengi ambao wana itikadi ya chadema wanavyopeleka watoto wao sunday school kujifunza maadili ya dini ya kikristo, sioni tatizo hapa.

Wewe umekurupuka kusema eti wanachadema wengi wanadharau elimu ya madrasa, umejuaje?

Kama una akili wakati mwingine fikiri kabla ya kupost chochote kwenye Javi letu. Unaoneka hata hiyo elimu ya madrasa huna.

Hakika!
 
Kwa sababu ya upeo wa waliopewa elimu hiyo hebu linganisha Padri na sheikh halafu waweke meza moja halafu tafuta uelewa wao wa mambo haswa general knowledge hapo ndipo utaelewa mmoja ana elimu kasumba bin fitna wakati mwingine ana elimu yenye upeo wa mambo isiyo na fitna na iliyo na haki

Chambua hotuba mbili za viongozi wa dini zilizotolewa wakati wa mazishi ya watu waliouawa na Polisi ktk maandamano ya kupinga meya wa Arusha na kufanyiwa ibada uwanja wa NMC, utajua kuwa siyo wanachadema tu. Utatambua linalopigiwa kelele humu.
 
Dah nimemsoma mwana hauja 2lia! Kwani unaposema elimudunia unamaana waislam wana elimu ya akhera?BABKUBWA kama unaamini hzo ni dini mbili Islam ni ya Mungu na Hiyo yako ni ya fremanson! Ndo mana kuna makosa zaidi ya 50,elfu kny Biblia.NA BILA KUBISHA CHADEMA NA KANISA NI SAWA NA RANG YA MAWINGU NA MAJI YA BAHARI. Kwani kama unaelimu wewe unajua maana ya ugaidi?kama ujui 2lia mana utakuta mpaka Pengo ni Gaidi kwakua anaongoza Commion of
Armed force ndan ya JWTZ.Uwe makini mpwa.

Upupu! Usiongelee Biblia usiyoijua, na makosa unayoyaona ni kwa vile inampinga shetani na wewe ni mfuasi wake! Yeyote anayeiona Biblia ina kasoro yeye ni rafiki wa shetani tu.
Omba Mungu akusamehe na akupe ufahamu، pia ni vyeme hapa tukaachana na udini ktk mambo ya kitaifa، imani zihubiriwe Makanisani na misikitini، poa
 
Mimi nimesoma madrasa nikaelewa na ni mwislamu halafu naipenda chadema. Huna hoja.
Mwislamu ndio nini?..mkuu soma na kama hukuelewa soma tena na tena, elewa hoja kisha jibu kama unayo majibu, huna kaa pembeni. Dadisi kama kuna kosa ama jambo hukuelewa lakini usivamie kutoa jibu ambalo halihusiani..
 
Back
Top Bottom