Ndugu yangu pole sana.
Ilinitokea miaka fulani nikiwa nasaka demu wa kuzugia kisiwani Unguja.
Nikakutana na mabinti warembo watatu Forodhani wapo kwenye kimkeka na keki kubwa ya birthday.
Nilikaa pembeni yao, mmoja akaniomba niwapige picha, mazoea yakaanzia hapo.
Nikaja kugundua ni wanafunzi wa Chuo kikuu Tunguu.
Nikaona niwape ofa ili walau nitanue wigo wa kunizoea ili nimpate mmoja wao.
Nikaanza na juice za miwa glass kubwa tatu (3,000/-)plus chips sahani tatu (4,500) na mishikaki ya kuku miwili kwa kila mmoja (6,000)
Baada ya muda wakasema wana hamu na shawarma-wakati huo ilikuwa 3500 la pack moja (10,500/-). Jumla nilimaliza kama 24,000/-
Kufikia saa tatu usiku kabla sijaomba namba ikaja kirikuu wakaniaga na kuondoka.
Dah, safari ya kutoka Forodhani kwenda Mkunazini nilipokuwa naishi ikawa ndefu sana. Nilihisi kuumia sana moyoni yaani 24,000/- nimeimaliza bila kuambulia chochote.
Baada ya wiki nikiwa Restaurant fulani maeneo ya Malindi pale karibu na benki ya Exim; ghafla nikaitwa Uncle Uncle, kugeuka hivi ni yule binti aliyekuwa na birthday.
Kutokea hapo sikujutia ile 24,000/- maana ilikuwa ndio msingi wa kuniwezesha kula vitu vinono.
Usife moyo baharia, ipo siku utaanza kula faida ila pia hasara inaweza kutokea.
Alamsiki.