Nina mashaka na huyu mwanamke

Nina mashaka na huyu mwanamke

Nionavyo mimi hapo uyo dada anaonekana ndio anajifunza ayo mambo ya kiafrika pia nia yake sio mbaya sana kwako, kingine anashawishika alipowaona wenzake wameolewa ndio kachanganyikiwa sana, labda nikuulize swali mzee baba kwako mpango wa kumuoa uyo mdada upo au ndio kiburudisho tu na je itachukua mda gani mpk uje umuwowe? Mana ninavyoona mimi kinachofuata hapo ni kwenda kwenye mizizi na habari ya mizizi si mchezo utaenda mwenyewe kutangaza ndoa
Mpango upo, mkubwa mtu. Labda niwashikirikishe jambo jingine. Mbali na kumuhudumia yeye kimahitaji yote ya kiuchumi, kumfungulia duka la nguo na vifaa vya watoto na akina mama, kumpatia moja ya gari langu kutumia. Lakini pia nalipia sehemu ya ada ya mdogo wake.

Hayo yote yanaonesha utayari wangu wa kuwa na yeye kwa muda mrefu hata ndoa. Ila hatuwezi tu kuanza kuoa. Katika kipindi hiki chote mbali na niliyomkuta nayo, ni binti mkarimu na mwenye adabu sana. Muelewa na mcheshi hata kwa ndugu zangu wanaomfahamu.

Samahani, nimekujibu yote kwa urefu maana kuna mchangiaji mmoja amesema huyu binti anajitolea na nampoteza muda. Nadhani akipitia hapa ataelewa na mimi jinsi nilivyoanza kuwekeza kwake.
 
Labda nijipe muda zaidi na niweke mawazo mbadala zaidi. Yeye hajui kama sikuoga yale maji. Hajui kama nilimuona.

Kwa sasa nitakuwa makini zaidi na zaidi.
.................Elewa sipingani na ushauri alioutoa mdau hapo juu ila kwa manufaa ya muda mrefu ushauri huo hautakuwa na afya kutokana na hatua utakayofikia baada ya kuufata itaweza ije ikuumize maisha yako yote.

Huyo mwanamke ni mshirikina na usikubali kufanya naye ndoa ukiwa forced anataka kuolewa kuwaiga wenzake hali ya kuwa hazijui changamoto za ndoa atakuja akusumbue ujute,pia maoni yangu mwaka mmoja kwa uchumba ni mdogo sana kufanya mfikie kwenye ndoa chakata akili kama muislam owa mbele ya safari akibadilika utamalizana naye kiutu uzima ila kama mkristo kaa chini uwaze sawa sawa.
 
Kusali ni namnanya kuweka ukaribu wetu na Mungu lakini pia ukaribu wetu binafsi. Kama ni mtu niliyefikiria na kuamua kuwa naye, sioni shida juu ya hili. Wangapi tunasali na bado tunasema na kushuhudia wengine uongo? Tunachukia? N.k
Uwa mnasali pamoja baada ya kusali mnazini pamoja sasa uwa mnasali nin? Km sio kumukebehi Mungu acheni unafiki?
 
Mpango upo, mkubwa mtu. Labda niwashikirikishe jambo jingine. Mbali na kumuhudumia yeye kimahitaji yote ya kiuchumi, kumfungulia duka la nguo na vifaa vya watoto na akina mama, kumpatia moja ya gari langu kutumia. Lakini pia nalipia sehemu ya ada ya mdogo wake.

Hayo yote yanaonesha utayari wangu wa kuwa na yeye kwa muda mrefu hata ndoa. Ila hatuwezi tu kuanza kuoa. Katika kipindi hiki chote mbali na niliyomkuta nayo, ni binti mkarimu na mwenye adabu sana. Muelewa na mcheshi hata kwa ndugu zangu wanaomfahamu.

Samahani, nimekujibu yote kwa urefu maana kuna mchangiaji mmoja amesema huyu binti anajitolea na nampoteza muda. Nadhani akipitia hapa ataelewa na mimi jinsi nilivyoanza kuwekeza kwake.
Sasa mkuu kinachokuzuia kuoa ni nini?
 
Pole sana mkuu, binafsi nilishawahi kulimbwatishwa, ni vigumu kumdhania, akifanikiwa lengo lake utakuwa zuzu, akili yake akiwa ameiweka kwenye pochi yake, fanya utafiti, ukijiridhisha, piga chini mara moja
 
Jamaa......kweli hlo jambo sio la kawaida na kwa akili za hawa wenzetu nnavyowafaham, ukimweleza shaka yako hyo tafsir na mkazo atakaotoa yeye na vile sie wanamme hatujui kujibzana (.........) ukwel cjui utauzma vp huo moto. Nina option mbili, mchunguze sana njia zake kwa kina mno, pili kama huwez weka kifuan hlo uloona basi mweleze ila ujiandae kuzima moto.. ukikushnda ndo mambo yataishia hapo maake najua tu atakuwakia umemsuspect anakuloga so yeye ni mchawi.
 
Huyo mpenzi wako naye kacheza card zake vibaya, kama anataka hiyo ndoa sijui harusi bora angetegesha mimba tu, ila kwa ushirikina hapo nakataaaaa kabisa, wadada tunakwama wapi jamani tucheze card vizur unamrambisha dume mchezo kwisha mambo ya tunguri yalipitwa saizi ni kucheza na akili zao tu.
 
[emoji3][emoji3][emoji3] subiri waje wakuambie unahukumu, kwani wewe ni mtakatifu? Kuna kaka mmoja tulikuwa tynafanya kazi wote eti siku hiyo anatuambia eti yeye na girlfriend wake walikuwa wanapiga magoti pamoja wanaomba Mungu awape mtoto, na walipata mapacha. Nilicheka nikasema Mungu huyu kweli anajua kuchukuliana na akili za sisi waja wake. Huwa namuelewa sana Abiud Misholi na wimbo wake ule anaimba ' Ni wewe Mungu pekee wastahili cheo hicho'. Kuna muda wanadamu tunafanya mambo ya ajabu lakini tunachukulia kawaida eti Mungu anasamehe daah ningekuwa mimi ni Mungu hakika nisingevumilia huo ujinga.

Wewe ni umeoshwa ubongo, ni wapi huyo Mungu wako kasema kuna kufunga ndoa.... na kabla ya ‘ndoa’ ukimwomba hasikii..?
 
Wewe ni umeoshwa ubongo, ni wapi huyo Mungu wako kasema kuna kufunga ndoa.... na kabla ya ‘ndoa’ ukimwomba hasikii..?
Wewe, utaratibu wa kuoa upo kwenye biblia....labda hapo kwenye harusi ndio utaratibu umewekwa na kanisa ila utaratibu wa kuposa, kutoa mahari na kupewa mke na wazazi upo tangu enzi za akina Ibrahim vinginevyo msamiati uzinzi usingekuwepo
 
Wewe, utaratibu wa kuoa upo kwenye biblia....labda hapo kwenye harusi ndio utaratibu umewekwa na kanisa ila utaratibu wa kuposa, kutoa mahari na kupewa mke na wazazi upo tangu enzi za akina Ibrahim vinginevyo msamiati uzinzi usingekuwepo

Well uzinzi ni kula chakula ya mwingine, ila kama ndo chaguo lako kuelekea ‘ndoa’ tatizo liko wapi.... huyu mwamba ameshatambulishwa hadi ukweni sema anajichelewesha ndio maana katafutiwa ‘fundi’ anyooshwe fasta.
 
Habari wana bodi.

Hii ni mara yangu ya kwanza kuandika kwenye jukwaa hili, japo kuwa ni mshiriki mzuri wa kusoma na kutoa maoni kwenye mada mbalimbali jukwaani. Leo kuna kitu ningependa kuwashirikisha, pengine kuna wajuvi wa mambo ambao watanisaidia vema.

Nipo kwenye mahusiano na binti mmoja mwenyeji wa mikoa ya Kanda ya Ziwa. Ni muda wa mwaka sasa nipo naye kwenye mahusiano haya. Tumekuwa na wakati mzuri sana, japo mikwaruzano ya hapa na pale haikosekani ila sio mikubwa sana kuleta taharuki.

Kitu ambacho nakiona na najifunza kutoka kwa mwenzangu ni utayari wake wa kutaka kuolewa. Tokea mwezi wa sita mwaka huu yeye habari zake ni mahala pa kufanyia harusi, gharama za ukumbi na chakula, wangapi waje kwa harusi n.k.
Mbaya zaidi, karibia rafiki zake wote wameolewa na nimekuwa napata shinikizo kutoka kwa wenzake kwa njia zisizo za moja kwa moja.

Binafsi, sipo tayari kwa mahusiano ya ndoa kwa hivi karibuni. Ila mpango wa kufunga nae ndoa upo kwa zaidi ya asilimia 50. Shida inakuja kwa upande wa mwenzangu kulazimisha, kuwa karibu na ndugu zangu, hata kunitambulisha kwa watu wazito wa mkoani hapa.

Kilichonifanya niandike uzi huu, ni jambo lililotokea na kulishuhudia binafsi asubuhi hii. Mara nyingi, huwa akiwa amekuja nitembelea kwangu basi huwa tunaenda kuoga pamoja kila mara, iwe asubuhi au jioni au hata baada ya chakula adhimu.

Ila leo asubuhi mwenzangu akaenda oga peke yake. Wakati anaoga, nilienda taratibu kwa lengo la kujumuika naye ila nikasema ngoja nijibanze ili nimfanyie utani wa kumshtua, michezo ya hapa na pale. Mlango wa bafu ulikuwa wazi, nikaweza mtazama alichokuwa anafanya. Mwenzangu alianza kujisafisha sehem zake za siri akawa anarudia rudia mara nyingi kuliko kawaida na jambo la kushangaza, ule mkono aliokuwa anajisafishia akaudumbukiza kwenye ndoo ya maji ambayo niligundua alikuwa amenitengea nije kuoga.

Tokea asubuhi tukio hili limenifikirisha sana na kunifanya kuanza kumtazama tofauti mwenzangu. Sio kwa ubaya ila wasiwasi unanifanya niwaze zaidi.

Nje ya jambo hili, huwa tunasali pamoja na kushirikiana mambo kadha wa kadha ya sala. Ila hili la leo limenishtua mno na kunikosesha amani.

Kwa wajuvi wa mambo, je kuna haja ya mimi kuwa na wasiwasi juu ya tukio hili au nifunike kombe mambo yaendelee?

Nawasilisha.
Kimbia usione nyuma,ameona ktk hali ya kawaida unakuwa mzito kaamua kukubust ila uharakishe mambo.
 
Kaona unasuasua kakutana wa wajanja wamemfundisha mbinu... Kabla hajaharibika zaidi na kama unampenda kwa dhati... Ongea naye kwa upole na makhaba.. Mweleze ubaya na athari wa kitu alichofanya kisha mhakikishie ndoa..
Huwa hawabadiliki hata ukiongea nae kwa lugha mbinguni.atapumzika tu,yamenikuta ndo maana nina experience.
 
Back
Top Bottom