activisty
JF-Expert Member
- Apr 1, 2012
- 315
- 107
Taarifa niliyoisikia kutoka kwa Mwenyekiti wa CHADEMA kuwa wameridhia KATIBU mkuu wetu Dr Slaa, kupumzika kwa mda usio julikana. Kiukweli nimeumizwa na kusikitishwa kwa uamuzi huo wa Dr Slaa hasa nikikumbuka taabu na mateso aliyoyapata katika kukikuza na kukisimamia leo anaamua kuacha kwa namna alivyo amua kufanya.
Naomba nitumie fursa hii kumuomba mh😀r Slaa fikiri mara nne ni maumivu makali kiasi gani utakuwa umeyasababisha kwa watanzania wenzako na hasa tunao kuunga mkono na kutambua umuhimu wako na mchango wako ndani ya chama cha CHADEMA na UKAWA kwa ujumla tafadhari nakuomba rejea kambini kwa masilahi ya chama na Taifa.
Nitakuwa wa mwisho kabisa kuubeza, kudharau mchango wa dr slaa ndani ya Chadema na taifa kwa ujumla katika safari ya mabadiliko. Kazi aliyoifanya 2010 ndiyo iliyozaa nguvu hii ya ushawishi wa mabadiliko kwa watanzania. Nasema nitakua wa mwisho kuungana na Mbowe, ati dr slaa apumzike. Nitakuwa mnafiki kufanya hivo na muongo kabisa. Naamini na nitasimama imara katika kufanya lolote kuhakikisha mabadiliko yanapatikana.lakini pia natambua nguvu ya Lowassa na umuhimu wake katika safari hii ya mabadiliko makubwa lakini pia kwa hekima kabisa ingekuwa vyema Mbowe angeeleza kwanza hoja iliyopelekea kuleta maamuzi hayo kisha tukamsikiliza dr slaa kwani nitamshangaa sana mwanachadema aliyeishangilia kauli ile bila hata kuuliza, kutafakari majibu, na kupima athari zake.
Tunayahitaji mabadiliko kwa gharama yeyote ile ila si kwa kukubali kuitenganisha nguvu tuliyonayo katika safari hii ya mabadiliko."mchango wa lowassa ni mkubwa katika safari hii ya mabadiliko lakini pia nguvu ya dr slaa ndiyo daraja kuu litakaloiunganisha nguvu ya chadema na nguvu ya Lowassa"
By Fikra mfumo.