Nimeoa single mama

Nimeoa single mama

Ndoa yenu na iwe heri....

Nimewaza kukaacha katoto kangu miaka 2 masikini, kisa mbo0o0 aaah mamaeeeehhh ishia kule kafie mbali haipo hii

Huyu nae muoaji chenga tuu ni bora angemchukua huyu mtoto akamlea tuu hakuna shida yeyote tena angekuwa amemuwin mama yake asilimia mia! Mwanamke akitaka kukitembeza atakitembeza tuu wala si mpaka amtafute aliyezaa nae.....

I bet hawa lazima washindwane mapema na huyu ni mwanamke wa ajabu sana yani mtoto wa miaka miwili unamuacha kisa kukimbilia ndoa....
 
Mwambie akuonyeshe kaburi la Baba mtoto kabisa........usije kulaumu watu hapa??siku ukiambiwa napereka mtoto Kwa Baba ake ukae kimya watu wakapashe kiporo
 
Hii nchi mpo wewe na Masanja tu akili zenu.

Kama ana mtoto wa kike,sawa! Ila kama wa kiume jipange mbeleni.
 
Kuna watu wana comment humu ila ukichunguza wamelelewa na wanaume ambao sio baba zao na leo wanaanua midomo siwez kuoa sijui kusaidia mtoto wa mtu, ndugu zangu tuweke akiba ya maneno hatujui mama zetu wamejitoa kwa kias gani na wamedhalillika namna gan mpaka leo tumekuwa watu wazima,
Kuna uzi uko humu walolelewa na mama tu wametitirika balaa hadi huruma mama zao walivyopigana hadi wamefika hapa..ajabu humu wanachamba na kujiona bora
 
Habarini wakuu,

Wiki hii nimeoa single mom, mtoto wake ana miaka 2 tangu azae jamaa alikimbia na hajulikani alipo hadi sasa hakutoa hata mia kwenye malezi ya mtoto, alisaidiwa kulea mtoto na mama yake, mtoto kamuacha kwao na mimi sitaki kuishi na huyo mtoto wake na yeye ashalikubali hilo maana tangu uchumba wetu wa mwaka mmoja, nishamwambiaga sitokaa na mtoto wako.

Ananipenda sana tena ile sana sijawahi kupendwa kama hivi kwa huu umri wangu wa 29 years nimewaacha wengi sana nimeamua yeye kumuoa nimeona hatasumbua kwa chochote maana ni mpole na msikivu sana.

Nimekuja tu humu kuwapa hiyo taarifa na kuja kuona mnaniusia wosia gani, kwa hiyo karibuni kwa maoni ya jinsi ya kuishi nae, na vitu gani nijitahadhari navyo, ushauri wowote pia unaruhusiwa na chochote ulichonacho cha kuniambia hata kiwe kibaya sawa tu karibu sana.
Kizuri unaoa kwa utashi wako haina shida ila kibaya ni kwamba umejichanganya shabani Kaoneka 😂
 
Anakuzuga tu kuwa jamaa hatoi matunzo jua fika mpaka alibeba mimba take basi alimkubali jamaa-jiandae tu kuyombewa hapo badaye.
 
hadi saiv ananitambua kuwa mi ndo baba ake,naongea nae na ashatambulishwa kuwa mi ndo baba ake,ila aliambiwa akae na bibi ake tu
Kwa muandiko huu hakuna Mwanaume hapo,
Endelea kulelewa akikuchoka atarudi kwa baby dady wake wayajenge,

Mtoto wa miaka 2 unambagua! Aisee
 
huwa hawasiliani nae tangu mimba ikiwa na miez mitano jamaa alisepaga , kweny mawasiliano sijawahi kumwona anawasiliana nae,,pia kwa sabab mtoto hatukai nae atakuwa anampigia bibi ake kumuulizia habar za mtoto.
Huyo mwamba akijua tu kuwa bidada kaolewa, chances za yeye kurudisha majeshi ni kubwa sana. Kama akili za huyi mkeo ni ndogo, lazima mwamba atamla, ndoa yako itaingia doa au kufa kabisa. Omba Mungu awe mke mwema.
 
Back
Top Bottom