Nimetokea mahabusu kumuona Lema leo

Nimetokea mahabusu kumuona Lema leo

Bado sijaamini kama hayo maneno yametoka kwenye mdomo wako Bujibuji nakuheshimu sana. Lazima kuna shida zinakuandama kwenye ubongo wako.

kuna lugha ya mazungumzo na maandish,bujibuji hajaongea ila ameandika.gud moment
 
Kuna time alipatishiwa na polisi wanataka kumnywesha sumu....so this time awe makini na vyakula anavyoletewa huko.
 
Wacha aendelee kukaa huko jela kama alivyotaka.
Pale ndipo panapomstahili yeye na wahalifu wenzake.
Nadhani alikuwa amewa-miss sana machalii waliofungwa siku nyingi....sijui walimpokeaje.

Arusha is a better place without Lema!

Ngoromiko you're NUT!!!

Hivi wewe kwa akili yako ya Masaburi unafurahia huu uonevu wa Jeshi la Polisi kweeri???Kwa taarifa yako tu ni kuwa POLISI HUWA HAWANAGA RAFIKI,NDUGU WALA MZAZI. Usije ukashangaa siku moja umeswekwa lupango PASIPO NA KOSA LOLOTE!!!Hiyo ndiyo style za Polisi Tanzania!

Godbless Lema is a hero of this country, he is a callibre of those heroes like Nelson Mandera,Steve Bhiko(SA),Martin Luther King Jr.(US).Ni watu waliowekwa gerezani kwa ukandamizaji wa tawala za Makaburu na kibaguzi kwa mtu mweusi. Lakini watu hawa leo ni MASHUJAA si katika nchi zao tu baali kwa dunia nzima! Wao ndiyo waliopelekea nchi zao kuwa huru na kuondokana na tawala hizo za kibaguzi na kikandamizaji.

Serikali ya CCM haina tofauti na Utawala wa Makaburu wa A.Kusini miaka ile. No difference. Polisi wa CCM wanachowafanyia Watanzania kwa sasa ni UONEVU,UKANDAMIZAJI na UNYANYASAJI uliovuka mipaka. Kila mtu mwenye akili timamu anajua na anaona kuwa kile wanachofanya Polisi kwa sasa ni kutimiza maelekezo ya Mabwana zao Viongozi wa CCM. Baada ya Uchaguzi Mkuu wa 2010, CCM wamegundua kuwa HAWAKUBALIKI kama vile tu serikali ya MAKABURU wa SA walivyokuwa hawakubaliki. Kwa hiyo dawa ni KUTAWALA KIMABAVU. Kamatakamata,piga mabomu ya machozi,mwagia maji ya washawasha,piga risasi za moto na kuua,weka mahabusu,fungulia kesi zenye ushahidi wa kubambika! Ilmradi tu kama ni Mpinzani asipate nafasi ya kutumikia Wananchi!!!!

Najua kuna wana-CCM na watu wa serikali ya Magamba wanapitiapitia kwenye ukumbi huu. Hebu tu tuwape ushauri wa bure kwamba,KILE WANACHO MFANYIA LEMA na WABUNGE wengine wanaopambana na mfumo kandamizi na onevua Serikali hii WAJUE KUWA kwanza WANAWAPA UMAARUFU SANA WAHUSIKA NA VYAMA VYAO na wakti huohuo wao CCM WANAJITENGENEZEA JENEZA LA MAZISHI YAO katika muda mfupi sana ujao.

Kama CCM na VIBARAKA wao(Polisi,UWT,UVCCM n.k)hawawezi kusoma alama za nyakati kwa kulingana na yale yanayotokea huko Afrika Kaskazini k.m. LIBYA,TUNISIA,MISRI,YEMENI n.k basi tutawaita ni WENDAWAZIMU WA KARNE. CCM wafanye wanavofanya lakini wajue kwamba there is a day THEY HAVE TO QUIT,NO WAY!!!!
 
Akitoka mkutano mkubwa wa hadhara na wapiga kura wake iwajuze yaliyomo...Nadhani ngoma ikangurume mpaka jangwani DSM
 
Si ajitolee mshahara wa mwezi huu wanawake wanunue hizo pedi? Hata yeye mpaka atoke huko mahabusu atkuwa TEJA la Pedi pia. Watch out
 
hilojina ngoromiko ni mnyama asiyeona mchana
mkuu nakumbuka umelelewa kwa wale wazee wa kiislam pale machame
tunasikia kwenu mna laana
je ni kweli???

Kweli tupu. Maana kama sio laana ni nini .Halafu mwenye jina masumbuko husumbuka , je ngoromiko ? Huyu tumpotezee maana hamna cha kumsadia.
 
Lema umeonyesha ulimwengu si Tanzania tu kuwa haki inapatikana kwa machungu na si matamu tu. Ninajua siku moja WANANCHI wote wataelewa kwa nini umefanya maamuzi haya magumu. Wewe unaipenda Tanzania na si watu wa Arusha tu. Tuko pamoja nawe.
 
Laana wanayo wanaojipeleka wenyewe jela, pamoja na mashabiki wao kama wewe.
Mnahitaji ukombozi wa fikra.

Wehu kama nyie tumeishawazoea na hamtusumbui vichwa,halafu naona bado una harufu ya maziwa,ukikua na kuanza kujitegemea utakubali mwenyewe.
 
Uchaguzi ulikuwa Octoba 2010; leo ni Novemba 2011 mwaka mmoja umeisha imebaki miaka mitatu na nusu kabla ya maandalizi ya uchaguzi mkuu 2015 kuanza. Nachelea kusema Mbunge wetu hataweza kufikia hata 10% ya mambo aliyowaahidi wapiga kura wake hususani "Machinga complex" kutokana na sintofahamu yake na vyombo vingine kama baraza la madiwani na halmashauri. Uongozi ni mfumo na si matakwa ya mtu mmoja; watu ambao angeweza kushirikiana nao kuleta maendeleo ndio wale madiwani waliofukuzwa, baraza la madiwani chini ya uongozi wa meya (hata kama hakuachaguliwa kihalali). Ifahamike madiwani wanaongozwa na Meya ambaye yeye hamtambui sasa sijui hiyo kasma ya kutekeleza ahadi zake itapitishwa na chombo kipi?

Kukaa gerezani wakati jamii inamhitaji kuhamasisha maendeleo nao si uamuzi wa busara kama kweli Mheshimiwa huyu anafahamu thamani ya muda. Mheshimiwa huyu ni waziri kivuli wa mambo ya ndani na hivi sasa vikao vya kamati vinaendelea Dar es Salaaam sijui nani anawakilisha mawazo yake.

Kushikamana na watu wasio na mchango wowote katika uchumi wa Taifa bila ya kuwapa mbinu za kujikwamua ili waweze kuchangia maendeleo ya Taifa hakuna maana yoyote na kuzidi kuwaharibu hao vijana waendee kuwa tegemezi kwa ndugu na jamaa. Mimi nilifikiri Mheshimiwa angeomba Serikali iwatafutie hao "machalii" pori la kwenda kulima badala ya kupiga debe kwenye vituo vya mabasi, shoe shine, kucheza pool table au kuwaamrisha waende kumtembelea gerezani muda ambao wanatakiwa wawe kwenye shughuli za uzalishaji.

Labda kama alihitaji kukaa peke yake kwa maandalizi fulani kama kujiandaa kwa mtihani hapo naweza kukubaliana na uamuzi wake wa kususia shughuli za ujenzi wa Taifa na kwenda kupumzika gerezani lakini vinginevyo uamuzi wake ni kama amechukua dhahabu (muda wa siku 14) na kuitupa mtoni. Muda ni mali na ukashapita haurudi tena.

Nachojiuliza hizo siku 14 ambazo atakuwa gerezani Bunge litaendelea kumtambua yuko kazini na kumlipa stahili zake ikiwemo mafuta kwa ajili ya kuzungukia jimboni kwake? Kama jibu ni ndiyo, hao machalii wanaotakiwa kwenda kumwona gerezani wao wataishi vipi kwa kuacha shughuli zao wakati yeye analipwa?

Nawasihi watanzania wenzangu muda tulio nao wakati tuna nguvu tuutumie kwa busara kwa faida ya familia zetu na Taifa kwa ujumla.
 
Wacha aendelee kukaa huko jela kama alivyotaka.
Pale ndipo panapomstahili yeye na wahalifu wenzake.
Nadhani alikuwa amewa-miss sana machalii waliofungwa siku nyingi....sijui walimpokeaje.

Arusha is a better place without Lema!

akili mgando!
 
Asante mkuu kwa taarifa hizi muhimu sana. A Tanzanian hero in the making, kwa sababu viongozi wote tulio nao sidhani kama kuna hata mmoja aliwahi kukaa mahabusu. Labda Mwali Nyerere enzi za kupigania uhuru aliwahi kufnguliwa kesi. Sasa Lema anakuja huyo, kwa wanaobeza waangalie wasije yakawakuta ya Mzee Gadaffi ambaye alikufa kifo dhalili lakini alichojitengenezea yeye mwenyewe

Big Up!
 
Mtu muhimu katika jamii daima anathaminika. Mfano ni namna Wamarekani walivyopokea kifo cha Mwanamuziki Michael Jackson, walijazana katika hospitali hihyo - zaidi ya watu laki tatu, hiyo ilikuwa ni kuonyesha kutambua mchango wa Michal katika jamii yao, walidiriki kuacha ajira zao na kwenda kuthibitisha kama kweli mtu wao amewatoka.

Taarifa ambayo wangeipata hata kwenye vyombo vya habari, hivyo hata wale machalii wanaoenda gerezani kumuona Mbunge wao sio kwamba hawana akili kama wewe! Waache wakamuone anayepambana na Wakoloni weusi wanaoshabikia MAGAMBA. "hABARI NDO HIYO"
 
Mtu muhimu katika jamii daima anathaminika. Mfano ni namna Wamarekani walivyopokea kifo cha Mwanamuziki Michael Jackson, walijazana katika hospitali hihyo - zaidi ya watu laki tatu, hiyo ilikuwa ni kuonyesha kutambua mchango wa Michal katika jamii yao, walidiriki kuacha ajira zao na kwenda kuthibitisha kama kweli mtu wao amewatoka.

Taarifa ambayo wangeipata hata kwenye vyombo vya habari, hivyo hata wale machalii wanaoenda gerezani kumuona Mbunge wao sio kwamba hawana akili kama wewe! Waache wakamuone anayepambana na Wakoloni weusi wanaoshabikia MAGAMBA. "hABARI NDO HIYO"

Kwamba nina akili au sina "time will tell"
 
Nimeipata mkubwa, tunahitaji watu kama Lema, na nahisi Arusha kitakuwa kitovu cha ukombozi wa nchi hii.
 
mimi namwamini lema,na siku anatoka tunaomba taarifa kama wadau wakubwa wa mapinduzi tumpokee kwa maandamano makubwa zaid ya mazisha ya january.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom