Mimi binafsi ni mdau mkubwa sana na muumini mzuri wa siasa za CCM na mara nyingi napenda sana kutembea kwenye matawi ya CCM kujua yanayoendelea.
Katika kipindi cha wiki moja tangu lile zuio la kutofanya mikutano ya hadhara ya kisiasa kutenguliwa nimekuwa nikifuatilia kwa ukaribu kujua mtazamo wa wanachama wa upinzani, je wamechukuliaje?
Nilichokiona kimenistaajabisha sana. Makundi kwa makundi wanarejesha kadi za vyama vyao na kuchukua kadi za CCM na wengi wakipongeza uamuzi wa Samia na kusifu mabadiliko ambayo CCM imenuia kuyaleta.
Karibu wote nilioona wanarejesha kadi ili kuchukua za CCM ni wale wakereketwa wa upinzani. Ni wale wa 'nitafia upinzani', nimewajua kutokana na juhudi walizoonesha kipindi fulani kuupambania upinzani.
Binafsi nampongeza sana Rais Samia kwa uamuzi wake mgumu kwa kukirudisha CCM katika enzi yake, Ile enzi ambayo imebaki kovu kwa upinzani mpaka leo.
Uamuzi wa Rais Samia ni muafaka kwa mustakabali za siasa za hoja.
Upinzani najua wanaamini sasa ni wakati wao lakini wangejua kinachoendelea huku chini namna gani watu wanavyopagawa na maamuzi ya Chifu Hangaya basi wangetumia majukwaa yao kumpongeza badala ya kumponda na kuwakasirisha Wananchi.
Katika kipindi cha wiki moja tangu lile zuio la kutofanya mikutano ya hadhara ya kisiasa kutenguliwa nimekuwa nikifuatilia kwa ukaribu kujua mtazamo wa wanachama wa upinzani, je wamechukuliaje?
Nilichokiona kimenistaajabisha sana. Makundi kwa makundi wanarejesha kadi za vyama vyao na kuchukua kadi za CCM na wengi wakipongeza uamuzi wa Samia na kusifu mabadiliko ambayo CCM imenuia kuyaleta.
Karibu wote nilioona wanarejesha kadi ili kuchukua za CCM ni wale wakereketwa wa upinzani. Ni wale wa 'nitafia upinzani', nimewajua kutokana na juhudi walizoonesha kipindi fulani kuupambania upinzani.
Binafsi nampongeza sana Rais Samia kwa uamuzi wake mgumu kwa kukirudisha CCM katika enzi yake, Ile enzi ambayo imebaki kovu kwa upinzani mpaka leo.
Uamuzi wa Rais Samia ni muafaka kwa mustakabali za siasa za hoja.
Upinzani najua wanaamini sasa ni wakati wao lakini wangejua kinachoendelea huku chini namna gani watu wanavyopagawa na maamuzi ya Chifu Hangaya basi wangetumia majukwaa yao kumpongeza badala ya kumponda na kuwakasirisha Wananchi.