Mkulungwa01
JF-Expert Member
- Jul 14, 2021
- 3,977
- 5,352
Salaam, nimekuja kujua kitu kilichonitonesha kidonda changu, na kinaendelea kunitonesha. Ni kuwa nikiwa na miaka 7 au 8 hivi, mama yangu mzazi alitaka kuniua, kwa mujibu wa aliyenisimulia ni kuwa siku moja alinikaba mno shingoni ili aninyonge, baadaye roho ya huruma ikamuingia mara baada ya kuona naanza kutoa macho na kukosa nguvu, akaniacha. Anasema kuwa mama alishadhamiria kunimaliza, alishapanga.
Nakumbuka nilikuwa mtundu, ndiyo sababu kuu iliyopelekea kutaka kuuawa, haya nimeyajua nikiwa MTU mzima hivi hivi! Nimehuzunika sana!
Ila mama hajui kama nimeshajua, nafikiri alitaka iwe siri.!
Nakumbuka nilikuwa mtundu, ndiyo sababu kuu iliyopelekea kutaka kuuawa, haya nimeyajua nikiwa MTU mzima hivi hivi! Nimehuzunika sana!
Ila mama hajui kama nimeshajua, nafikiri alitaka iwe siri.!