Nimeolewa ila nimefall kwa jamaa

Nimeolewa ila nimefall kwa jamaa

Wakuu nahitaji mawazo yenu kwa kipindi hiki cha majaribu nachopitia.
Mi nimeolewa nna miaka kama 9 kwenye ndoa na kwa kipindi hiki chote nimepitia mazuri na changamoto pia ila sikuwahi kujutia ndoa.Jamaa aliyenioa ni msomi na anajua kuitafuta hela.Kiufupi tuna maisha mazuri nina kila kitu nachokihitaji km nyumba,usafiri wa maana na two beautiful kids.

Ktk kipindi cha ndoa nimepitia changamoto kwa huyu mume wangu.Kiufupi anapenda starehe pombe kwa sana na company za washikaji.Me sio mnywaji wala sitoki kiivo nikitoka job ni home kuangalia watoto na nyumba.Kiufupi ni mke mwema flan!!yes najiamini kwa hilo.Jamaa nishafumania msg za wanawake mara kibao ila naishia kusamehe na sikuwahi kuwaza kulipiza.Huwa nasali sana nikipitia hizi changamoto na Mungu ananivusha salama.

Sasa basi kilichonifanya nilete huu uzi jamvini ni situation niliyonayo now.Kiufupi miezi km 6 iliyopita nimekutana na jamaa ktk kazi flani.Jamaa ana mvuto na alikua ananipa attention flan ivi throughout..Tuliclick haraka sana tukawa close.Ilitokea tu sijui kwa nn..Nilinotice jamaa ananicare vby sana. Mwanzo nilichukulia poa ila siku zilivoendelea kwenda nikaanza kumfeel taratibu.

The eye contact was awkward btn us na imefika mahali najiona nashindwa kuresist.Nikiwa nae under one room nashindwa kabisa napoteza uchangamfu naishiwa pozi kbs.Jamaa anaonyesha interest za wazi ila najikaza knowing kwamba am married ataniona a cheap woman.

Huwa tunaongea mambo mengi na ananieleza issues zake kibao.Kuna siku alinifungukia ila nikavunga nikamwambia its better tuwe mbalimbali coz me ni mke wa mtu na siwezi cheat on my husband.Baada ya hapo akanikaushia km wiki.Aisee nilikonda kwa mawazo.Baadae tukaanza kuwasiliana upya na jamaa anaomba kidate na mm anataka tuspend tym wawili.Kashanialika kwake mara kibao nachomoa.Imefika mahali najiona ntashindwa huko tunakoelekea siko.
Kiufupi kinachonitatiza ni haya yafuatayo:

1.jamaa anajua me ni mke wa mtu so its obvious anataka game tu hakuna mapenzi.

2.Since ni coworker baada ya game ntamwangaliaje ofcn?

3.Naogopa reputation yangu among my workmates wakijua nimetoka na jamaa since wanaume hawana siri.Aisee mi ni mdada nayejiheshimu na wananiona nina bonge la mume.

4.Namfeel mno jamaa na siimagine kupotezea hizi feeling.Ni mtu anayenifanya niwe happy muda wote,confident about myself na I feel lyk a woman again.

Wakuu nisaidieni namna nitakavyohandle hii situation maana naumia kiukweli natamani niuridhishe moyo wangu ila nawaza consequence,kumpotezea jamaa nashindwa naumia at the same time sitaki kuharibu maisha yangu.
Unachokitaka utakipata na kitakupata cha kukupata. Mke wa mtu hastahili kuwa na ukaribu sana na mwanaume asiyekuwa ndugu au mumewe.
 
Mamy, huyo ni shetani anataka kukuharabia maisha yako kabisa. Kaa mbali sana naye. Wewe umesema umekuwa unamwomba Mungu. Ukimwona, anza kumwomba Mungu kimoyomoyo. Tafakari watoto wako wazuri. Huyo anayejua wewe ni mke wa mtu halafu bado anakufuata ni mbaya kuliko shetani. Unaweza kumkubalia ukute hata hakuridhishi, si lolote si chochote. Halafu akakutangaze kwa wenzio wote ofisini. Akuachie na ukimwi. Halafu uachwe na mumeo. Na kazi itaisha maana ile aibu utakayopata baada ya ofisi nzima kujua itafanya ufanisi wako kikazi ushuke, kila mtu akudharau. Ujikute huna mume, huna kazi, na watoto uwaachie mumeo 'avute' kifaa kingjne fasta. Tafuta muda mzuri. Mridhishe mumeo kwa yale anayopenda. Wakati ame relax mweleze jinsi unavyom miss. Na wewe kubali uwe unaenda nae kwenye hizo 'company' zake angalau mara moja moja.
 
Ishinde tamaa ya mwili, heshimu ndoa yako kwa kujiheshimu wewe kwanza.

Story za namna hii zinatufanya wanaume tuwe wapole sana, ni ngumu kuusoma moyo wa mwenzi wako.
 
Mamy, huyo ni shetani anataka kukuharabia maisha yako kabisa. Kaa mbali sana naye. Wewe umesema umekuwa unamwomba Mungu. Ukimwona, anza kumwomba Mungu kimoyomoyo. Tafakari watoto wako wazuri. Huyo anayejua wewe ni mke wa mtu halafu bado anakufuata ni mbaya kuliko shetani. Unaweza kumkubalia ukute hata hakuridhishi, si lolote si chochote. Halafu akakutangaze kwa wenzio wote ofisini. Akuachie na ukimwi. Halafu uachwe na mumeo. Na kazi itaisha maana ile aibu utakayopata baada ya ofisi nzima kujua itafanya ufanisi wako kikazi ushuke, kila mtu akudharau. Ujikute huna mume, huna kazi, na watoto uwaachie mumeo 'avute' kifaa kingjne fasta. Tafuta muda mzuri. Mridhishe mumeo kwa yale anayopenda. Wakati ame relax mweleze jinsi unavyom miss. Na wewe kubali uwe unaenda nae kwenye hizo 'company' zake angalau mara moja moja.
Asante sana kwa ushauri.Duh umenigusa sana!Najipa moyo this too shall pass.
 
Hiyo n changamoto kubwa sana inayowakuta wengi sana, kwa situation ulionayo utakuja kuleta majbu hapa lazma jamaa akupitie.. Hapo ulipofika lazima utagawa mzigo lasvyo mshirikishe mumeo hapo ndio utapona
 
Ubaya w'ume hawana siri na mambo haya, lazma atamuambia best yake mmoja tuuuu. Na huo ndio utakuwa mwanzo wa kuchafuliwa jina lako
 
Ombi sana Mungu akupe ujasiri wa kuepuka hilo ni tatizo maisha hayo mazuri yatakuwa balaa ndoa yako itakuwa ndoano usijiruhusu kushindana mmeo endelea kumthamini zaidi ingawa yeye ana wanawake wengine usijari sana na usijidanganye mwanamke alie ktk ndoa akitoka nje ya ndoa amekwisha Mimi ni mwanaume ila nipenda hii kuhitaji ushauri ni mara mia hata kama ni boss wako aliekuajiri achukie akuachishe kazi ila endelea kujiheshimu usiupe nafasi Moyo wako kuyawazia hayo anayo kutamkia kukonda nikwa kuwa unayawaz hayo aliyokutamkia ,jiulize umekosa nini kwa mmeo Mapenzi hakutoshelezi?mmeo hakuheshimu maana yake aliwahi kukuletea awala nyumbani?Nini unadhani utapata kwa hyo ukimvulia nguo ambacho hupati kwa mmeo?ukijilahisi ndoa umeivunja mwenyewe kwa mikono yako pls jiepushe na mazea huko kwenda kwake pia ukome ipo siku utashindwa kujizuia ,huyo ana kutamani tu yaani akuweke kwenye rekodi ya wale aliowahi kuwapitia,Nakushauri epukana naye mapema usije ukajuta badaye ,mmeo ni mmeo tu kumbuka man familia usijifunze tabia isio yako ikakugharimu by Counselor
 
Dada ushauri wangu ni huu, " baki njia kuu"... MUNGU ni mwaminifu sana kwako.
 
"Namfeel mno Jamaa na siimagine kupotezea hizi feeling " aliesema wanawake mwalimu wetu kipofu hakika hakukosea.....ngoja nikakojoe nilale miee.[emoji9][emoji9]
 
Ushaur wng we endelea kusali kama zaman najua utayashnda hayo majarb its better to stay away na hy mtu
 
Kuwa makini,we umeolewa tena kwa ndoa,heshimu ndoa huwezi kulipizana kisasi na mwanaume.
 
Mpe tu hakuna namna, vitu vyenyewe mmebandikwa paah...(). Roho mbaya inatoka wapi?
 
Mpe jamaa apige mambo, kwani heshima shingi ngapi!! Alafu akitokea mwingine mpe nae ... Unaonekana unataka kulipiza kisasi kwa mumeo, don't do that..
 
Sio kila unachokitamani basi ni lazima ukipate.

Ukicheat uta regret tu, then hakuna kipya sanaa utakacho discover. Kemea pepo hiloo
 
Women need to be Appreciates, they need to feel wanted, they need to praised. Even DUH MKE WANGU HIKI CHAKULA LEO KITAMU SANA, MAKES A BIG DIfference .

So with this foolish guy in your office, has touched were you are most vulnerable, thats why you feel recipocative its not love nor any other thing.

Challenge yourself to win you man back but with dignity and inteligence, usimbembeleze, make you life arround your children and maybe arround his part of the family, make yourself very beautiful n uour house very immaculate, make it a heaven.

Confuse him, make him wonder, umejiremba na hutoki njee, na ukitok una wanao ama ndugu zake, lazima hatapata pressure na atashtuka. He should always see you loking like a million dollars.

I pry for u to succeed, and be a women n half
Mwambie Ras Simba akurudishie ada yako yote.
 
Unachokitaka utakipata na kitakupata cha kukupata. Mke wa mtu hastahili kuwa na ukaribu sana na mwanaume asiyekuwa ndugu au mumewe.
Mpenzi wa mtu je
anapaswa kujenga mazoea na wanaume wasio ndugu zake ?
 
Back
Top Bottom