Nina nguvu za ajabu mpaka najiogopa

TumainiEl

JF-Expert Member
Jan 13, 2010
6,184
11,200
Jamani miaka 20 imepita naninachokiona kinanitisha.

Tukio la kwanza nipale nikiwa shule ya msingi miaka 20 iliopita kuna kijana alinivua nguo nakunichania nguo ya ndani. Jambo lile alikuniacha na furaha nililia sana nakumshitakia kwa Mungu leo hii nasikia yule kijana na yeye alichanganyikiwa na kuvuwa nguo mtaani nakutembea uchi. Nikashituka sana.

Tukio jingine nilimuota mtu amekufa kifo kibaya sana nikaona ndoto siku nikasikia sauti inaniambia mwambie akifa utadaiwa basi mimi kwa roho ya ugumu nikamwambia utakufa acha njia yako.. Same year before end akafa kifo kibaya kwa kugongwa gar na ubongo kupasuka airport.

Nikiwa shuleni A level akatokea mtu ananitishia maisha nikakosa amani sana. Siku moja muda wa jioni nikakutana naye uso kwa uso ajabu nikaona machoyangu yanatoa miale ya moto nakusema maneno makali kwa yule kijana kirohoni pasipo sikia kweli haikupita week jamaa akafukuzwa shule kama mbwa.

Mtu mmoja alie kuwa mlez wetu maanasikuwa na wazazi alitutesa kweli jaman eee yaniachoz yanatisha leo hii hadi namuonea huruma.

Kazini kwangu sikumoja nafika kiongoz wa ngazi yajuu akanipigia sim nakuniambia niache kaz ama atanishusha daraja maana amechoka na mim mimi nikawa mnyonge na kujiuliza nimefanya nini sikumjibu nikamkabidh kwa Mungu ninavyo andika hali yake yule boss inatia huruma yeye ndie alishushwa na ni yeye anatamani acha kazi inatisha sana.

Mh Rais kabla yakuwa rais wala kujulikana niliandika Rais ajaye na kweli ndie hyu tulie nae.

Nilipata kazi kwakusimama kwenye jengo la kampuni kwakusema nataka kufanya kazi hapa jaman same job nikapata kwa miujiza.

Mtu mmoja akatengeneza zengwe nifukuzwe kazi kwakuwa yeye alikuwa na uwezo na anajuwana na wakubwa kulichotokea mpaka kesho nashangaa yeye na kundi lake wakafukuzwa kazi mm nikabaki.

Nilimwambia mtu wangazi ya chini utapandacheo miaka ikapita siku na shangaa amepanda cheo japo yeye alikuwa hataki. Lakini akapanda cheo.

Nikimwambia mtu acha usiende hivi kweli akikataa lazima yampate madhara.

Najiona sina nguvu zakawaida maana siku moja nilisimama kwenye shamba la wazazi wangu lilo dhulumiwa miaka 24 iliopita nakusema maneno mazito kiasi nikaapa kama shamba lile tusingerudishiwa majira ya mchana kweupe basi Mungu wangu angekuwa sio Mungu namwamini. Jaman amini usiamini mchana kweupe saa saba yule mvamizi alitolewa kwenye ile nyumba mtaa mzima ukakumbuka maneno yangu nakusema yule kijana sio wakawaida.

Jambo lingine la ajabu sana nikiwa shule ya msingi kuna kiranja alikuwa kila akiniona ananipa adhabu na kusema ukweli wakati mwingine kwakuwa wazazi sikuwa nao nilikuwa nakuja na ndala au sipo na nguo nzuri ila yule kiranja aliniwajibisha na kuniitweza utu wangu na kunidhalilisha yeye alivaa vizuri nakuwa kijana mtanashati. sitaki kuwaicha siku moja nashuka kwenye gari namkuta amevaa nguo chafu na anaosha magari kiukweli nilishituka kiasi nikaogopa kama angenijuwa japo yeye alinijuwa nakuona aibu wala hatuku salimiana.

Pia kuna siku wakati wa usiku niliamka nakuambiwa mtu fulani angefukuzwa kazi kiukweli nilikataa ile sauti nakusema kwanini miaka ilipita na lile jambo likatimia yule mtu alifukuzwa kazi kama masihara kiukweli nilishangaa sana nakuogopa.

Siwezi sahau mwaka jana 2018 ambapo alikuja mgeni ndani ya nyumba yangu na alikuja kumsalimia mtu alikuwa akituangalizia nyumba yetu. sasa mimi niliposikia ameinga ndani pasipo kumuona wala kuongea naye nikampigia simu mke wanu na kumwambi ingiza flat tv yetu ndani ajabu mke wangu akasema watajisikia vibaya maana hatukuwahi ingiza tv ndani huwa inakaa sebuleni amini usiamini mim nikamwambia mtu huyo ni mbaya hakuamini siku ya tatu mgeni akiwa hayupo fla tv yetu ikaibiwa mchana kweupe jambo ambalo sio la kawaida.
Sijasahau kuandaa karam nzito ikulu na wakati wakubwa wakila wakasema mimi ndio nimeanda wakasifia sana sijajuwa maana ya ile ndoto mpaka leo.

Niliona Rais ajaye niJoseph Pomebe Magufuli na kama moderator anaweza weka post zangu nilipost kabla yaku chaguliwa kuwa Rais wa tano wa jamuhuri ya Tanzania kweli ikatokea.

Tarehe 13/03/2016 nilitabiri chadema itasambaratika leo 2020 imetimia neno ambalo wengi waliniona kama mtu sijielewi au kujitambuwa ila yametimia.. Naona yasio onekana nakuyasema yakatokea.

Nilipo soma post za kijana anaitwa Ben Sanane jambo likanijia kumshauri asipost mambo yanavuka mipaka ya uwandishi wake nilisema kwa nia njema kwa aina ile ya uwandishi uwenda ingetokea siku asipost tena jambo hili limetokea na wengi wanao soma ile post wanaona kama mm ni mtu mbaya na hatari sana ila ukweli nikwamba niliona ktk roho ben kunasiku asingerud kupost na ikawa hivyo.

Ninanguvu za ajabu naomba msaada
 
Hizo nguvu zako tunaomba uzitumie kutuondolea hilo jitu linaloitwa Chadema hapa nchini .

Linaharibu vijana wetu wanakuwa watu wa kulialia bila sababu .
Juzi hapa limesababisha kifo cha mwanafunzi asiyekuwa na hatia kwa kuhamasisha maandamano haramu.
Watu wenye mapepo ya kijani utawajua tu, hawajui hata wanacho kinena, saa hii ndio Kumaaaa anisha nini? we mkuuundu gu yangu hii ndo nini sasa?
 
Kama ulitbiri kuwa Mh. Atakua Mungu anakuona
ac2513e0f568d348ba21758462b687f1.jpg
 
"Katika hali ya Mh Rais kutaka kusikia kilio cha watu wake katika jiji fulani kubwa... Team x inafanya kazi nzito kumletea mkuu taarifa kamili itakayosaidia kuwapa mkoa fulani mkubwa...

Wakuu hao wana angaziwa kulamba jiji hilo kubwa Tanzania wakati aliekuwepo akipewa kazi mpya....."

Huu ni moja ya tabiri zako lkn mpk leo haujatimia ili kuthibitisha hizo nguvu zako za ajabu

Au una muda maalum wa wiki, mwezi, au miaka kwa utabiri wako kutimia ili tuendelee kusubiri

Maana tutathibitisha ukweli wako kupitia haya uliyosema kuliko hizo story ambazo hatuzijui
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom