Nimevamiwa na kunguni

Nimevamiwa na kunguni

Nimevamiwa na Jeshi la kunguni naomba msaada nimejaribu dawa mbalimbali za kunguni bila mafanikio tafadhali naomba msaada ili niweze kupambana na jeshi hilo!!.
Kupigana na kunguni inatakiwa ujue makazi na mazalio yao kwanza. Kunguni wanapenda kujificha kwenye kuta zenye nyufa/matundu/upenyo, Kona za kitanda na ndani ya godoro na sehemu zozote zenye cracks na pia nguo, matandiko na hata viti na sofa. Kwa kifupi unatakiwa utoe vitu vyote nje, unyunyizie dawa na ndani na hasa kwenye kona na nyufa. Ikiwezekana mwaga maji ya moto mkali kwenye hizo sehemu baadae ndiyo upige dawa. Vitu ulivyotoa nje pia inabidi uvi-treat kwa dawa na nguo uzichemshe kama supu.
 

Piga usafi mkali. Anika godoro, kochi juani. Kitanda mwagia maji moto alafu chukua dizel na sabuni ya unga paka. NB. Hakikisha usafi wa geto(nyumba mara kwa mara almost kama baada ya 2wks. Usafi sio panapoonekana na pasipo onekana. Mashuka uwe wabadilisha ama kufua Kila wakati. Pangilia vitu katika mpangilio mzuri. Baada ya mwezi njoo uwape wengine matokeo
 
Hapo tafuta dawa ya rungu spray toa vitu nje vitanda makochi na matandiko yote fanya usafi alafu piliza rungu kwenye maficho yote ya kunguni wataisha kwa rungu spray
 
Pia kuna ile ya kumix sabun ya unga na mafuta ya taa na chumvi laini japo mi bnafsi sijawahi itumia hiyo nilitumia diazon hiyo tatzo likaisha nasi
 
Kama ukiwa mtu wa usafi home hata kama ulimchukua kwenye daladala hatoweza kuishi.
Hapana mkuu, labda uwe type ya fumigations kila miezi 3,kitu ambacho sio common kwa watanzania kumbuka hawa jamaa sehemu zao wanazokaa sometimes ni pale huwezi zania na si kitandani pekee na wanatabia ya kwenda kula na kurudi wanakoishi safety pia hawaitaji madume kuzaliana huyo ndio Baba na mama dadek, very soon within 3weeks wanakuwa maelfu ndani, kitendo mpaka uwaone itambue wako maelfu ndani mwako.
 
Chukua petrol tafuta kichupa chenye pampu au toboa kifuniko Cha chupa kitundu kidogo alafu nyunyizia majibu n hapo kwa papo
 
Nimevamiwa na Jeshi la kunguni naomba msaada nimejaribu dawa mbalimbali za kunguni bila mafanikio tafadhali naomba msaada ili niweze kupambana na jeshi hilo!!.
Mkuu kama una buku hapo,
chukua mafuta ya taa ya jero na sabuni ya unga ya 200
changanya mafuta ya taa na sabuni ya unga viganja viwili tu..
Koroga kidogo tu kisha chukua kitambaa chovya hapo halafu paka moja kwa moja kunguni walipo

dakika kumi nyingi watajifia vibaya sana.
 
Nunua mafuta ya taa nusu Lita chukua sabuni ya unga pamoja na chumvi changanya vyote kwa pamoja vijiko vitano vitano vya chai Kunguni kwisha habari yake .

NB Mafuta ya taa Yana harufu Kali kwa muda wa siku kadhaa hivyo uvumilu ni muhimu pia hakikisha umeacha madirisha wazi ksbb Yana maliza oksijeni.
 
Back
Top Bottom