Nimetokea mahabusu kumuona Lema leo

Nimetokea mahabusu kumuona Lema leo

Hivi kwa kesi ipi jamani, mbona wengi hatuijui?

Si kesi ni unyanyasaji ambao umepangwa na CCM, UWT na unatekelezwa na polisi. Usijishughulishe maana yanatuhusu watu wa Arusha. Si unakumbuka "YARABI NAFSI YANGU"
 
Yote haya yanamwisho. Mh.Lema asante kwa kutuonyesha njia.
Kilichobakia kwetu Ndugu zangu Watanzania tuungane.
Hatuna cha kupoteza ila umaskini wetu utokanao na CCM
 
Shaka yangu kubwa sana ni kuwa ufikiri wa Lema ni mkubwa sana, sasa endapo kutakuwa na gap kubwa baina ya ufikiri wake na wananchi walio wengi wenye mtazamo wa kati na wasio washabiki hataeleweka na atakuwa na jukumu kubwa sana la kujieleza aeleweke.

Kwa sisi wa Arusha fikra zake ni sawa sawia na zetu. Kama wengine hawamuelewi ambayo ni kweli shauri yao. Anatimiza matakwa ya wana Arusha
 
Hujui usemalo!! Anza kuwahamasisha ndugu zako kule kijijini kwenu ambako pengine ukienda unawaonea
kinyaa! Vijana wanajiajiri hakuna umeme miaka 50 ya uhuru! Unajua Arusha mgao unaendaje? Unajua mfumko wa bei sasa sukari inauzwa bei gani? Unga kilo 1800 maskini wataweza vp? Alafu kwa dharau mnawaita panya!! Wewe huna dhiki ila jamaa zako wanataabika anza kuwahamasisha hao utoe mfano.


Sikatai juu ya ugumu wa maisha kwani sisi pia tunachangia hali hii.Miaka ya themanini kulikuwa na azimio la nguvu kazi na wananchi na vijana wasio kuwa na kazi mijini walichukuliwa kwa lazima na kupelekwa katika vijiji vya ujamaa.Maamuzi haya ya Mwl na Kawawa yalikuwa na lengo mahususi katika uboreshaji wa vijiji pamoja na uzalishaji.

Leo hii kila mtu anahitaji kukaa mjini,awe na shule hana shule msemo ni ''tutabanana hapa hapa''.Tazama idadi ya vijana wetu inayoingia mijini kila siku,madereva piki piki wamekuwa wengi.Ebu tujiulize ukosekanaji wa sembe ama ghara ya sembe kuwa juu nayo imachangiwa na umeme?

Tunahitaji kufikiri zaidi sio kila kitu visingizio.Yapo ya kuwalaumu wanasiasa na yapo pia ya kuyaangalia sisi wenyewe.Je!tuko tayari kujitolea kujenga nchi yetu bila kuwa na tamaa ya mali?kama ni hivyo uko tayari kurudi kijijini kuongeza nguvu ya uzalishaji badala ya kulala kwenya baraza mjini?.Je!kuendesha pikipiki mjini ni bora kuliko kusaidia nguvu katika kilimo kijijini?

Hapa kuna kazi ''hata Mussa alisalitiwa na watu wake,Yesu hivyo hivyo sembuse binadamu huyu wa leo asiye mtakatifu bali mtakavitu?''
 
Jamani tusidanganyane kwa kufarijiana katika Nchi hii.Sikubaliani na maamuzi ya Lema kimsingi kwani hakuna anachofundisha zaidi ya kuwafanya waharifu waendelee kuwa waharifu kwa maana ya kuhisi kuonewa.

Wananchi wanahitaji kiongozi wa kuwahamasisha katika maendeleo.Hawana shida ya kutafuta haki kwani wana uhuru wa kufanya yote watakayo ilimradi wasivunje sheria.Uhuru wa kiuchumi,kijamii na kisiasa vyote vinapatikana Tanzania tofauti na nchi nyingine kama Uganda na Libya tuliyofananisha na nchi yetu.Kamwe tusikufuru na kubakia watu wakulalamika tu pasipo kufanya kazi.

Tazama, nimeona vijana wakiwa katika hali isiyoridhisha kwa maana ya kutokuwa nadhifa hapa ITV wakinyoosha vidole viwili kwa maana ya kumuunga mkono Lema.Maisha haya yatadumu mpaka lini, vijana hawa mbali na kutokuwa na kazi,wakipata kazi watafanya kazi kweli?.Nasema uhuru wa kisiasa tunao,ndio maana tunazunguka nchi nzima na kumtukana Rais pasipo hofu.

Tunahitaji ukombozi wa kifikra hasa kufikiri kujishughulisha badala ya kuhisi kuonewa kila wakati.Tukiendelea na hali hii, hata ije serikali gani bado tutaikosoa na kuendeleza usaliti hatimaye kugharimu maisha yetu.

Obama kasifiwa na kupewa ushindi, lakini leo anabezwa na hata kutishiwa kutorudi tena ''white house''.Ubinadamu kazi.

Anzia ukombozi wa fikra kwako; naona unachanga mambo. Maendeleo ya Ujerumani yaliletwa na Hitler akaondolewa ni dikteta. Kama una umri kama wangu uliona siku ya uhuru uchumi na maendeleo yalivyokuwa mfrano 1. Tanganyika ilikuwa kinara wa kilimo cha katani, Almasi na mashamba ya kutosheleza mahitaji ya chakula na mifugo. Tuseme ndicho kipimo. 2 Tulikuwa vinara duniani wa vyama vya ushirika KNCU etc. 3. Tuliamini ukombozi wa kweli wa mwafrika. 4. Mashamba ya Bibi (National Parks) na Mlima Kilimanjaro na theluji

Miaka hamsini baadae niambie kati ya yote hayo tuko wapi? Kwa mantiki yako ni maendeleo kwa wengine ni dhalili inayohitaji ukombozi. Ndiyo tofauti ya wewe na Lema na baadhi yetu tunaemuelewa hata kumchagua atuwakilishe.
 
Wacha aendelee kukaa huko jela kama alivyotaka.
Pale ndipo panapomstahili yeye na wahalifu wenzake.
Nadhani alikuwa amewa-miss sana machalii waliofungwa siku nyingi....sijui walimpokeaje.

Arusha is a better place without Lema!

Nazidi kukubaliana na wazo hapo juu kuwa siasa anazoziendesha Mh. Lema ni next level wengine tutaambulia kufahamu baada ya miaka kadhaa. Watu wa aina yako tunawakuchukulia kama wafu wa mawazo. Ila itakapotimia rudi ukiri.
 
Wacha aendelee kukaa huko jela kama alivyotaka.
Pale ndipo panapomstahili yeye na wahalifu wenzake.
Nadhani alikuwa amewa-miss sana machalii waliofungwa siku nyingi....sijui walimpokeaje.

Arusha is a better place without Lema!

Watu kama nyie mnastahili kufa kabla ya ukombozi wa kweli maana hamna tofauti na upele unaowasha bila mpango mahali popote stupid.
 
Sikatai juu ya ugumu wa maisha kwani sisi pia tunachangia hali hii.Miaka ya themanini kulikuwa na azimio la nguvu kazi na wananchi na vijana wasio kuwa na kazi mijini walichukuliwa kwa lazima na kupelekwa katika vijiji vya ujamaa.Maamuzi haya ya Mwl na Kawawa yalikuwa na lengo mahususi katika uboreshaji wa vijiji pamoja na uzalishaji.

Leo hii kila mtu anahitaji kukaa mjini,awe na shule hana shule msemo ni ''tutabanana hapa hapa''.Tazama idadi ya vijana wetu inayoingia mijini kila siku,madereva piki piki wamekuwa wengi.Ebu tujiulize ukosekanaji wa sembe ama ghara ya sembe kuwa juu nayo imachangiwa na umeme?

Tunahitaji kufikiri zaidi sio kila kitu visingizio.Yapo ya kuwalaumu wanasiasa na yapo pia ya kuyaangalia sisi wenyewe.Je!tuko tayari kujitolea kujenga nchi yetu bila kuwa na tamaa ya mali?kama ni hivyo uko tayari kurudi kijijini kuongeza nguvu ya uzalishaji badala ya kulala kwenya baraza mjini?.Je!kuendesha pikipiki mjini ni bora kuliko kusaidia nguvu katika kilimo kijijini?

Hapa kuna kazi ''hata Mussa alisalitiwa na watu wake,Yesu hivyo hivyo sembuse binadamu huyu wa leo asiye mtakatifu bali mtakavitu?''

Just to know, ivi watu wengine mkiwa mnaandika huwa mnashirikisha ubongo kweli au basi tuu ili mradi umeandika.
let me ask you.. kuna miundombinu gani kule vijijini ya kufanya vijana waweze kuendeleza uzalishaji?? to be honest kama kila kitu kingekuwa sawa hakuna haja ya watu kujazana huku mijini, leo hii ukitembelea mikoa yote ambayo ni maarufu kwa kilimo cha chakula hasa kusini miundombinu haifai watu wanalima kwa jembe la mkono hekari kwa hekari..mazao yakivunwa hakuna hifadhi za kutosha, vyama vya ushirika vyote vimekufa wewe unasema watu wazembe are u crazy or what????? nina hofu na wewe kwamba ni wale chapati tayari hujui hata pembe moja ya nchi hii zaidi ya masaki na oysterbay na chuo ulichosoma marekani.

kama ungekuwa mzalendo usingeandika crap crap hizo.
 
Nimetokea magereza kuu ya mkoa wa Arusha, Kisongo ambako nilikwenda na mke wa Lema na watoto wake. Watoto wake wawili Allbless na Brilliant hawakuruhusiwa kumuona baba yao na wamelia kwa uchungu mkubwa sana wakati askari magereza walipowazuia.

Lema yupo Imara na still msimamo wake uko palepale. Ameona na azidi kujifunza mengi, amewakuta watu wengi wanaolalama kwa kubambikiziwa kesi, amewakuta maskini kibao ambao wamefungwa kwa sababu ya kushindwa kulipa faini ya pesa kidogo na ameomba watu wenye nia njema wachange fedha kuwasaidia watu hao waondoke magereza.

Amewakuta wafungwa wanawaKe wakikosa huduma muhimu kama vitambaa vya kike yaani pedi na hali ni mbaya sana.

Wakati tunaondoka alimwambie mke wake "BE STRONG, The purpose of life sio kisses na maisha mazuri. BE STRONG KAMA MKE WA MARTIN LUTHER CORETTA KING"

Wanaonibeza wacha wanibeze lakini kukaa gerezani kuna maana kubwa sana kwangu.

Nawasilisha.

lema watetee wananchi wako. yaani hawa polisi ni ovyo kweli. mie jana napita pale bamaga, si wakanipiga konozz, akaniuliza dada naomba leseni, nikampa leseni matoke yake kwamba mbona una leseni ya zamani twende kituoni. mie si nikawa mbishi, hapo naambiwa faini laki tatu. nilimshukuia huyo mshenzi kweli, yaani kuniona mwanamke ndo anidhalilishe na kutaka kuninyanyasa. basi alivyo na upolisi wake basi mimi pia nikamwambia lazima nimfanyie. hapo nikampigia mwema, mbona alinyata na kunirudishia leseni yangu.. heti ondoka hapa hii ni onyo ya mwisho. sasa tuone ikiwa ataendelea na kazi. lema wafanyie huko arusha pengine ndo utakuwa mwisho wa magamba
 
Du,haya mdau,kuhusu wafungwa wanawake hapo,amewezaje kukutana nao?

Wengi wa mahabusu wa kike ni chakula ya soldier boys na wafungwa wa kiume wenye sarafu so sio ajabu kukutana nao lupango ya kiume wakiliwa mzigo, nchi hii chochote chawezekana
 
Nimetokea magereza kuu ya mkoa wa Arusha, Kisongo ambako nilikwenda na mke wa Lema na watoto wake. Watoto wake wawili Allbless na Brilliant hawakuruhusiwa kumuona baba yao na wamelia kwa uchungu mkubwa sana wakati askari magereza walipowazuia.

Lema yupo Imara na still msimamo wake uko palepale. Ameona na azidi kujifunza mengi, amewakuta watu wengi wanaolalama kwa kubambikiziwa kesi, amewakuta maskini kibao ambao wamefungwa kwa sababu ya kushindwa kulipa faini ya pesa kidogo na ameomba watu wenye nia njema wachange fedha kuwasaidia watu hao waondoke magereza.

Amewakuta wafungwa wanawaKe wakikosa huduma muhimu kama vitambaa vya kike yaani pedi na hali ni mbaya sana.

Wakati tunaondoka alimwambie mke wake "BE STRONG, The purpose of life sio kisses na maisha mazuri. BE STRONG KAMA MKE WA MARTIN LUTHER CORETTA KING"

Wanaonibeza wacha wanibeze lakini kukaa gerezani kuna maana kubwa sana kwangu.

Nawasilisha.

Dah! Very touching!...ndiyo Tanzania yetu hiyo!!! Watu wasiokuwa na uwezo kunyanyasika na vyombo vya dola huku mafisadi wa mabilioni wakiendelea kupeta.

images
 
Imekuwa vizuri watoto kutoruhisiwa manake wanaweza kuambukizwa ugonjwa wa baba yao wa kupenda kujipeleka jela.


How did you ever became a member here! Kutoa ushuzi Kama huu from your mouth. Well one day utajua kama wewe ni wa kike au wa kiume, as of now I wonder Kama unaijua jinsia yako
 
i will always shout viva chadema viva lema . U are making a difference and history.
 
Wacha aendelee kukaa huko jela kama alivyotaka.
Pale ndipo panapomstahili yeye na wahalifu wenzake.
Nadhani alikuwa amewa-miss sana machalii waliofungwa siku nyingi....sijui walimpokeaje.

Arusha is a better place without Lema!

Acha ujinga unatumikia usiowajua na hofu yako ni maslahi uliyonayo katika mfumo wa kifisadi woga wako ndo umaskini wako kalagabaho
 
Lema is a Strong Person, he can stand alone for the poor.
 
sasa nimeelewa kwa nini lema yuko huko.kweli ni muwakilishi wa wana arusha .
 
mimi binafsi nakubali sera za lema jukwaani ,bungeni na hata mtaani anaijua Arusha tulikotoka na tulipo,ila katika utendaji namshauri awe result oriented na apunguze kuwa too emotional ,kweli tuko tabuni dhidi ya kucha na milija nyonyezi ya CCMM lakini hatujafikia hapo .bado kuna njia passive kabsa za kuushinda mtandao na huka ya kifisadi,namshauri achukue dhamana ,akapambane mahakamani huku akitatua au kusimamia matatizo ya wananchi wake.i submit
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom