Nimefanyiziwa na rafiki!!!!

Nimefanyiziwa na rafiki!!!!

ple sana mkuu Mvaa Tai ila kisasi ni cha MUNGU tu so we mwangalie na kumwacha hivyo hivyo ila punguza mazoea na uishi naye kwa akili kubwa sana na uangalifu wa hali ya juu,
madhara ya kisasi:

hujui yeye amejiandaa kiasi gani akiwa ana uhakika kuwa iko siku utaujua ukweli,so unaweza amua lipa kisasi lakini akakushinda au kukuumiza hata zaidi.

kisasi kitakupotezea muda wako bure ambao ungeutumia kutafuta pesa zaidi kuzibia hilo pengo la hasra alilokuletea

mpotezee huyo rafiki mnafiki you still have opportunities to earn more than aliyokudhulumu,ila kuwa makini sana kuanzia sasa mazoea yawe ya salamu tu na sio mambo yako ya pesa au ya ndani zaidi na pia hakikisha hawi karibu hata na mke wako na watoto pia marafiki wa aina hiyo ni hatari sana.

kila la kheri mkuu.
 
Last edited by a moderator:
Kwanz jamaa laikupiga sound atm kadi ya kutoa 2.5 bado haikuruhusiwa by then....haukuwa makini na je alikuomba mda gani kama ni mchana hata j.pili ilimlazimu kutoa ndani bila hata kadi ni id zake tuu zahitajika....pili alikupiga sound why you of all the pipo umpe hiyo hela!!!!uwe unareason siku nyingine...haupajui kwake au kazini kwake?hupajui panapouzwa maji ya kuchoma!!beba tindikali kampe dozi au kamuharibie kwa ngumi tuu au kazini kwake!!!au mfanyie umafia na wana mumteke mumpige picha za uchi azikomboe kwa mil 6!! Wewe kweli umetoka kijijini matombo....
 
Pole mwaya;
Siku hizi watu hawaaminiki.
Rafiki yako akija kwa jina la mkopo
kama unazo mpe kama zawadi tu; vinginevyo ni kulizwa tu.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
pole sana mkuu hii imekula kwako tu fanya mambo mengine!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! kuwa kama me urafiki wa kuombana hela amana... usimwamini mtu kwenye swala la hela kabisa never okey!!!!!!!!
 
Watu wengine hawana soni,
hisani kwao ni historia Usife moyo utapats zaidi ya hio *100%
 
Una uhakika bado yuko kwenye hiyo kazi mpaka sasa? manake hapa pananukia harufu ya utapeli!! huyu jamaa ni tapeli mzoefu.

Huyu atakuwa hana kazi hiyo,na kama ni yeye aliyekuambia amehamishiwa makao makuu alikuwa anakujenga tu,na unabahati angekula ile 15M ingekuwa hatari zaidi,ni tapeli mzoefu huyu
 
Kwa kuwa wewe ni ALWATAN wa mjini na kijijini MSAMEHE bwana, si unjua ww ni Alwatan unazo za kumwaga!
Ahhhh ALWATAN bwana hadai madeni madogo kama hayo!
 
Tumezaliwa kijiji kimoja, nimekuwa naye kijijini na nimesoma naye shule ya msingi, tuliachana tukiwa tunakwenda Secondary mpaka tunamaliza vyuo vikuu ambavyo tumesoma vyuo tofauti, tulikuwa tukionana pale kijijini mara chache sana wakati wa likizo mpaka tulipomaliza chuo.

Baada ya kumaliza chuo tulionana Dar katika mihangaiko ya kutafuta kazi, tulibahatika kupata kazi katika Taasisi mbili tofauti, yeye alipangiwa mkoani mimi nilipata nafasi hapa hapa Dar, ni zaidi ya miaka sita hatukuwahi kuonana face to face zaidi ya kuwasiliana kwa simu na kuchart kwenye mitandao.

Mwaka 2012 alihamishiwa kikazi hapa makao makuu ya Taasisi yao, kutokana na ukweli kwamba hapa mjini mambo ni mengi hivyo imekuwa ngumu sana kuonana mara kwa mara kwa masaa ya kutosha kiasi kwamba tunaweza tukastukiana kama kuna mabadiriko makubwa ya tabia baina yetu, tumekuwa tukionana mara chache sana tena sehemu za Starehe.

Mwezi July2012 alinishirikisha deal moja zuri sana lilikuwa la maslahi ya kutosha lakini, ilitakiwa nichangie kama Million15 ndani ya wiki moja, kutokana na hali yangu kifedha nilipigana sana ndani ya wiki hiyo ikaniwia ngumu kuikamata M15 hivyo nikalikosa lile deal nilisikitika sana.

Mwezi April 2013 miezi saba iliyopita ilikuwa ni jioni siku ya jumapili alinipigia simu kwamba yupo Mlimani City kuna transaction ya 2,500,000 anataka kuifanya amefanikiwa kutoa 800,000 lakini kadi imezama itabidi aifuate kesho yake asubuhi, akaniambia anahitaji hard Cash 1,700,000 za haraka haraka kama itawezekana vinginevyo atapata hasara kubwa, kiukweli ishu aliyoniambia ilikuwa ni lazima niamini, isitoshe ni mshkaji.

Kutokana na ukweli kwamba huwa ananisifia kwamba mimi ni 'ALWATANI' hapa mjini nililazimika kupambana ili ipatikane hiyo 1,700,000 nisimuangushe jioni hiyo hiyo japo mimi nilikuwa na 900,000 kwenye Akaunti yangu nikaongezea na 700,000 kutoka kwa mshkaji wangu aliye na duka pale Mwenge, then nikamkabizia.

Kesho yake asubuhi ya saa4 alinipigia simu kwamba wamepatwa na msiba wamefiwa na mfanyakazi mwenzao Ofisini yeye kateuliwa kuwa mmoja wa watu waliotakiwa kwenda Kilimanjaro kupeleka Maiti/Msiba, hivyo akadai akipata time atachomoka mara moja aende Benki arekebishe ule mzigo, siku hiyo hakufanya hivyo sikutaka kumsumbua sana nikasubiri arudi ila nikajitahidi kumalizana na mshikaji wangu wa dukani kwa kuhamishia deni kwa mtu mwingine, aliporudi toka Kilimanjaro akanishirikisha tatizo lingine, amekuwa akifanya hivyo kila ninapompigia huku akiniomba nimvumilie.

Siku zimekwenda miezi inakatika mpaka sasa nikimpigia simpati nahisi kani-Block, nikimpigia kwa simu nyingine anapokea lakini akistukia ni mimi ananikatia simu, hiki kitu kimekuwa kinanikera sana hakuna kitu kinachokera kama kukatiwa simu na mtu ambaye wewe unadhania ni rafiki yako.

Wadau nishaurini nimfanyeje huyu jamaa, ikumbukwe kwamba sina ushahidi kwamba kanidhulumu na kanisababishia usumbufu.

Huyo atakua kakutapeli hata lile deal la milioni 15 ilikua magumashi,hii ilinitokea mwaka juzi nilipigwa kama wewe tena mwanamke sema nilicheza na police hadi nikamtia mikononi na hela akarudisha.Nakushauri ufuatilie hadi ujue anapoishi au kazini kwake tafuta mjeda lazima hela atarudisha hata kama sio yote
 
duh kikulacho kiko nguoni kwako jaribu kuendelea kumvumilia tu kama alivyokuambia ila taa ya hatari inakaribia kuwaka

Taa ilishawaka ndiyo maana nimejikuta naandika haya, na humu JF naamini yupo maana ni mpenzi sana wa mitandao
 
Yaani siamini

let me tell you my swt brodah!!
mtu wa kudhulumu hawez kudumu abadan! tena wala usimtakie makuu wewe sema ni kama vile ujenge nyumba iungue utasikitika lakin utajipanga life iende sio?? sasa hata kwa huyu umeshasikitika acha maisah yaende.
wala usiumize akili yako ipo siku yatakuja kumkumba ya kumkumba
 
Pole yako watu kama hao ndo wanafanya hata watu wengine wakiwa na shida washindwe kusaidiwa

manake na wewe nae ukajifanya ALWATAN haswa kwa kuitafuta hiyo pesa kumkopesha rafiki.....

Ofisin kwao hukujui....we nenda mvae face to face uone ye anaongea nini kama kwenye sim anakuzingua

Nilishawahi kufunga safari, nionane naye face to face ila nilipofika karibu nikajifikiria mbali kama ameamua kunifanyia ushenzi kama kuni-block nakadhalika atashindwaje kunianzishia bifu ofisini kwake then nionekane muhuni bure
 
da aisee,mfuate bwana akupe chako,je mliandikishana mahali?mara pili usirudie bora mnaandikishana mbele ya mwanasheria na anaweka rehani kitu,usimwamini mtu
 
Back
Top Bottom