Nimekata tamaa ya maisha nahitaji msaada

Nimekata tamaa ya maisha nahitaji msaada

Mkuu pole sana na hongera pia maana una spirit ya upambanaji, believe me utafanikiwa sana mbele ya safari.

Hali uliyonayo sasa tumekutana nayo wengi, huwa hazidumu hufikia hatua mambo yanabadilika.

Nakuombea upate msaada unaohitaji kwa sasa. On the other hand kuna opportunity ya kupata training na funding toka kwenye foundation ya Tony Elumelu (Tony Elumelu Foundation) kama ushawahi kumsikia. Walianza toka 2014, wanatoa mafunzo na pesa kwa wajasiliamali 1000 across African, $5,000 kwa kila mmoja kila mwaka though mwaka Jana hawakufanya kwa sababu ya Covid 19.

Kinachohitajika ni wazo tu la biashara ama biashara ambayo haina zaidi ya miaka mitano. Unatuma maombi and then kuna mambo mengine yanafuata. Nitaweka link hapa kwa faida ya wengine pia kama watakuwa interested. Application ziko open toka January mosi na mwisho wa kuapply ni 31March. Tz tuko nyuma kidogo kwenye hizi mambo. Kenya, Rwanda na wenzetu wa magharibi wametengeza mpaka clubs za kuwasaidia vijana kupata hizo fedha.

TEF website
 
Watanzania sisi ni wanafiki sana, sasa wewe kujua situation yake inamsaidia nini, kwa yeye kua REAL na kusema unamjua, umeshampa msaada gani ?!

Sent using Jamii Forums mobile app
Tuliza mshono huo hata wazazi wako ni watanzania pia ni wanafiki kaa utulie unataka msaada nikuambia sipend shobo
 
12,000/= kwa siku nafasi gani?
Mkuu kukusaidia nenda mwanza kuna kiwanda cha kutengeneza nondo kinahitaji wafanyakazi malipo 12000tshs per day,kipo veta kiregesh kuelekea buswelu kinaitwa nyakato industry
 
Maisha ni magumu kweli, ila jambo muhimu ni kutokata tamaa.
Asante kwa kunitia nguvu kaka, kuna muda unaomba sana Mungu, unakuwa mtu loyal kabisa na unapambana ila hii ya kushindwa hata kuafford foos for my self it very difficult to feel as normal issue, unaweza kuwaza hata kujiua maana unalaza buti aaah wapi yaani maisha haya jamani acheni tu
 
Asante kwa kunitia nguvu kaka, unajua mtu unaangaika unatamani umwambie mtu magumu unayopitia ili upunguze ya moyoni, maana unawaza hata kujiua sometimes mambo hayaendi kabisa, unaweza kudhani kuna mkono wa mtu ila Mungu yupo unamuomba hadi unawaza tofauti, sijui ni majaribu au mapito. Nitapitia hiyo link ubarikiwe sharing is caring
 
Brother though mimi id yako sijakuhamu kwa heshima naomba utulie tufanye hili jambo liishe, nathamini uwepo wenu nyote
Tuliza mshono huo hata wazazi wako ni watanzania pia ni wanafiki kaa utulie unataka msaada nikuambia sipend shobo
 
Watu wa humu wengi huwaga hawana msaada wengine watakuponda na kukuongezea machungu nakupa angalizo usishtuke sana.
maoni yangu kwanini usitafute partnership na watu wenye mitaji.

Si ndio anachokifanya hapa mkuu? Anaomba msaada wa kumkwamua kutoka hapa alipo hata ikiwezekana kufanya nae ushirika.
 
Mwenzako changamoto yake sio kuchafuka kwa tope wala kushindwa kusimamia au kuingia shambani, mtaji au pesa ya kuendeshea shughuli za shamba ndio tatizo.

Sasa wewe unaelezea usimamizi wa vibarua na mambo ya boot wapi na wapi? Lakini hongera kwa kuwa na shamba.
 
Mwenzako changamoto yake sio kuchafuka kwa tope wala kushindwa kusimamia au kuingia shambani, mtaji au pesa ya kuendeshea shughuli za shamba ndio tatizo.

Sasa wewe unaelezea usimamizi wa vibarua na mambo ya boot wapi na wapi? Lakini hongera kwa kuwa na shamba.
Mimi naona huyo lengo lake ni kutuonyesha shamba
Maana mwenzie anaelezea kukwama ila yeye anakuja sema shamba halihitaji usharobalo..dah ila nampongeza pia kwa kuwa na shamba.

Anyway
Brother naomba umsaidie huyu kijana mtoa mada please..popote pale utakapoweza
Pls nakuomba mdogo wako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pamoja mkuu. Umefanya vema pia kufunguka hata hapa, mbali na kupata msaada umerelease vitu moyoni. Dunia ina mengi, at least huna familia kwa maana ya mke na watoto kwa sasa, jaribu kufikiria uwe kwenye hali uliyonayo with a family unaweza kuingia kichaa. Me kuna rafiki alipitia wakati mgumu kiuchumi kwa miaka miwili, kuna siku alimwaga machozi mbele yangu na mtu mzima almost 38 years by then. Hana chakula ndani, mtoto anaumwa anatakiwa kufanyiwa operation, hata buku mfukoni hana na marafiki zake wote wamemkimbia. At the end of the day Mungu amemsaidia yuko vizuri now kashasahau na machungu aliyopitia.

Nimechukua namba yako, nikipata neema ntakusaidia hata pesa ya kula chief.
 
Kaka ubarikiwe mno, ni jambo ambalo nimekaa nalo moyoni muda mrefu, kila nikitaka kuandika moyo mzito n.k lakini nafsi ikaniambia uenda hii ikawa nafasi yako nyingine jitahidi uifanikishe nashukuru Mungu, kuna walionipm ushauri wengine connection japo bado sijafanikiwa ila nyote nawashukuru sana ndugu zangu, Mungu awabariki zaidi na zaidi mkinisaidia mimi mtakuwa mmesaidia vijana hata 10 mbeleni tuombe Mungu mambo yaende sawia, tutabebana sote humu
 
Back
Top Bottom