muafi
JF-Expert Member
- Oct 6, 2015
- 2,117
- 4,808
Ukweli ni kwamba, Ndugai amekua mbabe kwa muda mrefu sana kwa wabunge kule mjengoni lakini alikua mtiifu namba moja wa Rais John Magufuli (R.I.P).
pamoja na mapungufu yote ya serikali ya JPM ikiwa ni pamoja na bajeti hewa mfano kuna baadhi ya wizara zilikua zinapewa hela ya bajeti 18% tu ya zile zilizotegemewa na hasemi,
Kipindi cha JPM mikopo mingi ilikopwa bila kuidhinishwa na bunge, miradi mingi ilifanyika bila kupitishwa na bunge, sikuwai kusikia hata sikumoja ndugai anasemea haya zaidi tu ni kuwa wapinzani walikua wakiibua hizi hoja anawazima,
Ndugai alimtii sana JPM na alimuheshimu kama Rais kamili
Tatizo lilikuja tu alipoapishwa Rais mwanamke, nafikiri hapa tatizo ni jinsia
Ndugai alianza kuota mapembe nakumbuka mtiririko wa visa Ndugai mbele ya hadhara na Media anasema "mwanamke ni mwanamke tu, huwezi kujilinganisha na mwanaume, unaenda kila sehemu unajisema wewe ni mwanamke kwani nani hajui? " hapa ni dhahiri kabisa Job alimlenga Rais na ukifuatilia clip ile ni wazi kabisa alikuwa akimteta Samia Suluhu.
Mbali na hilo nakumbuka siku ya kupokea fedha za uviko ile hafla Ndugai alipopewa nafasi ya kuongea ni kama vile alikuwa anafokea watu, Ndugai alikuwa akilalamika waliopanga ujenzi wa madarasa wapange kulingana na idadi ya watu wa kwenye majimbo, ni kweli kauli yake ilikuwa na mantiki lakini kwa namna alivyoongea ni kama vile alikuwa anafokea watu, imagine Sehemu ambayo na Rais yupo unaongea kama unafokea watu as if wewe ndio kiongozi mkuu upo unahutubia watoto, nilijiuliza sana siku ile ila nikanyamaza,
Hii ya kuhusu mkopo wa juzi huyu Job inawezekana alichoongea kina mantiki lakini ni kwa namna gani alikiwasilisha, alikuwa anamfokea nani pale? Ni kama vile alikuwa anamfokea aliyefuata huo mkopo, na kwanini ahusishe mkopo ule na uchaguzi wa 2025? kwanini aliwahii kisema uchaguzi wa 2025 tutaamua wenyewe?
Aisee itoshe tu kusema Ndugai aliota mapembe akaanza kujiona yeye ndio mkuu wa nchi Ndugai hana uchungu wowote na nchi hii isipokua hamataki Rais Samia, na hamtaki kwasababu ni mwanamke kiufupi Ndugai ana dharau hafai kuendelea kuwa spika wa Bunge amekosa heshima
Afukuzwe iwe fundisho kwa wote wenye dharau za kijinga
Anachofanya ni uhaini, Afukuzwe bila kuonewa haya angekuwa na uchungu na hii nchi asingeacha JPM akaenda kukopa mikopo ya kibiashara tena ya muda mfupi, angalia leo hii hata reli ya SGR haijakamilika lakini mikopo yake imeshaanza kurejeshwa tena na Riba juu, Ndugai alikuwa halijui hilo? Ndugai anajua nchi inapoteza shingapi kwa kuwalipa wabunge wasio na vyama? Ana uchungu gani na hii nchi huyu mtu analeta chuki zake binafsi dhidi ya Rais
Nataka kumwambia Job acheze na wabunge wake huko Taasisi ya Urais aachane nayo, dharau zake apelekee wagogo huko
pamoja na mapungufu yote ya serikali ya JPM ikiwa ni pamoja na bajeti hewa mfano kuna baadhi ya wizara zilikua zinapewa hela ya bajeti 18% tu ya zile zilizotegemewa na hasemi,
Kipindi cha JPM mikopo mingi ilikopwa bila kuidhinishwa na bunge, miradi mingi ilifanyika bila kupitishwa na bunge, sikuwai kusikia hata sikumoja ndugai anasemea haya zaidi tu ni kuwa wapinzani walikua wakiibua hizi hoja anawazima,
Ndugai alimtii sana JPM na alimuheshimu kama Rais kamili
Tatizo lilikuja tu alipoapishwa Rais mwanamke, nafikiri hapa tatizo ni jinsia
Ndugai alianza kuota mapembe nakumbuka mtiririko wa visa Ndugai mbele ya hadhara na Media anasema "mwanamke ni mwanamke tu, huwezi kujilinganisha na mwanaume, unaenda kila sehemu unajisema wewe ni mwanamke kwani nani hajui? " hapa ni dhahiri kabisa Job alimlenga Rais na ukifuatilia clip ile ni wazi kabisa alikuwa akimteta Samia Suluhu.
Mbali na hilo nakumbuka siku ya kupokea fedha za uviko ile hafla Ndugai alipopewa nafasi ya kuongea ni kama vile alikuwa anafokea watu, Ndugai alikuwa akilalamika waliopanga ujenzi wa madarasa wapange kulingana na idadi ya watu wa kwenye majimbo, ni kweli kauli yake ilikuwa na mantiki lakini kwa namna alivyoongea ni kama vile alikuwa anafokea watu, imagine Sehemu ambayo na Rais yupo unaongea kama unafokea watu as if wewe ndio kiongozi mkuu upo unahutubia watoto, nilijiuliza sana siku ile ila nikanyamaza,
Hii ya kuhusu mkopo wa juzi huyu Job inawezekana alichoongea kina mantiki lakini ni kwa namna gani alikiwasilisha, alikuwa anamfokea nani pale? Ni kama vile alikuwa anamfokea aliyefuata huo mkopo, na kwanini ahusishe mkopo ule na uchaguzi wa 2025? kwanini aliwahii kisema uchaguzi wa 2025 tutaamua wenyewe?
Aisee itoshe tu kusema Ndugai aliota mapembe akaanza kujiona yeye ndio mkuu wa nchi Ndugai hana uchungu wowote na nchi hii isipokua hamataki Rais Samia, na hamtaki kwasababu ni mwanamke kiufupi Ndugai ana dharau hafai kuendelea kuwa spika wa Bunge amekosa heshima
Afukuzwe iwe fundisho kwa wote wenye dharau za kijinga
Anachofanya ni uhaini, Afukuzwe bila kuonewa haya angekuwa na uchungu na hii nchi asingeacha JPM akaenda kukopa mikopo ya kibiashara tena ya muda mfupi, angalia leo hii hata reli ya SGR haijakamilika lakini mikopo yake imeshaanza kurejeshwa tena na Riba juu, Ndugai alikuwa halijui hilo? Ndugai anajua nchi inapoteza shingapi kwa kuwalipa wabunge wasio na vyama? Ana uchungu gani na hii nchi huyu mtu analeta chuki zake binafsi dhidi ya Rais
Nataka kumwambia Job acheze na wabunge wake huko Taasisi ya Urais aachane nayo, dharau zake apelekee wagogo huko