Kiukweli kabisa hakuna wanawake walioumbwa maalumu na kupigwa mihuri kwamba huyu ndio wa kuoa la hasha bali ni miongoni mwa hao unaowachezea na kuwaacha kabla hujalalamika kuwa umekosa wife material jiangalie wewe mwenyewe kwenye ulingo wa mapenzi je rekodi yako inasemaje.
Kwa mfano watu wanawaona room kwako wanawake wanapishana kama clinic au sokoni hakuna mwanamke anayejitambua atakaye thubutu kuwa karibu na wewe kwa tabia yako mbaya kama hiyo.Lazima uhakikishe kuwa kama unamtaka chiriku uhakikishe kuwa umeandaa mazingira ya kumvutia chiriku.
Yaani kama unataka mke lazima na wewe ujiandae kuwa mume kisaikolojia na kiuhalisia ionekane kuwa unataka mke mpaka ukimwambia mtu kuwa unataka kumuoa basi anajua kuwa kweli una maanisha kwa sababu ndoa sio jambo la mchezo.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.