Nimekoma, yule mwanamke ni chuma ulete

Street brain

JF-Expert Member
Oct 24, 2022
486
606
Habari wana jf,

Moja kwa moja kwenye mada, katika pita pita hapa na pale nikiwa mkoani manyara alimaarufu kama mkoa wa Wambulu mix Wamasaai na wengine wanajiita Wairaq sijui kwanini wanajiita hio ila ni walewale Wambulu lugha ni moja kila kitu.

Siku moja ilikuwa ni siku ya mnada ndani bahati sehemu moja hivi wanaita Gendi kwa mwenyezi wa maeneo hayo atakuwa anapafahamu, siku kama hiyo soko huwa linajaa kila aina ya bidhaa na kila mtu akijaribu kutafuta riziki yake.

Sasa siku hiyo jamaa angu mmoja akaniomba nimsindikize huko mnadani, nikavaa freshi kadeti yangu kali nikatupia tisheti ya maua maua tukaelekea mnadani, daah tulipofika huko moja kwa moja tukaelekea sehemu moja wanauza nguo za mitumba, jamaa angu akachagua pale.

Mimi nikiwa naangalia angaza macho huku na kule tukagongeshana macho na mwanamke mmoja wa Kimbulu, alikuwa na shape no 8, sasa sijui ikawaje huyo mwanamke ananiangalia kama ananijua na mimi huku ghafla nikamtamani, yule manzi akawa anajizungusha ile sehemu lakini macho hayatoki kwangu na kila nikimtazama na yeye ananitizama halafu tunakwepana, yaani ni kama alikuwa ananiambia nimfuate kwa kutumia lugha ya macho.

Sasa nikamstua jamaa pale nikamueleza akasema tumfuate lakini ni kama yule mwanamke anakuja upande wetu, alipofika tulipokuwa akajaribu kujichagulisha nguo halafu akaondoka mimi hata sikumsalimia nikaona.

Anarudi tena daaaaah nikasema hapa simuachi nikamgusa mkono akageuka nikampa hi akaitika hi, nikamuuliza vipi mbona unaniangalia sana akajiona aibu akasema samahani kaka nilikuwa nakufananisha na mtu fulani, nikamuuliza unaishi wapi akajibu Babati karibu na kanisa la katoliki, ilikuwa ni karibu na sehemu ninapoishi mimi.

Nikamuomba no akanipa nikasema nitakuchekI mida nikaondoka na jamaa angu. Imefika muda fulani hivi ya night, yaani nishatoka mnadani nikamcheki akapokea, nikamueleza mimi ni yule wa mnadani akanipata akaniuliza kama hiyo ni no yangu akaisave, so siku ikapita.

Siku moja ilikuwa siku ya Jumamosi nikamcheki kwenye phone akapokea, nikamuuliza muda huo ana kazi gani ili tukapate lunch pamoja, akasema anajiandaa na safari ya kwenda chuoni UDSM, alikuwa anaenda kuchukua bachi ya law. Nikamuuliza anaondoka akaniambia wiki moja mbele, nikasema siyo mbaya tukikutana ili tufahamiane zaidi akasema siyo mbaya.

Siku ya Jumanne tukameet mida ya jioni kwenye restaurant fulani hivi, pale Babati inaitwa UZUNGUNI CITY PARK wenyeji wanapaelewa, so nikaagiza pale dinner mimi nikaagiza pizza yeye akaagiza ugali nyama tukala huku tunaongea.

Siku hiyo nilijipanga kisawasawa kuhakikisha hachomoki salama kwenye huo mtego, mwanamke alikuwa mkali, maji ya kunde, yaani kiufupi pale restaurant kila mtu alihusudu urembo wake. Nikatupia ndoano mwanamke akanasa ila kwa masharti matatu, yaani nimpende kweli, nimjali, nisimdanganye.

Nikasema hayo hayana shida, nikamuomba twende apaone hata pale ninapoishi, akakubali, nikasema hapa ni afe kipa afe beki. Oóh my ghossh, tukafika home, tukaingia ndani akakaa kwenye sofa pale, so namimi nikamsogelea sasa akawa kama hataki nimsogelee sana.

Hilo nikalijua, nikatumia mbinu moja nikamuomba simu yake akanipatia, nikamuambia anirushie baadhi ya picha zake. Hapo ndipo alikosea, maana wakati anasogea kuchua simu ili asican xender akanisogelea simu yake ikawa inasumbua kuscan, ikabidi anisogelee karibu.

Sasa vile kuhemeana karibu uzalendo ulinishinda pale pale, nilikuwa kama akili yangu haipo. Nilimshika kiuno nikamsogelea zaidi, nikaona hakatai wala hafanyi lolote. Ile kumsogelea akasapoti akanikalia kwa juu nikamchezea pale huku anatoa miguno ambayo nilijua zilikuwa ni miguno ya kimahaba, nikambinua ili niwe juu yake.

Nikapitisha mkono ikulu kwake ili nilambe asali akaushika mkono wangu na kuisukuma kwa nguvu, nikajaribu tena kagoma kabisa. Haikuwa kesi nikamuacha akaanza kunililia akilalamika kumbe simpendi lengo langu ni kumchezea tu, nitajitahid kumuweka sawa kumuminisha kuwa nampenda na kilichotokea nilishindwa kujizuia akanielewa.

Siku ya kuondoka chuo ikafika akaniomba nimsaidie laki 2 ya matumizi nikampa. Akaondoka UDSM, alipofika huko maigizo yakaanza. Aiseee yule mwanamke alikuwa ni chuma ulete sijawahi ona, siku moja tu ndiyo amefika Dar akaniomba tena elfu 50 nikampa. Shida kwake alikuwa nduguye, yaani shida hazikauki utadhani mimi ndiyo mzazi wake.

Sasa yaani hadi ada aliiomba nikasema hapa mpaka tukutane, nikamueleza aje Dodoma namtumia nauli, akaja siku hiyo nilikuwa na langu jambo kupiga na kupotea. Mwanamke akaja Dodoma tukaenda zetu lodge kilichotokea ni siri yangu na yeye.

So nikamuambia arudi chuo halafu ada namtumia, alipofika UDSM kama kesho akanicheki kuhusu ile ada nikamwambia subiri wiki ijayo harakati hazijakaa vizuri akaelewa. Akanicheki tena siku nyingine akidai hana hela ya kula hadi hata mkopo amekosa, hapo nilicheza kama Pele yaani kiliweka kindege.

Finally nikamblock hadi sasa anakitafuta kwa namba nyingine, nikisikia sauti yake na hiyo namba nablock. Yule mwanamke ni chuma ulete, mchunaji na mvunaji.
 
Back
Top Bottom