Nimemfanyia upasuaji mwanamke aliyenikataa

Nimemfanyia upasuaji mwanamke aliyenikataa

mandokwa

JF-Expert Member
Joined
Jun 5, 2013
Posts
620
Reaction score
865
Hii Dunia ina mambo kabisa,

Kuna binti amekuwa akinikataa kwa muda mrefu sana amekuwa akinikataa kwamba sifit vigezo vya kumuoa. Nilimpenda sana hadi basi but ikashindikana hadi ikanibidi nioe mke mwingine.

Baada ya miaka kadhaa jana nikapangiwa kumfanyia operation mwanamke baasi paap namkuta ni yuleyule aliyeninyanyasa.

Basi baada ya nurse kumaliza kumuandaa nikafika kumuona huyo mgonjwa iliniuma sana kwani pamoja ya kwamba nilimpenda lakini sikutaka kumchezea au kumvunjia heshima. Nikamuuliza kama anaamani kufanyiwa operation nami akanijibu nakuamini endelea tu.

Mungu amjaalie afya njema.

============================
Nadhani watu wengi mnashindwa kuelewa maana ya maadili. Maadili katika kazi zetu ni pamoja na kuhakikisha taarifa za mgonjwa na ugonjwa wake unabaki kuwa siri ya daktari husika mpaka pale mgonjwa atakapo ruhusu vinginevyo. Kusema huyu mgonjwa ni ndugu yangu au mke wangu sio katika kukosa maadili. kusema kwamba nilipoingia kumhudumia nilijihisi uncomfortable sio kukosa maadili.

lamwisho, msidhani kwamba madaktari wote tunasahau habari zote za mgonjwa mara baada ya kumhudumia. sio kweli, wapo wadaktari ambao huendelea kuwa na contact na wagonjwa na wengine huendelea kuwa na mahusiano baada ya kuwahudumia vizuri. wapo wagonjwa wakishahudumiwa vizuri hulazimisha kila akija hospitali ahudumiwe na the same doctor. Na wakati wmingine wapo wagonjwa ambao huwasumbua madaktari ambao waliwahudumia vizuri . so kama una mke wako anakuambia kila siku anaenda kwa dr.flani kuwa makini fuatilia.

======
kwa wale ambao mnaweza kusoma naomba msome kitabu cha Ben Carson "Gifted hands " ndani yake kuna simulizi nyingi sana ambazo zinahusu jinsi alivyohudumia wagonjwa wake.... sijuwi kama mnaweza kusema hajui ethical codes...
 
Dr ulikuwa stable psychologically kufanya hiyo operesheni?
 
Nilikuwa najisikia vibaya kumuona maeneo yake mtu ambaye akiwa mzima hakutaka niyaone. Hili ni sawa ukitakiwa umfanyie operation mama au dada yako. sio kazi rahisi mjue nasi ni binadamu.
 
Eti iliniuma sana,uliumia nini sasa!kwahiyo ukaona kama nawe umejibu mapigo,utabakia kuangalia tu mkuu,timiza wajibu wako wa kazi,hata mkeo kule nyumbani siku moja ataumwa na atafanyiwa operation na wanaume wengine nao watamchungulia,afterall umeoa achana na kuwazia hayo makitu,hana tofauti na yule uliemuacha nyumbani,unajidanganya tu..
 
Acha uongo wewe,kama unadhan kutumia jina la dokta humu JF ndo utampata wanawake umejidanganya.

Hakuna dokta asiye na siri kama wewe. Hujui miiko ya kidokta. Usichafue fani za watu
Sema hakuna Dr ninayemfahamu asiye na siri!Kuna visharobaro vimekua ma Dr vinaongea upuuzi wakiwa bar hadi unashangaa,kila fani imevamiwa
 
Back
Top Bottom