Hongera sana kijana, wanaokuponda hawajui tabu wanazopata ndugu zetu huko vijijini. Mimi nimefanya sana kazi vijijini, nilichokiona ukilinganisha na hawa mafisadi wanavyotoa majibu rahisi kwa maswali magumu ya hatma ya Tanzania unaweza kulia. Mimi namkaribisha kila mtu mwenye nia ya kuikomboa nchi yangu, haijalishi ametoka wapi.
Kazi yetu sisi underground ni kuhamasisha elimu ya uraia ili 2015 ukombozi upatikane kwelikweli, tusisubili DR slaa kuitisha mkutano, mabadiliko yaanzie nyumbani kwetu, mimi nimefanikiwa kumbadilisha mama yangu na mke wangu, nina imani hata mtoto wangu atakuwa cdm siku akikua!!!! Mungu ibariki Tanzania.