Nimeshangaa hii Mahari, sikuitegemea

Nimeshangaa hii Mahari, sikuitegemea

Leo nlimtuma mshenga na ancle wangu kuchukua majibu ya posa na thamani ya Mahali cha ajabu wamepewa karatasi yenye mchanganuo wa vitu na thamani yake jumla wamepata laki 658000 hata siamini hapo hapo wakatoa laki 2 nadaiwa laki 458000 (walienda na millioni 1 ila waliona ni dharau kulipa yote)
 
Hongeraa Brother, wenzako wakifika tu wanaambiwa toa Ngombe 6 na vinginevyo kibao shukuru wewe wakwe zako hawana tamaa
 
Mimi mwenyewe Jana waliwambia washenga wajihukumu kwa walivyoandaa, wakataja 1m wala hawakubishana wenyewe wanasema hawamuuzi ila natoa zawadi tu .mpaka nikafikir kwa nini wasingesema kilo 5
 
oya mkuu niachie goma hilo nakupa 2mil yao afu me nawapa hyo laki sita yao
 
uache utoto wa kuchangia serious post kwa utumbo wako
 
hyo mbili inawatosha mtoto kama anakupenda atakuja kama hataki aache
 
wacha nikusaidie ulivyopigwa

  1. Blanketi la bibi 30,000
  2. Koti la Babu 50,000
  3. Kanzu ya Baba 50 000
  4. Khanga ya Mama Mkwe na Tenge lake 50,000
  5. Kishiika kaka 20.000
  6. Kishika mjomba 50.000
ukweli ni kwamba umeileta mda yako kwa wakti muafala na nadhani itungwe sheria ya kudhhibiti mahari
 
oya mkuu niachie goma hilo nakupa 2mil yao afu me nawapa hyo laki sita yao


wengi wanakosea kumwona mwanamke kama chombo cha kiburudisho.

mahari inategemea hali ya familia kiuchumi, dini, utashi na mazingira\eneo anapotekea huyo mwanamke anayeolewa...

mahari, ni kama aksante au heshima kwa familia ya mwanamke.

mahari ipo ktk thaman ya pesa. lkn thaman ya mwanamke ni zaidi ya pesa\mahari

(japo simu inaweza kuwa na thaman ya juu kuliko mahari ya mtu!)
 
Leo nlimtuma mshenga na ancle wangu kuchukua majibu ya posa na thamani ya Mahali cha ajabu wamepewa karatasi yenye mchanganuo wa vitu na thamani yake jumla wamepata laki 658000 hata siamini hapo hapo wakatoa laki 2 nadaiwa laki 458000 (walienda na millioni 1 ila waliona ni dharau kulipa yote)
Kuna wenzio wanatoa 2milion
 
uncle wangu mmoja alioa 2014,kwenye kikao mshenga alinichekesha sana,alisema"jamani hili ni jambo la kujenga na si kubomoa,kwa hyo usitake mahali ikulipie madeni yako yote au uanze kufikiria kufyatua matofali ili uanze kujenga nyumba ktk kiwanja chako ulichonunua" hata wale wazazi wa mwanamke walicheka lakini ndo message sent.uncle alipigwa 800,000/= ile kauli nadhani ilisaidia.hongera mkuu by the way.hao wazaz wa shem ni waelewa.mahali sio mtaji wala kukomoana wala malipo,bali ni masharti ya kimila/kidini tuu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom