Nimeshangaa hii Mahari, sikuitegemea

Nimeshangaa hii Mahari, sikuitegemea

daa sijui ya kwangu watataka mahari sh ngap! ila nadhan haitazid bei ya king'amuzi
 
Unaoa wapi? kama bado anao mabinti nami nije nichukue hapo. Huku nimeambiwa ng'ombe zenye afya njema ziwe 30, mbuzi 5, kuku 2, vitenge, blanketi, panga, jembe, fyekeo, sufuria nk nimetulia natafakari ukuu wa Bwana, maana hata ng'ombe mmoja sina, hata kuku sina. Hebu huyo mukwe wako niunganishe nae tulonge kwa HERUFI kubwa kama bado ana mabinti wastaarab
 
Hongera kwa kuoa bukoba ndo bei cheeee kwetu bila ng'ombe zile za kwetu zenye pembe ndefu utakoma
 
Wewe ulitaka utajiwe mahari kubwa? Kwani unanunua bidhaa adimu?
 
Leo nlimtuma mshenga na ancle wangu kuchukua majibu ya posa na thamani ya Mahali cha ajabu wamepewa karatasi yenye mchanganuo wa vitu na thamani yake jumla wamepata laki 658000 hata siamini hapo hapo wakatoa laki 2 nadaiwa laki 458000 (walienda na millioni 1 ila waliona ni dharau kulipa yote)

Huyo Uncle wako (Mshenga) kapiga cha juu usikute hata 150,000/= haijafika wakati mwingine dai receipt tena iwe na TIN & VRN baadae claim VAT yako na Dr Magufuli atakuwa kakutambua.

Kila manunuzi dai receipt Baba vinginevyo sheria itachukua mkondo wake.
 
Wakumbushe kulipa kodi Mkuu......kabla iliyopanda haijaanza kutumika
 
Familia zilizo bora mahari zao zinakuwa juu ili kuendelea kufanikisha ndoto zao za kumiliki dunia lakini kwa wenzangu na mimi mahari ni jambo la heshima na hata maisha tupitiayo kwa % kubwa tumerizika nayo sasa tutoze mahari kubwa wakati maisha yanabaki yaleyale ni kumzalilisha binti yetu,maskini au wenye vipato vya kawaida kwao utu mbele kuliko kitu
 
Leo nlimtuma mshenga na ancle wangu kuchukua majibu ya posa na thamani ya Mahali cha ajabu wamepewa karatasi yenye mchanganuo wa vitu na thamani yake jumla wamepata laki 658000 hata siamini hapo hapo wakatoa laki 2 nadaiwa laki 458000 (walienda na millioni 1 ila waliona ni dharau kulipa yote)

Mkuu unatokea pande zipi za tized? Pale uchagani hiyo ni hela ya mbege debe kumi tu! Sasa sijui ingekua kule sijui ungeenda wapi! Anyway mahari inatolewa kwa mujibu wa mila na taratibu. Ni jambo la busara kutoa mahari na inaleta heshima kwako na jamii kwa ujumla. Usiniulize mbona wanaume hawapewi, jibu litakua simple, kuwa hawaolewi.


Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom