Dumelang
JF-Expert Member
- Aug 11, 2011
- 3,273
- 5,926
Wimbo maarufu ulioimbwa na Mwanamziki Bushoke Jr.
"Nimetoka kumuona msela jela amenipa ukweli wa kesi yake, kaongea kwa uchungu huku analia watu wanaamini kesi yake".
Wengi tunaamini wimbo huu ulimuhusu Papii Kocha ambae inasemekana alikuwa Rafiki mkubwa sana wa Bushoke.
Jana magazeti kadhaa yaliandika sana kuhusu kesi hii na wafungwa hawa babu seya "Nguza Viking" na mwanae Papii Kocha au "Papii Nguza" ambapo wameendelea kutafuta haki zao kwa kuamini hawana hatia. Gazeti moja limeandika kuwa katika Maombi yao ya sasa wanalalama kuwa kesi ilikuwa ya kutunga.
Mimi napata wakati mugumu sana, maana huku uraiani watu tumegawanyika makundi mawili, wapo wanao amini hawa wafungwa wameonewa na tuhuma zao si za kweli wapo wanao amini wana hatia na hawafai kuwa uraiani.
Hata hapa JF ili linatokea kila mara linapokuja suala hili. Hisia hizi za mgawanyiko pia zilidhihirika siku CHADEMA wanazindua kampeni zao pale jangwani.
Wakati mgombea wa CHADEMA alipoahidi atamaliza kesi za mashekh wa Zanzibar mara atakapopewa Ridhaa ya kuwa Rais wa JMT, Umma ilipaza sauti na kumwambia "na Babu seya"..
Lowassa alijibu kwa Ufupi "nimewasikia".
Hoja yangu ni hii, kama Kweli P alimwambia ukweli rafiki yake Bushoke ukweli, na katika madai yao yaliotoka jana pia wanadai ni kesi ya kupakaziwa, kwanini wasiuambie na Umma ukweli huo?
Ukweli ambao utawaweka huru, kwanini sasa wasiuseme? Kwa miaka kumi waliomba huruma za Kikwete mara kadhaa, bila mafanikio, Kikwete kaondoka sasa wameona hali ni mbaya wenda, sasa wameamua kwenda tena kwingine kutafuta haki. Swali kwanini kwa mara nyingine tena?
Kwanini Papii na baba yake hawajawai kukubaliana na maamuzi ya mahakama yaliokwishafanywa mara tatu? Kwanini wamelilia sana huruma za Rais? Kwanini wameendelea kuamini walisingiziwa na kutafuta haki kila mara wakiamini wataipata?
Jamii imegawanyika, mahakama imebaki moja lakn ikiporomoa hukumu zake mara kadhaa.
'P', UKWELI ULIOMWAMBIA BUSHOKE UAMBIE NA UMMA SASA, LA SIVYO...ENDELEENI KUKAA NDANI.
Naomba kutoa hoja.....
NOTE:
Nami nakanganywa sana na ukweli wa kesi hii.
Nipo 50/50..
"Nimetoka kumuona msela jela amenipa ukweli wa kesi yake, kaongea kwa uchungu huku analia watu wanaamini kesi yake".
Wengi tunaamini wimbo huu ulimuhusu Papii Kocha ambae inasemekana alikuwa Rafiki mkubwa sana wa Bushoke.
Jana magazeti kadhaa yaliandika sana kuhusu kesi hii na wafungwa hawa babu seya "Nguza Viking" na mwanae Papii Kocha au "Papii Nguza" ambapo wameendelea kutafuta haki zao kwa kuamini hawana hatia. Gazeti moja limeandika kuwa katika Maombi yao ya sasa wanalalama kuwa kesi ilikuwa ya kutunga.
Mimi napata wakati mugumu sana, maana huku uraiani watu tumegawanyika makundi mawili, wapo wanao amini hawa wafungwa wameonewa na tuhuma zao si za kweli wapo wanao amini wana hatia na hawafai kuwa uraiani.
Hata hapa JF ili linatokea kila mara linapokuja suala hili. Hisia hizi za mgawanyiko pia zilidhihirika siku CHADEMA wanazindua kampeni zao pale jangwani.
Wakati mgombea wa CHADEMA alipoahidi atamaliza kesi za mashekh wa Zanzibar mara atakapopewa Ridhaa ya kuwa Rais wa JMT, Umma ilipaza sauti na kumwambia "na Babu seya"..
Lowassa alijibu kwa Ufupi "nimewasikia".
Hoja yangu ni hii, kama Kweli P alimwambia ukweli rafiki yake Bushoke ukweli, na katika madai yao yaliotoka jana pia wanadai ni kesi ya kupakaziwa, kwanini wasiuambie na Umma ukweli huo?
Ukweli ambao utawaweka huru, kwanini sasa wasiuseme? Kwa miaka kumi waliomba huruma za Kikwete mara kadhaa, bila mafanikio, Kikwete kaondoka sasa wameona hali ni mbaya wenda, sasa wameamua kwenda tena kwingine kutafuta haki. Swali kwanini kwa mara nyingine tena?
Kwanini Papii na baba yake hawajawai kukubaliana na maamuzi ya mahakama yaliokwishafanywa mara tatu? Kwanini wamelilia sana huruma za Rais? Kwanini wameendelea kuamini walisingiziwa na kutafuta haki kila mara wakiamini wataipata?
Jamii imegawanyika, mahakama imebaki moja lakn ikiporomoa hukumu zake mara kadhaa.
'P', UKWELI ULIOMWAMBIA BUSHOKE UAMBIE NA UMMA SASA, LA SIVYO...ENDELEENI KUKAA NDANI.
Naomba kutoa hoja.....
NOTE:
Nami nakanganywa sana na ukweli wa kesi hii.
Nipo 50/50..