illuh
JF-Expert Member
- Mar 17, 2014
- 1,254
- 701
Unamawazo ya busara sana sijui we ni ndugu yangu??
Mtu ukishafikia umri wa kuoa, ina maana tayari wewe ni mtu mzima na una uwezo wa kuongoza familia na kutoa maamuzi yenye busara bila kuomba ushauri ambao wakati mwingine wenye nia mbaya wanaweza kukpotosha. Hebu jiulize kama aliyekuona angekuwa mtoto wako au mdogo wako, ungekuja kuomba ushauri ? Kumbuka kuwa huyo Binti yupo hapo kwa muda mfupi na ataondoka kwao, sasa iweje uwaze kumdhalilisha mkeo, huna ubavu wa kumwambia huyo Binti kuacha hiyo mitego yake mara moja ? Ala, unaitwa Baba, halafu ubaba wako haunekani !!!