Nimfanyaje mke wangu! Kwa tabia hii?

Nimfanyaje mke wangu! Kwa tabia hii?

Upuuzi huo mwambie ajenge familia yake aachane na mambo ya watu.
Mke wa mtu unapata wapi muda wa kwenda kuwatumikia marafiki zako wawili?
Hamna watoto?
Hamna shughuli za kufanya hapo nyumbani?
Mwambie asiwapikie tena bali aongeze jitihada kufanya mambo yenu ya ndoa.
wanasema mke wa mtu ni sumu huenda kuna mipanya nyumbani kwao kwa hiyo anendaga kuwaua
 
Halafu hao marafiki zake nahisi wanatabia chafu kwa hiyo mkanye mkeo mapema asifundishwe uchafu huko.
 
Mwambie haya:
"Kuanzia leo mke wangu sitaki use.nge usenge wako wa kuwapikia hao kenge" akikasirika mle kichuri mwambie "mke wangu hebu tusikilizane hii ni ndoa yetu na mimi kuna kitu utaniambia nitakusikiliza"
Na ukute huwa wanaelewana wale wanatoa pesa kabisa kwa wiki wapikiwe, sababu ya ubachela suala la kujipikia ni gumu jaman hata mimi nliishi maisha ya hao wadada na pesa nlikuwa natoa kwa shost anapika
 
Mimi Kulikuwa na mpangaji mwenzangu.
Mimi ninaweza rudi kazini nikamkuta yeye. Ila akitoka njee anakuuliza.
Umepika.
Siku nikamchoka Nikamwambia Kwani umenioa???
Naona alijifunza
 
Wakuu nina ndoa ya kama Mwaka mmoja hivi!
Wife tulioana kila mtu akiwa na maisha yake, I mean alikuwa anajitegemea na mimi najitegemea!

Tukaamua kuanzisha makazi mapya, tuachane na yale ya zamani, hii sehemu aliunganishiwa na marafiki zake wa karibu kwa sababu na wao wanaishi hapo, ni nyumba nzuri tulivyoamia mambo yalikuwa poa sana, bahati nzuri wote ni watumishi na tunakisehemu cha kufanya ujasiriamali.

Hao marafiki zake wawili ni watumishi pia, na mara nyingi mke wangu ndio huwa wakwanza kuwahi kurudi nyumbani kabla yao!
Ishu inakuja hapa, kwa takribani kama miezi 3 hivi naona wife ndio amegeuka kama mpishi wao! Kila akipika ni lazima wawe na share kwenye msosi wake, kwa wanawake wanaojitegemea kabisa! Na kila mtu ana nyumbani kwake.

Nilijiuliza wife huwa anapata msaada gani kwa hao wadada hadi awapikie kila siku nikakosa jibu.

Wao kupika ni week end tu! Na hawawezi kuleta msosi kwetu kama wife anavyowapelekea, she use her own money to buy all staffs bahati nzuri she never ask any money for food, due to some agreement, pesa yangu ikuze mtaji na kuendeleza ujenzi na yake ishughulike na mambo ya ndani yote ikiwemo mavazi na chakula Ishu inakuja hapo kwenye hizo affairs nyingine, natamani kumpiga stop! binafsi naona kama hili swala halijakaa vyema wakuu, Tushauriane!!
Kama ni utaratibu aliokuwa nao kabla hamjakuwa pamoja,sio vizuri kumzuia asiendelee nao,
Utakiwi kuachana na marafiki zako,au kufanya Yale(mema) uliyokuwa ukifanya na wenzio,kisa tu umeoa au umeolewa.
Ndoa sio kifungo,ni mkataba wa hiari,ikitokea mkaachana,unategemea atamtegemea nani,kama marafiki zake aliisha wadis kwa ushauri wako?,fikiria ingekuwa ni wewe,unatakiwa uachane na mambo yako,kisa tu mkeo hapendi.kama jambo halina madhara ktk kujenga familia yenu,kiuchumi,achana nalo,muache mama,afanye yake,hao anaowapikia wangekuwa wanaume,ningekuambia anzisha balaa,lakini kwa vile ni wanawake wenzie,wanawake wana mambo yao,kuwa na amani
 
Hahaha kichuri ni damu ilopikwa ya mnyama inachanganywa na nyongo nak hutumiwa na wakurya sana .. hii humpa mkurya ujasiri unaosikia ule wa musoma hhahaa..
Sasa yeye huyu sijamuelewa anamaanisha nini kwa kweli!!!
Yeah huwa wanachanganya damu na tumavi twa ng'ombe kidogo ndio maana aliposema amle kichuri mke wake mimi fikra zangu fasta zikaniwahisha kwa amberrutty.
 
Back
Top Bottom