Umemtumia rafiki yako kumfumaniaje tena wakati ulipanga na rafiki yako!?
Unashangaza kama mwanamke, sasa huyo rafiki yako ukikuta kesho amempa penzi analolitaka miaka yote utafanyaje?
Wewe kama mke ulishindwaje kuyamaliza na mume bila kumtumia rafiki yako.
Unajua wqnaume wanajua kujibu kwa visasi, unamlazimisha akubali nini tena wqkati umemfumania kama unavyodai? Umejichemshia maji ya moto.
Natabiri kumeo kufanya ambayo hata hukutegemea, kwanza umemshushia hadhi kwa kumuabisha live, na walivyo na vinyongo eeeeeh
Umeokoa kwa rafiki, subiri kupata wenzakonhata kumi na watoto wake huko nje.
Haya mambo yanataka utumie akili, kwangu mimi umechemka vibaya mno. Ungetumia njia zingine kuyazima hayo anayofanya. Unalo kama unamjua vizuri basi jaribu kujenga na sio kwenda unapiga tarumbeta kila mahala kumsema.
Usisahau kumchunga huyo rafiki yako aliyekubali kutenda mliyotenda, hakutakii mema. Angekuwa anakutakia mema angetumia njia ingine kumuonyesha kuwa amekuambia na hujui leo kaambiwaje kwa hizo dakika chache na labda kapenda ha ha haaaaa
Kila la kheri.