Mkali popote
JF-Expert Member
- Aug 18, 2014
- 633
- 340
- Thread starter
- #21
Nashukuruni kwa ushauri jamani manake apa presha imeanza kushuka wandugu
nenda haraka kituo cha ushauri nasaha kapime kisha uanzishiwe arv kwa ajili ya pep (endapo hutakuwa na virus). Hii inahitaji kufanyika haraka kabla ya kumaliza masaa 72.
nenda kapime. Vipimo pekee ndio vitathibitisha kama umeambukizwa au la.
Ndugu yangu huyu mtu ni msanii ametunga hii stori ili nae apate umarufu kama wangu hapa jf hahahahahahahahaa
1.Mtu aliye na ARVs sio lazima ziwe zake au anazitumia labda kama umethibitisha hivyo kwa kupata na kadi yake ya CTC 1.
2.Prostitutes wengi mjini wanatumia ARVs huku wakiwa hawana HIV.....hutumia kama Pre exposure prophylaxis(PrEP) yaani kujikinga na maambukizi kutoka kwa wateja wao..zinapatikana ktk black market
3.Kama ni kweli yeye ni muathirika wa HIV na anatumia hizo dawa vizuri basi huna sababu ya kuchanganyikiwa....
Reason and facts;
-Possibility ya kupata HIV kwa tendo moja ni 0.03%.
-Possibility hii imesimama kwenye ground ya Viral Load(wingi wa virus ktk damu)
Kwa mgonjwa aliyetumia dawa vizuri bila kuchakachua anategemewa kuwa na Undectable level of virus....hii inamaanisha ukipima viral load unakuta 0 ingawa mgonjwa ana HIV.....
Sasa mgonjwa mwenye undetectable level of virus au hata mwenye viral load ndogo uwezo wake wa kuambukiza unapungua sana na hivyo unaweza ukafanya "ngono peku"
na usipate maambukizi....
Ushauri.....
Usipanick....ukipima leo HIV ukaikuta basi sio ya huyo dada..ulikua nayo,
Kama ukipima ukakuta Negative basi nenda kwa daktari na utapewa ARVs dozi ya siku 28 Post Exposure Prophylaxis na utasalimika....dawa hii huwa effective kama dozi ya kwanza itatumika ndani ya masaa 72 post event....Sasa amua haraka na ukimbie hospital ukafanye mchakato huu....
Asante na pole sana jembe.!
Ndugu yangu huyu mtu ni msanii ametunga hii stori ili nae apate umarufu kama wangu hapa jf hahahahahahahahaa
Ufafanuzi wako mzuri sijui ni kweli?
Wakuu,
Katika pitapita yangu jana baada ya kupiga safari lager za kutosha si nikakutana na mrembo, maskini ya Mungu bila kujua kitu mwanaume nikakokota hadi geto nikajilia vyangu.
Maajabu leo katika kukagua kibegi chake nimekutana na ARV yaani hapa nimechanganyikiwa nimeamua tu nishinde bar kupoteza mawazo.
Embu nishaurini wakuu nimfanyaje huyu bidada manake japo nilitumia kinga sina furaha kabisa.
Wakuu,
Katika pitapita yangu jana baada ya kupiga safari lager za kutosha si nikakutana na mrembo, maskini ya Mungu bila kujua kitu mwanaume nikakokota hadi geto nikajilia vyangu.
Maajabu leo katika kukagua kibegi chake nimekutana na ARV yaani hapa nimechanganyikiwa nimeamua tu nishinde bar kupoteza mawazo.
Embu nishaurini wakuu nimfanyaje huyu bidada manake japo nilitumia kinga sina furaha kabisa.