Ngongo
JF-Expert Member
- Sep 20, 2008
- 18,893
- 31,101
Wakuu leo nimetimiza miezi miwili tangu nihamie Njiro kwa Msolla.Njiro ni sehemu ambayo imepangika (imepimwa)bila shaka hii ni sababu kubwa iliyonivutia kujenga hili kukwepa hadhaa ya msongamano kama maeneo ya Ungalimited,Kambi ya Fisi na Sombetini.
Leo pia nimetimiza miezi miwili kamili bila huduma ya maji AUWSA kila nikirejea nyumbani nalazimika kubeba maji ndani ya gari kwaajili ya matumizi ya nyumbani.Nimejaribu kuuliza majirani na marafiki kadhaa wote kilio ni maji Njiro ni sehemu nzuri sana lakini maji ni tatizo kubwa ambalo linahitaji jitihada madhubuti kukabilina nalngezeko la watu eneo la Njiro na Arusha kwaujumla haliendani kabisa na uwekezaji katika sekta ya maji.Mamlaka ya maji imekuwa imezidi kuwa hovyo tangu Mkurugenzi Mtendaji Eng Asili Munisi astaafu kazi kwa mujibu wa sheria.Chanzo kikuu cha maji mji wa Arusha ni mto Themi na mto Nduruma pamoja na visima virefu vichache sana bahati mbaya hakuna uwekezaji wa maana unaoendana na ongezeko la mahitaji.
AUWSSA Mamlaka ya maji jijini Arusha badala ya kuwekeza kwenye uchimbaji wa visima na mabwawa kwaajili ya kuhifadhi maji wakati wa mvua wameamua kujenga jengo refu kwaajili ya maofisi na kununua magari mapya [Mashangingi] kwaajili ya maofisa wake warasimu.
Naomba kuwasilisha.
Leo pia nimetimiza miezi miwili kamili bila huduma ya maji AUWSA kila nikirejea nyumbani nalazimika kubeba maji ndani ya gari kwaajili ya matumizi ya nyumbani.Nimejaribu kuuliza majirani na marafiki kadhaa wote kilio ni maji Njiro ni sehemu nzuri sana lakini maji ni tatizo kubwa ambalo linahitaji jitihada madhubuti kukabilina nalngezeko la watu eneo la Njiro na Arusha kwaujumla haliendani kabisa na uwekezaji katika sekta ya maji.Mamlaka ya maji imekuwa imezidi kuwa hovyo tangu Mkurugenzi Mtendaji Eng Asili Munisi astaafu kazi kwa mujibu wa sheria.Chanzo kikuu cha maji mji wa Arusha ni mto Themi na mto Nduruma pamoja na visima virefu vichache sana bahati mbaya hakuna uwekezaji wa maana unaoendana na ongezeko la mahitaji.
AUWSSA Mamlaka ya maji jijini Arusha badala ya kuwekeza kwenye uchimbaji wa visima na mabwawa kwaajili ya kuhifadhi maji wakati wa mvua wameamua kujenga jengo refu kwaajili ya maofisi na kununua magari mapya [Mashangingi] kwaajili ya maofisa wake warasimu.
Naomba kuwasilisha.