Nimepata mpenzi Jf

Nimepata mpenzi Jf

Mimi nakutakia kila lenye baraka, mjitahidi sana kuweka mambo yenu private, asijue mtu hata kama mnapitia magumu, especially humu.

.. lakini nasisitiza, mpeane tunda la adam ili mjuane vizuri, tunda ni tamu kama linatosha, tunda ndio kiunganishi cha maisha yenu. Peaneni na msinyimane...
 
Ohooo samaki mwingine huyu amekutana na baharia ,tumpe mwezi tu atarudi hapa analialia na hizo ngonjera zake zote zitakuwa vice versa.
Mambo mengine mtuulize sisi kwanza tuwape experience.
Tatizo la humu mabaharia hatupewi kipaumbele alipaswa kuchukua ushauri kwetu
 
1. Mpenzi wangu ni mzuri na mwenye nguvu,mashuhuri miongoni mwa wanaume elfu kumi wa hapa jf

2.Kichwa chake kizuri kama dhahabu safi,nywele zake ni za ukoka,nyeusi ti kama kunguru.

3.Macho yake ni kama ya hua kandokando ya kijito,ni kama njiwa waliooga maziwa kando ya kijito.

4.Mashavu yake ni kama matuta ya rihani, kama bustani iliyojaa manukato na manemane.

5.Mikono yake imewekwa bangili za dhahabu

6.Miguu yake ni kama nguzo za alabasta

7.Kinywa chake kimejaa maneno matamu,kwa ujumla anapendeza.

Basi, hivyo ndivyo alivyo mpenzi wangu,naam, ndivyo alivyo rafiki yangu,enyi wana Jamii forum

#Honey najua utapita hapa '
asante kwa kuniona katikati ya wengi, asante kwa upendo unaonipa, Nakuahidi heshima na unyenyekevu, nitakuwa faraja yako wakati wa majonzi, Msaidizi wako wakati wote, Aibu yako itakuwa aibu yangu, shida yako shida yangu, nitakuwa mshauri asiyechoka, Nitakuwa heri kwako siku zote za maisha yetu, Asante kwa kunipenda

#LoveIsSomethingElseWeeSikiaTuKwaJirani
Mtoa uzi jinsia yako ni ipi?
 
Back
Top Bottom