Nimeibiwa kiboya kweli, hata sijielewi

Nimeibiwa kiboya kweli, hata sijielewi

Step by step

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2014
Posts
1,184
Reaction score
1,315
Wakuu, naleta kwenu hili ili nipate uzoefu na namna ya kujikinga isitokee tena.
Ni hivi, nina nyumba yenye ukuta wa kozi saba kote na geti na ninaishi mimi na wife tu ndani kuna vyumba viwili havikaliwi na mtu. Sasa naamka nakuta flat sceen na remote yake haipo na mlango mkubwa uko wazi wakati kabla ya kulala niliufunga nakumbuka.

Jamaa karuka ukuta, kachana nyavu ya dirisha, kachukua funguo kafungua mlango kaingia sebleni kawasha taa kazunguka room zote manake nimekuta pamepekuliwa na mashuka yametanduliwa kama alikua anatafuta kitu isipokua chumba nilicholala mimi tu na taa kawasha cha ajabu kabeba hiyo tv na remote yake tu pamoja na raba zangu zilizokua mlangoni nje na kuacha vitu kibao vya thamani ambavyo vilikua wazi tu.

Baada ya hapo katoka na funguo kafungua geti then funguo kazitupa mlangoni. Naamka sioni tv, kuchek mlango umerudishiwa tu kuzunguka nje nakuta funguo zangu ziko nje zimetupwa ikanibidi nicheke tu na kushukuru Mungu.

Katika mazingira ya kawaida sio rahisi mimi na wife kulala hivi lazima kuna ujanja wamefanya hebu tupeane uzoefu na namna ya kujikinga na hizi mambo jamani manake ni hatari sana.
 
Mkuu Pole sana kwa tukio hulo.Na mumshukuru saana mungu kwamba mpo wazima.

Hembu tuambie Weekend yako uliianza vipi na kuimalizia jana kwa style ipi?

Maana kuna Mshkaji wangu yeye alilala nyumba yoote milango wazi,cha ajabu gari aliiacha Bar na yeye akakodi Taxi.
Cha kushangaza kuamka asubuhi akaanza kuitafuta gari na kusema imeibiwa,akaenda vituo vyoote vya Polisi kusema kwamba Gari yake Imeibiwa na nyumba imefunguliwa kwa Master Key.

Sasa alitokea jamaa mmoja mwenzie akamuambia mkuu haujavunjiwa nyumba wala haijafunguliwa,utakuwa ulilala milango wazo,jamaa alimtukana balaa,na kumuambia oyaaa mie ninaakili zangi timamu,siwezi kulala mlango wazi.
Basi jamaa akawa mstaarabu,na kumuambia unajua kwamba gari yajo uliicha Bar?na uzuri Bar yenyewe kwa mlio Zanzibar ni Gymkhana Bar ambapo ulinzi upo mzuri sana.Ikabidi jamaa aliganda akavuta kumbukumbu kwa aibu akasepa wiki nzima mtaani hayupo.

Sasa nakuuliza kujua je weekend yako iliishaje mkuu na mlikuwa nanani siku hiyo
 
Ina maana mlango wako hakuna zile koleo za kufunga kwa ndani.Kama hakuna tafadhali weke chini na juu yamkini zingekuwepo mwizi angefungua kitasa lakini angekwama kufungua mlango.

Halafu ndugu yangu kama unaishi wewe na familia tu kwanini usifuge mbwa wana msaada mkubwa sana kama wangekuwepo ingebidi wezi wafanye kazi ya ziada.
 
Wala hujaibiwa kiboya. Aliyekuibia anayafahamu vizuri mazingira ya nyumba yako, chunguza

huwezi amini mkuu yani nimeamka ikanibidi nicheke tu hasa baada ya kujiridhisha kuwa vitu viko salama. Seems alikua anaiotea tv mda mrefu sana lazma ananijua sio bure
 
Mkuu Pole sana kwa tukio hulo.Na mumshukuru saana mungu kwamba mpo wazima.

Hembu tuambie Weekend yako uliianza vipi na kuimalizia jana kwa style ipi?

Maana kuna Mshkaji wangu yeye alilala nyumba yoote milango wazi,cha ajabu gari aliiacha Bar na yeye akakodi Taxi.
Cha kushangaza kuamka asubuhi akaanza kuitafuta gari na kusema imeibiwa,akaenda vituo vyoote vya Polisi kusema kwamba Gari yake Imeibiwa na nyumba imefunguliwa kwa Master Key.

Sasa alitokea jamaa mmoja mwenzie akamuambia mkuu haujavunjiwa nyumba wala haijafunguliwa,utakuwa ulilala milango wazo,jamaa alimtukana balaa,na kumuambia oyaaa mie ninaakili zangi timamu,siwezi kulala mlango wazi.
Basi jamaa akawa mstaarabu,na kumuambia unajua kwamba gari yajo uliicha Bar?na uzuri Bar yenyewe kwa mlio Zanzibar ni Gymkhana Bar ambapo ulinzi upo mzuri sana.Ikabidi jamaa aliganda akavuta kumbukumbu kwa aibu akasepa wiki nzima mtaani hayupo.

Sasa nakuuliza kujua je weekend yako iliishaje mkuu na mlikuwa nanani siku hiyo

nilikua ok boss na wala sikulala nikiwa nimelewa ndo mana mpaka sasa siamini nabaki kucheka tu. Milango nilifunga mimi ndo mana kachana nyavu na kuchukua funguo. Nadhani alipuliza dawa ya usingizi asingejiamini hivyo mpaka kuwasha taa si bure
 
huwezi amini mkuu yani nimeamka ikanibidi nicheke tu hasa baada ya kujiridhisha kuwa vitu viko salama. Seems alikua anaiotea tv mda mrefu sana lazma ananijua sio bure
Aliyekuibia anakujua vizuri sana,...alikuwa ana kulia timing tu ili afanye yake
 
asante kwa kunitusi mkuu nakuombea usiibiwe wala kutapelia siku zote uwe mjanja tu
Step by Step,acha kupanic mkuu.
Humu JF humu kuna kipindi Jokes kama hizi ambazo ni serious Jokes kuchekeshana .
Hii Stye humu JF huwa inaitwa Raha ndani ya Shida
Yaani wewe umeibiwa,badala ya ushauri watu wanajipa raha kwa jokeskwanza,then we vumilia ushauri unakuja.
Acha kwanza watu waburudike
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom