Katika kosa ulilofanya ni hilo la kumwekea mtego!! kama unampenda kwa dhati mumeo huwezi kumwekea mtego,We kama mke mwema kama uliona dalili hizo ungemuonya mapema kwamba mume wangu siiependi hiyo tabia uiache ingekuwa vyema sana lakini ishu za kuwekeana mitego ndio mwanzo wa kuvunja ndoa yenu mnaachana halafu mwisho wa siku anakuja kumuoa shoga yako!! halafu tatizo lenu wanawake huwa hamfikirii mbali,Hata ukivunja ndoa wanaume wa kipindi hiki sio kama wa enzi zile utaumiza tu roho yako bure utapata mume mwingine atakuwa na tabia mbaya zaidi kuliko huyu mwingine hivyo uache tabia hizi za mitego ,Vipi kama mumeo angeshtuka achukue simu ya shoga yako aizime na waende sehemu nyingine ingekuwaje?? Kama unaona mumeo anaenda tofauti mkalishe chini mwambie anapoelekea sio na sio kuanza kumuwekea mitego