Nina mashaka na huyu mwanamke

Nina mashaka na huyu mwanamke

Sioni Shida hapo. Unahukumu kwa hisia. Timiza wajibu wako
Habari wana bodi.

Hii ni mara yangu ya kwanza kuandika kwenye jukwaa hili, japo kuwa ni mshiriki mzuri wa kusoma na kutoa maoni kwenye mada mbalimbali jukwaani. Leo kuna kitu ningependa kuwashirikisha, pengine kuna wajuvi wa mambo ambao watanisaidia vema.

Nipo kwenye mahusiano na binti mmoja mwenyeji wa mikoa ya Kanda ya Ziwa. Ni muda wa mwaka sasa nipo naye kwenye mahusiano haya. Tumekuwa na wakati mzuri sana, japo mikwaruzano ya hapa na pale haikosekani ila sio mikubwa sana kuleta taharuki.

Kitu ambacho nakiona na najifunza kutoka kwa mwenzangu ni utayari wake wa kutaka kuolewa. Tokea mwezi wa sita mwaka huu yeye habari zake ni mahala pa kufanyia harusi, gharama za ukumbi na chakula, wangapi waje kwa harusi n.k.
Mbaya zaidi, karibia rafiki zake wote wameolewa na nimekuwa napata shinikizo kutoka kwa wenzake kwa njia zisizo za moja kwa moja.

Binafsi, sipo tayari kwa mahusiano ya ndoa kwa hivi karibuni. Ila mpango wa kufunga nae ndoa upo kwa zaidi ya asilimia 50. Shida inakuja kwa upande wa mwenzangu kulazimisha, kuwa karibu na ndugu zangu, hata kunitambulisha kwa watu wazito wa mkoani hapa.

Kilichonifanya niandike uzi huu, ni jambo lililotokea na kulishuhudia binafsi asubuhi hii. Mara nyingi, huwa akiwa amekuja nitembelea kwangu basi huwa tunaenda kuoga pamoja kila mara, iwe asubuhi au jioni au hata baada ya chakula adhimu.

Ila leo asubuhi mwenzangu akaenda oga peke yake. Wakati anaoga, nilienda taratibu kwa lengo la kujumuika naye ila nikasema ngoja nijibanze ili nimfanyie utani wa kumshtua, michezo ya hapa na pale. Mlango wa bafu ulikuwa wazi, nikaweza mtazama alichokuwa anafanya. Mwenzangu alianza kujisafisha sehem zake za siri akawa anarudia rudia mara nyingi kuliko kawaida na jambo la kushangaza, ule mkono aliokuwa anajisafishia akaudumbukiza kwenye ndoo ya maji ambayo niligundua alikuwa amenitengea nije kuoga.

Tokea asubuhi tukio hili limenifikirisha sana na kunifanya kuanza kumtazama tofauti mwenzangu. Sio kwa ubaya ila wasiwasi unanifanya niwaze zaidi.

Nje ya jambo hili, huwa tunasali pamoja na kushirikiana mambo kadha wa kadha ya sala. Ila hili la leo limenishtua mno na kunikosesha amani.

Kwa wajuvi wa mambo, je kuna haja ya mimi kuwa na wasiwasi juu ya tukio hili au nifunike kombe mambo yaendelee?

Nawasilisha.
 
Kama limbwata basi nitakuwa nimeshakula sana. Maana angalau kila siku mbili katika wiki huwa anakuja na tunapika wote chakula hapa kwangu. Au mara moja moja huwa ananiletea chakula kwangu.. na wakati mwingine huwa nakula nyumbani kwake.

Kama lengo litakuwa hilo, basi limbwata za kwenye chakula zitakuwa hazijafanya kazi. Au unaonaje?
Mkimbie huyo manzi ni mshirikina anakuandalia limbwata
 
Inawezekana,

Ila sijawahi mshuhudia akifanya hivi kabla. Sijawahi mhisi kwa jambo la namna hii. Na ni mara yangu ya kwanza naona hili. Unadhani sina sababu ya kuuliza?
Hakuna kitu chochote kibaya hapo. Ila wewe unataka kumtafutia sababu tu.
 
Lakini, ni maridhiano ya hiari ndio yataleta tija na upendo halisia. Kama kuna nguvu imetumika, ikikaribia kuisha utaongeza nzito zaidi.. nakuendelea nakuendelea. Mwisho wa siku tutakuwa tunabomoa hatujengi
Wanaume dawa yenu ndogo, hueleweki taratibu unaeleweshwa
 
We jamaa yaani mnatenda dhambi za uchafu afu eti mnasali pamoja??????! Shit! Umenikumbusha dada mmoja alikuwa anajiita mpendwa na rafiki yake akawa anakuja na Biblia eti wamekuja kuomba wakaishia kupeana mimba. Guys hamuwezi fanya mapenzi nje ya ndoa afu mkaingia kwenye sala wote mkiwa wazinzi!!
 
Naelewa, wakati mwingine kama binadamu tunafanya hayo makosa. Mara kwa mara. Lakini faraja inaongezeka kama kunakuwa na nafasi ya kuweza kusali pamoja, ni kutengeneza matarajio bora mbeleni.

Dhambi inaweza isiwe kuzini tu, kuna kudanganya , wizi, kutamani n.k ukinihukumu kwamba ninasali halafu nazini, basi wahukumu pia wanao sali na wanaiba, wanadanganya n.k.

Shukrani.
We jamaa yaani mnatenda dhambi za uchafu afu eti mnasali pamoja??????! Shit! Umenikumbusha dada mmoja alikuwa anajiita mpendwa na rafiki yake akawa anakuja na Biblia eti wamekuja kuomba wakaishia kupeana mimba. Guys hamuwezi fanya mapenzi nje ya ndoa afu mkaingia kwenye sala wote mkiwa wazinzi!!
 
Kwa sababu umeshamuona anachofanya basi limbwata lake halitafanya kazi tena. We endelea kujilia mema ya nchi.

Kingine cha muhimu, mpaka hapo umeshamjua hana uvumilivu. Nyakati kama hizo ndizo huwa nzuri kumjua mwenzio uvumilivu wake ukoje. Kwa dalili hizi huko mbeleni mkipatwa na magumu basi hatasita kufanya mambo tofauti na unavyotegemea.
 
Ukija JF eleza vitu vyote unavyoweza ona vitasaidia watu kuelewa na kushauri just in a single comment...

Haya we baki usubiri wenye muda wa kuuliza maswali...

Sayonara

Unaweza kunichokoza upate maelezo ya kutosha. Niulize maswali ya kutosha ili niweze kukujibu. Siwezi kuweka kila kitu.
 
Habari wana bodi.

Hii ni mara yangu ya kwanza kuandika kwenye jukwaa hili, japo kuwa ni mshiriki mzuri wa kusoma na kutoa maoni kwenye mada mbalimbali jukwaani. Leo kuna kitu ningependa kuwashirikisha, pengine kuna wajuvi wa mambo ambao watanisaidia vema.

Nipo kwenye mahusiano na binti mmoja mwenyeji wa mikoa ya Kanda ya Ziwa. Ni muda wa mwaka sasa nipo naye kwenye mahusiano haya. Tumekuwa na wakati mzuri sana, japo mikwaruzano ya hapa na pale haikosekani ila sio mikubwa sana kuleta taharuki.

Kitu ambacho nakiona na najifunza kutoka kwa mwenzangu ni utayari wake wa kutaka kuolewa. Tokea mwezi wa sita mwaka huu yeye habari zake ni mahala pa kufanyia harusi, gharama za ukumbi na chakula, wangapi waje kwa harusi n.k.
Mbaya zaidi, karibia rafiki zake wote wameolewa na nimekuwa napata shinikizo kutoka kwa wenzake kwa njia zisizo za moja kwa moja.

Binafsi, sipo tayari kwa mahusiano ya ndoa kwa hivi karibuni. Ila mpango wa kufunga nae ndoa upo kwa zaidi ya asilimia 50. Shida inakuja kwa upande wa mwenzangu kulazimisha, kuwa karibu na ndugu zangu, hata kunitambulisha kwa watu wazito wa mkoani hapa.

Kilichonifanya niandike uzi huu, ni jambo lililotokea na kulishuhudia binafsi asubuhi hii. Mara nyingi, huwa akiwa amekuja nitembelea kwangu basi huwa tunaenda kuoga pamoja kila mara, iwe asubuhi au jioni au hata baada ya chakula adhimu.

Ila leo asubuhi mwenzangu akaenda oga peke yake. Wakati anaoga, nilienda taratibu kwa lengo la kujumuika naye ila nikasema ngoja nijibanze ili nimfanyie utani wa kumshtua, michezo ya hapa na pale. Mlango wa bafu ulikuwa wazi, nikaweza mtazama alichokuwa anafanya. Mwenzangu alianza kujisafisha sehem zake za siri akawa anarudia rudia mara nyingi kuliko kawaida na jambo la kushangaza, ule mkono aliokuwa anajisafishia akaudumbukiza kwenye ndoo ya maji ambayo niligundua alikuwa amenitengea nije kuoga.

Tokea asubuhi tukio hili limenifikirisha sana na kunifanya kuanza kumtazama tofauti mwenzangu. Sio kwa ubaya ila wasiwasi unanifanya niwaze zaidi.

Nje ya jambo hili, huwa tunasali pamoja na kushirikiana mambo kadha wa kadha ya sala. Ila hili la leo limenishtua mno na kunikosesha amani.

Kwa wajuvi wa mambo, je kuna haja ya mimi kuwa na wasiwasi juu ya tukio hili au nifunike kombe mambo yaendelee?

Nawasilisha.
Balehe inakusumbua
 
Back
Top Bottom