pole sana, kesi yako juu ya matendo ya mumeo sio ya kwanza. Natoa lawama kubwa kwa wanaume wenzangu kwa matendo mabaya tunayowatendea wake zetu. Kuna rafiki zangu wa kike well educated with very high profile jobs lakini wanashida na wanaume zao kama zako kupelekea kuchanganyikiwa na wengine ninavyoongea wameshavunja mahusiano ya ndoa. Wanawake wengi mmekua waadilifu na wengi wanaobadilika tabia katika ndoa husababishwa na waume zao. Waume hasa generation hii, huendeleza tabia zao za kabla ya kuoa ikiwepo kujali zaidi na kuthamini marafiki na kutumia muda mwingi na marafiki kuliko rafiki zao, kurudi nyumbani usiku wa manane kila siku, kutoka out zaidi na marafiki kuliko wake zao. Kunywa pombe kipita kiasi kupelekea low sperm count na kushindwa ku perform home. Kudharau wake na kufanya ngono sana nje na kushindwa kuwaridhisha wake zao. Mbaya zaidi hawatunzi familia kabisa hususani pale wake zao wanapokuwa na kazi za maana huwa ni mzigo mkubwa kwa wanawake. Imefikia mahali mwanamke hasa msomi economically independent anauma kuwa na maisha mapya. Mjini hapo, wale wasioweza kutoka kwenye ndoa wanatunza ndoazao kwakuwa na relathionships nje ya ndoa ambazo huwa zinawariwadha sana na kuwafanya wajione wanawake kama unavyojisikiawewe. Inafika mahali mwanaume hawala ndio anamshughulikia mke wa mtu kwa kila kitu hata kumpeleka kliniki mwanamke anapokuwa mjamzito. Kwakweli, sisi wanaume wa sasa ni shida tumebaki kudai haki zetu na heshima wakati hatutimizi wajibu wetu. Wanaume tunapaswa kuelewa kuwa it is our primary responsibility ku take care of our family for one hundred percent regardless of wife's financial muscles, mwanamke akiwa na mali ni added advantage lakini tunapaswa kumlisha, kumvisha, malazi, matibabu, elimukwa watoto, tujifunze kutokuwa tegemezi au kusaidiwa wajibu wetu na wake zetu.
Sasa wewe dadangu kwa kesi yako sikulaumu kwakuwa mumeo ndiye aliyekusababishia hivyo and believe me mumeo hawizi kubadilika wako wengi wa aina hiyo. Huyo jamaa yako uliyefall ni mtihani sana kwako kwakuwa mnafanyakazi pamoja. Nimeona na nina marafiki wengi wa kike ambao ndo zao hazifai kabisa wanaishi maisha ya kuwa na boyfriends ila hawafanyikazi pamoja. Sikushauri uwe nae huyo jamaa kwakuwa lazima itafahamika tu na utapoteza integrity yako na heshimu ebu jitahidi kujizua ingawa ni ngumu. Pole sana