Nimevamiwa na kunguni

Nimevamiwa na kunguni


Piga usafi mkali. Anika godoro, kochi juani. Kitanda mwagia maji moto alafu chukua dizel na sabuni ya unga paka. NB. Hakikisha usafi wa geto(nyumba mara kwa mara almost kama baada ya 2wks. Usafi sio panapoonekana na pasipo onekana. Mashuka uwe wabadilisha ama kufua Kila wakati. Pangilia vitu katika mpangilio mzuri. Baada ya mwezi njoo uwape wengine matokeo
Mimi nejaribu hivyo hapa ghetto lakini madogo wakija likizo tu kumekucha
 
Kunguni wanaletwa na uchafu.
Ila unaweza kuwabeba kutoka huko kuliko kuchafu na wakaendelea na maisha hata palipo pasafi.

Hivyo usafi peke yake hautawaondoa maana chakula chao ni damu sio uchafu, hivyo wanachohitaji wao kuishi ni Binadamu...uwe msafi au mchafu.

Hivyo hatua ya kwanza ukiwaona ni kuhakikisha unawapoteza kwa mbinu yoyote maana wana uwezo wa kubaki hai muda mrefu sana mafichoni hata kama hawajapata chakula.
 
Chief unaesumbuliwa na kunguni umelalaje na umeamkaje?
 
Kunguni hakai kwenye kitanda Cha chuma lazima akimbie fasta.
 
Nimevamiwa na jeshi la kunguni, naomba msaada nimejaribu dawa mbalimbali za kunguni bila mafanikio. Tafadhali naomba msaada ili niweze kupambana na jeshi hilo!
Tumia hii ni kiboko yao
1.jpg
 
Dawa ya hao ni sisimizi
Paka asali kiasi kwenye mbao za kitanda, sisimizi watafuata watashambulia hao kunguni pamoja Na mayai yake, hawatorudi tena, mmi nilkuwa nao ndani kila aina ya dawa nilitumia lakin hawakuisha, komesha ya hao viumbe ni sisimizi
Sisimizi wanakula Kunguni ?
 
Kama ukiwa mtu wa usafi home hata kama ulimchukua kwenye daladala hatoweza kuishi.
Akiwa mjamzito ataishi tu mpaka mje kustuka wameenea nyumba nzima.

Nililetewa beki 3 toka vijijini baada ya week 2 au 3 walienea kila mahali.

Ilibidi nifanye fumigation tukawa salama.Siku hizi kila tukiletewa mdada tunachukua tahadhari kubwa.
 
kunguni tunapo wapatia kwenye misongamano,dalala na mabasi na wageni tunapo wakaribisha.

Kama kaingia nyumbani kwako itakubidi siku nzima kupuliza dawa sehemu kama kwenye makabati,kitanda tena engo zote,godoro,nguo na kitu chenye mbao.
 
Mimi Nina uzoefu na ninacho-sema
Upo sahihi ila mie nimeeleza tu kuwa wakati mwengine hao wadudu wanaweza wasiweke makazi kwenye kitanda kabisa ila usiku ukaona wanakusumbua, kuna mtu alitoa kila kitu chumbani na kusafisha na mwisho kupiga deki chumba kizima ila usiku wadudu wakaja kumsumbua kama kawaida.
 
Upo sahihi ila mie nimeeleza tu kuwa wakati mwengine hao wadudu wanaweza wasiweke makazi kwenye kitanda kabisa ila usiku ukaona wanakusumbua, kuna mtu alitoa kila kitu chumbani na kusafisha na mwisho kupiga deki chumba kizima ila usiku wadudu wakaja kumsumbua kama kawaida.
Kweli
 
Back
Top Bottom