Nimekuja kumegewa siri hii baada ya miaka mingi!

Nimekuja kumegewa siri hii baada ya miaka mingi!

Salaam, nimekuja kujua kitu kilichonitonesha kidonda changu, na kinaendelea kunitonesha. Ni kuwa nikiwa na miaka 7 au 8 hivi, mama yangu mzazi alitaka kuniua, kwa mujibu wa aliyenisimulia ni kuwa siku moja alinikaba mno shingoni ili aninyonge, baadaye roho ya huruma ikamuingia mara baada ya kuona naanza kutoa macho na kukosa nguvu, akaniacha. Anasema kuwa mama alishadhamiria kunimaliza, alishapanga.

Nakumbuka nilikuwa mtundu, ndiyo sababu kuu iliyopelekea kutaka kuuawa, haya nimeyajua nikiwa MTU mzima hivi hivi! Nimehuzunika sana!

Ila mama hajui kama nimeshajua, nafikiri alitaka iwe siri.!
Na ile siri alotaka kukwambia baba ako vipi ameshakwambia?
 
Yaani ulikuwa na miaka 7/8...

Ulikabwa sana koo kiasi cha kukaribia kutolewa uhai...

Lakini huna kumbukumbu yoyote juu ya tukio hilo???

Binafsi siamini kwamba mtu hakumbuki matukio yaliyomtokea katika umri huo!!!! maana mimi naweza kumbuka hadi vitu nimefanya au fanyiwa nikiwa na 5yrs...

7/8 yrs huo ni umri akili imeshakomaa na mtoto enzi hizo yupo like std 1 or 2 or 3...
 
Mkuu na wewe utakuwa ulipitiliza utundu alaf tukio kama ilo unashindwaje kulikumbuka mbona mimi nakumbuka vitu vingi tu nikiwa na huo umri mpaka ukumbushwe na uyo aliyekukumbusha amejuaje kama ulikabwa nusu kufa kama sio mbea
 
Mkuu na wewe utakuwa ulipitiliza utundu alaf tukio kama ilo unashindwaje kulikumbuka mpaka ukumbushwe na uyo aliyekukumbusha amejuaje kama ulikabwa nusu kufa kama sio mbea
Halafu ashindwe kukumbuka wakati kasema alikuwa na miaka 8?
Eight years ni mkubwa sana hauwezi kusahau ujue.
 
Duh nimecheka
Mkuu huyu ukute unakutana nae kwenye kona anakupiga kabali halafu anaongea kiingereza..😬
Yani unajua kabisa ni msomi! Akileta stori Kama hii si tutasema heri mama asingeachia shingo ya jamaa😂
 
Salaam, nimekuja kujua kitu kilichonitonesha kidonda changu, na kinaendelea kunitonesha. Ni kuwa nikiwa na miaka 7 au 8 hivi, mama yangu mzazi alitaka kuniua, kwa mujibu wa aliyenisimulia ni kuwa siku moja alinikaba mno shingoni ili aninyonge, baadaye roho ya huruma ikamuingia mara baada ya kuona naanza kutoa macho na kukosa nguvu, akaniacha. Anasema kuwa mama alishadhamiria kunimaliza, alishapanga.

Nakumbuka nilikuwa mtundu, ndiyo sababu kuu iliyopelekea kutaka kuuawa, haya nimeyajua nikiwa MTU mzima hivi hivi! Nimehuzunika sana!

Ila mama hajui kama nimeshajua, nafikiri alitaka iwe siri.!

Msamehe Na haikuletei Faida yeyote kuyawaza
 
Huyo aliyekwambia ndio mchawi

Mchonganishi


Mharibifu

Ana husda


Na shetani


Mkimbie.
 
mkuu huyo aliekwambia kama sio mama yako mzazi basi jua ni mchawi. alikuwa wapi asimzuie wakati anataka kukunyonga
utaharibu familia yako kwa kumchukia mama yako.
 
Na huyo aliekuambia mchawi tuu
Lengo lake pia la kukuambia kwa umri huu nini yaani kwanini akuambie hio taarifa ungepewa na mama yako
Kama mpo fresh na mama yako muulize kwenye maongezi rahisi tuu kuhusu hilo jambo na mwonyeshe kwamba hulitilii maanani kwasababu kwa sasa lazima mama yako ni mtu mzima sana isije ikawa hilo jambo linamsumbua sana kichwani ana kosa raha ila kukuambia hawezi hapo inakuwa ni jukumu lako kuhakikisha linamtoka kichwani huyo ndo mama yako huwezi kubadilisha hilo
 
Kwamba umetendewa tukio ukiwa na miaka 7 ila wewe hulikumbuki mpaka uhadithiwe?
 
Miak 7 una sahauje tukio kama hilo? Hizi chai za saivi mna weka chumvi sana
 
Umenikumbusha tukio!

Mama yangu aliwahi kunishikia kisu nikiwa na miaka 7!! Nilirudi kutoka shule nikiwa natembea kwa kutanua miguu.. nilikua nimevimba nodes za kwenye mapaja, alinishika akaniingiza chumbani kwake nimwambie ukweli nimefanya nini nkimdanganya atanichinja!

Baadae aliniachia baada ya kugundua ni nodes tu ndo zimevimba..
 
Umenikumbusha tukio!

Mama yangu aliwahi kunishikia kisu nikiwa na miaka 7!! Nilirudi kutoka shule nikiwa natembea kwa kutanua miguu.. nilikua nimevimba nodes za kwenye mapaja, alinishika akaniingiza chumbani kwake nimwambie ukweli nimefanya nini nkimdanganya atanichinja!

Baadae aliniachia baada ya kugundua ni nodes tu ndo zimevimba..
Bimkubwa alizani ushabanduliwa na wahuni...😅, ila mama alikushikia kisu kwa nia safi tu ya kutaka useme ukwelli, ni alikutishia tu hakuwa na nia ya kukuchoma nacho
 
Salaam, nimekuja kujua kitu kilichonitonesha kidonda changu, na kinaendelea kunitonesha. Ni kuwa nikiwa na miaka 7 au 8 hivi, mama yangu mzazi alitaka kuniua, kwa mujibu wa aliyenisimulia ni kuwa siku moja alinikaba mno shingoni ili aninyonge, baadaye roho ya huruma ikamuingia mara baada ya kuona naanza kutoa macho na kukosa nguvu, akaniacha. Anasema kuwa mama alishadhamiria kunimaliza, alishapanga.

Nakumbuka nilikuwa mtundu, ndiyo sababu kuu iliyopelekea kutaka kuuawa, haya nimeyajua nikiwa MTU mzima hivi hivi! Nimehuzunika sana!

Ila mama hajui kama nimeshajua, nafikiri alitaka iwe siri.!
Hivi inawezekanaje ulikua mtoto usikumbuke vitendo vya ukatili mpaka usimuliwe na mtu baki
 
Salaam, nimekuja kujua kitu kilichonitonesha kidonda changu, na kinaendelea kunitonesha. Ni kuwa nikiwa na miaka 7 au 8 hivi, mama yangu mzazi alitaka kuniua, kwa mujibu wa aliyenisimulia ni kuwa siku moja alinikaba mno shingoni ili aninyonge, baadaye roho ya huruma ikamuingia mara baada ya kuona naanza kutoa macho na kukosa nguvu, akaniacha. Anasema kuwa mama alishadhamiria kunimaliza, alishapanga.

Nakumbuka nilikuwa mtundu, ndiyo sababu kuu iliyopelekea kutaka kuuawa, haya nimeyajua nikiwa MTU mzima hivi hivi! Nimehuzunika sana!

Ila mama hajui kama nimeshajua, nafikiri alitaka iwe siri.!
Kuna kitu ninawasiwasi nacho aliekuambia labda ana nia ugombane na mama yako, hivi kwa ukatili wote huo aliofuanya mama yako ushindwe wewe mwenyewe kuukumbuka mpaka usimuliwe
 
Unachonganishwa na mama yako na kwanin awe comfortable kukuambia hayo mambo
Huwa unawafikiliaga sana kabla ya kuandika jambo comment nyingi naona, na hongera sana, mimi nimejiuliza swali hilo hilo je ameambiwa ndiyo kastuka kuwa mama yake alitaka kumuua hiv katika hali ya utoto unashindwaje kukumbuka vitendo vya ukatili, mimi. Nimewaza pia aliemwambia anataka wakosena na mama yake
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom