Nimefanyiziwa na rafiki!!!!

Nimefanyiziwa na rafiki!!!!

Dai hela yako bana hakuna kuacha, tafuta watoto wa mjini wape nusu hasara atarudisha mwenyewe.
 
Mkuu Mvaa Tai pesa yako uliyoipata kwa jasho lako italalaje nje kwa miezi saba Mkuu huku jamaa akiendelea kukufanyia usanii wa kutotaka kuongea nawe!? Mfuate kazini kwake Mkuu ukamwambie bila kumung'unya unataka pesa yako haraka sana na ufuatiliaji uwe ni wa kila wiki usimpe nafasi kabisa ya kumuonyesha kama vile hiyo pesa yako ndio umekubali kwamba ameshakudhulumu. Fuatilia kwa karibu sana Mkuu kama ulivyoshauriwa na akina Rocky na Heaven on earth na kama hutajali rudi hapa kutufahamisha matokeo ya ufuatiliaji. Kila la heri.

Ndio marafiki tulio nao kwa siku za leo na uaminifu umekwisha
Huwa sitaki sana kukumbuka marafiki maana ni mengi yamepita
mkuu mfuatilie na kama unafaham ofisi yake mfuate kabisa muonane uso kwa uso umsikilize nakuja na sera gani
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mvaa Tai bora somo umelipata na wakati mwingine uwe makini sana maana marafiki wa sasa sio na unaweza ishia kujiona mjinga wakati mwingine maana unamwamini mtu mpaka mwisho ila anachokutendea unabaki kujiuliza maswali yasiyo na majibu
Chunga sana maana marafiki wako kimaslahi zaidi na wako kutafuta kukuangusha wewe na sio kukupeleka kwenye mafanikio
 
Last edited by a moderator:

Ila nahisi alitaka anipige M15 ile siku ya kwanza, sijui ningekuwa katika hali gani kwasasa

Pole ndugu yangu.....na sasa hivi yupo humu anasoma mbinu zote!!!
Ila Alwatan na mimi nataka ukiipata hyo unikopeshe M (serious)
 
achana nae huyu, life will tell nakuambia!!!!!
Hii dhambi itamsumbua miaka yake yote

Mmenipa uchungu....nilimkopesha rafiki yangu alipungukiwa ada 1.2m na ilikua ni karibu na mitihani so angekosa kadi ya kufanya mtihani. Ni mfanyakazi na najua hadi kiasi cha mshahara wake mpaka ninavyoongea research amemaliza na anagraduate dec 2013. Kila nikimuuliza esa yangu ananipa matatizo ya nyumbani kwao na hii ni toka june 2012. Hata kupunguza japo 50,000 amegoma. Namuachia mungu.
 
mfate huko kazini kwao umwambie unataka hela yako akizingua onana na meneja muajiri wao unaweza kusaidiwa kuwa aluwatan kweli la sivyo ndo umeishakatwa kidesign fulani
 
mmmmh kukopeshana bila maandishi tena hela fupi namna hiyo.....yataka moyo.
 
Mkuu Mvaa Tai pesa yako uliyoipata kwa jasho lako italalaje nje kwa miezi saba Mkuu huku jamaa akiendelea kukufanyia usanii wa kutotaka kuongea nawe!? Mfuate kazini kwake Mkuu ukamwambie bila kumung'unya unataka pesa yako haraka sana na ufuatiliaji uwe ni wa kila wiki usimpe nafasi kabisa ya kumuonyesha kama vile hiyo pesa yako ndio umekubali kwamba ameshakudhulumu. Fuatilia kwa karibu sana Mkuu kama ulivyoshauriwa na akina Rocky na Heaven on earth na kama hutajali rudi hapa kutufahamisha matokeo ya ufuatiliaji. Kila la heri.

huu ushauri akiufanyia kazi,mbona pesa yake atalipwa maana jamaa ataona imekuwa kero.
 
harakati za yahya..........

dawa ya watu kama hao ni kumpotezea mazima.............

bora amekuliza hiyo hela ndogo, kwahiyo umeshamjua ni kijana wa aina gani.

pole sana.
 
duh kikulacho kiko nguoni kwako jaribu kuendelea kumvumilia tu kama alivyokuambia ila taa ya hatari inakaribia kuwaka

Marafiki hawakopeshani bhana wanapeana tuuuu mimi huwa sikopeshi nje ya kiasi ambacho nikizikwa nitalalamika; kama mtu anataka milioni 5 namwambia nina laki 8. Kichwani nishapima kama hazirudi ni poa tu kama msaada kwa jamaa yangu
 
Naam Mkuu Asnam, Mtu yeyote akitaka kukudhulumu jasho lako inabidi iwe kero mpaka kieleweke ili kumpa fundisho na labda kutorudia tena uhuni wake.

huu ushauri akiufanyia kazi,mbona pesa yake atalipwa maana jamaa ataona imekuwa kero.
 
Last edited by a moderator:
Naam Mkuu Asnam, Mtu yeyote akitaka kukudhulumu jasho lako inabidi iwe kero mpaka kieleweke ili kumpa fundisho na labda kutorudia tena uhuni wake.

wakati mwingine inabidi umpotezee ili siku nyingine akihitaji msaada asithubutu kukutafuta.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Nakumbuka nilikuwa na Biashara na rafiki yangu, mimi ndio niliyevumbua ile Biashara nikamshirikisha na yeye, tukawa tunafanya pamoja, Mzigo tunapeleka wote, pesa ikitoka napokea mimi tunagawana sawa bin sawia, siku moja nilimuagizia yeye achukue ile pesa, kilichotokea !!? alitia ndani pesa yooote, niliamua kuiua ile Biashara na hatukuongea kwa mwaka 1, japo tulikuwa ofisi moja, Sikutaka Boss wetu ajue, lakini alihisi kuna kitu kinaendelea kati yetu, japo kulikuwa na maneno yakiendelea kwa kuwa mwanamke ambaye niliachana naye yeye akawa naye hivyo wengine walihisi hicho ndio chanzo cha ugomvi wetu, hii ilikuwa zamani kidogo.
 
Hii story inafanana sana na yangu. Mimi alifika kwangu mtu niliyemsimamia ndoa yake akaomba nimpe hela. Sasa nikawa sina za haraka muda ule na nilikuwa mbali kidogo. Tena alikuwa kwa njia ya kukopa. Sasa kulikuwa na mtumishi mwenzangu alikuwa anakopesha hivyo nikamtaka kama yuko tayari akope nitamdhamini. Nilimdhamini mwaka 2008 2,500,000 na akaahidi atarejesha ndani ya miezi mitatu. Hakurudisha ule mkopo, na simu akawa hapokei. Sasa ninataka nimweke hapa jamvini kwa kuwa ni msomi wa Chuo Kikuu alimaliza degree ya Uchumi mwaka 1996. Siku moja nikakutana naye ghafla maeneo ya bank alishtuka sana, na akaomba ohhh mara vile ngoja jumatatu ya pasaka nitafika. Na hajaonekana hadi leo. Deni sasa limefika zaidi ya 10m. Hawa ndiyo binadamu. Sasa kama anasoma humu, ninataka nimtoe hapa na picha yake na part ya mkataba ili wengine wapate adhabu. Na waajiri waliowaajiri waone jinsi walivyofuga majizi.
 
Nakumbuka nilikuwa na Biashara na rafiki yangu, mimi ndio niliyevumbua ile Biashara nikamshirikisha na yeye, tukawa tunafanya pamoja, Mzigo tunapeleka wote, pesa ikitoka napokea mimi tunagawana sawa bin sawia, siku moja nilimuagizia yeye achukue ile pesa, kilichotokea !!? alitia ndani pesa yooote, niliamua kuiua ile Biashara na hatukuongea kwa mwaka 1, japo tulikuwa ofisi moja, Sikutaka Boss wetu ajue, lakini alihisi kuna kitu kinaendelea kati yetu, japo kulikuwa na maneno yakiendelea kwa kuwa mwanamke ambaye niliachana naye yeye akawa naye hivyo wengine walihisi hicho ndio chanzo cha ugomvi wetu, hii ilikuwa zamani kidogo.

Mkuu Renegade umenikumbusha machungu yangu na hii issue huwa sipendi hata kuiongelea maana bora hata wewe ya kugawana mimi sikupata kitu kwenye ile biashara na kairusha moja kwa moja na kabadilisha kila kitu kiko kwenye jina lake na jamaa alikuwa rafiki yangu mkubwa na nilimthamini kama ndugu yangu ila mwisho niliona nyota nyota bana
 
Last edited by a moderator:
mmetoka kijiji kimoja, mlisoma pamoja, na ni mshkaj wako ILA KWAKE HUPAJUI. Umeweza kumkopesha hela yote hyo kwa kuitwa alwatan tu...Nisikuhukumu kwenye ulichokwisha tenda. "tetea haki yako" hyo hela inaumuhmu kwako kama ilivyokwake. Fkria mwenyewe cha kufanya uipate ila kumbuka hutoipata kwa urahsi.
 
mkuu unanikumbusha miezi michache tu iliyopita mtu tuliyehusiana naye kama huyo mtu wako!!

Mke wake alikuwa anajifungua akaniomba nimkopeshe kiasi kadhaa cha fedha ambacho angerejesha wiki ambayo ingefuata,.

Yeye kama rafiki, jirani na kaka yangu isitoshe tumekulia wote kijijini bila hiyana nikampatia kiasi alichoniomba na kwa sababu mimi nilikuwa na shida pia ila nikampa yeye kipaumbele kwanza nikamuambia kwamba hizo hela nimeazima hivyo arejeshe mapema nimrudishie mwenyewe!!

Kila wakati ananipiga tarehe tuu,..

Mpaka leo hii takriban miezi sita imeshapita hapokei simu yangu wala
kujibu meseji!!

Kiukweli nasema wakati mwingine kuliko kumkopesha mtu bora umwambie hauna ili kuepuka usumbufu wa aina hii..
 
Mkuu Renegade umenikumbusha machungu yangu na hii issue huwa sipendi hata kuiongelea maana bora hata wewe ya kugawana mimi sikupata kitu kwenye ile biashara na kairusha moja kwa moja na kabadilisha kila kitu kiko kwenye jina lake na jamaa alikuwa rafiki yangu mkubwa na nilimthamini kama ndugu yangu ila mwisho niliona nyota nyota bana

Pole sana Mr Rocky, mkionana vp hasemi lolote? Msumbue angalau uambulie nusu hasara!
 
Back
Top Bottom