Nimechanganyikwa naomba mawazo yenu wanajf wenzangu.

nnunu

JF-Expert Member
Mar 4, 2011
654
230
NAHISI DUNIA IMENIGEUKA,
muda wangu wote,juhudi zangu zote,ndoto zangu zote,
maisha yangu yote naona kama ndiyo yamefikia mwisho.

Nilifanya mtihani wa kidato cha sita kama private candidates,
lakin NIMEFELI nina Dvn four (4) ya 18,GS-s,hst f, kisw -D,na eng f.
ndoto za kwenda chuo kikuu zimeyeyuka ghafla,
naona giza totolo mbele yangu,ila naamini kupitia,
hapa JF naamini wadogo zangu,wanangu,wajukuu zangu,
pamoja na wakubwa wenzangu mtanisaidia kimawazo nini cha kufanya.
mimi napenda sana nikasomee CBE mambo procurement kwa kuanzia na
diploma je ntaweza kufanikiwa kupata nafasi.Form nimeshachukua ila
sijarudisha,wasiwasi wangu je nitaweza kupata nafasi??.
matokeo ya form four yana hst-c,kiswa-c,eng-b,geo-d,
civic-d,. Yataweza kunisaidia kuingia diploma??.

Sitaki mkopo najilipia mwenyewe kwa sababu mimi siyo mwajiriwa,
nimejiajili mwenyewe na vibiashara vyangu vyenye uwezo wa kuniwezesha,
kumudu gharama zote kipindi chote cha masomo.
Sijapeleka jukwaa la elimu kwa sababu kule kuna wachangiaji wachache,
tofauti na huku ambako naamini nitapata mawazo mengi sana na yenye kunifaa.
Nawaomba muwe wa wazi tu,kama inawezekana sawa na kama haiwezekani niambieni pia. Ukweli wako ndiyo mafanikio yangu.

Samahani kwa maelezo marefu.
 
Pole sana NNUU!
Huna ya kukata tamaa kiasi hicho, sidhani kama kufeli kwako masomo ndiko kufeli maisha, ninachoamini maisha yataendelea na madamu maisha yanaendelea u can try again and again ukiamini kuwa kwa juhudi ufanyazo mwisho wa siku utafikia lengo lako.

Kuhusu CBE jaribu kupata ushauri kutoka kwao nafikiri itakuwa ni njia nzuri ya kuwa sure na kuokoa muda pia!!

Pole sana huna haja ya kukata tamaa na kupoteza matumaini kiasi hicho!!!!
Mungu akutangulie usifikie maamuzi ya kuutesa Moyo wako!!!
 
Kama umechukua form zijaze kisha rudisha kisha subiri majibu , usikate tamaa. tuma vyuo vingine pia.
 
Unajua mkuu si kwamba wanaofeli huwa ni vilaza, hasha. Kufaulu inategemea pia na utulivu wako unapofika chumba cha mtihani. Usikate tamaa kwani bado una 99% za kufaulu maisha. Evidence umeshaionesha kwa kutaka kusoma cbe.
Kuhusu cbe nenda kaongee nao, japo kuna uwezekano mkubwa wa kuanza ngazi ya cheti, ukifaulu unaenda diploma.
 
pole sana nnuu!
Huna ya kukata tamaa kiasi hicho, sidhani kama kufeli kwako masomo ndiko kufeli maisha, ninachoamini maisha yataendelea na madamu maisha yanaendelea u can try again and again ukiamini kuwa kwa juhudi ufanyazo mwisho wa siku utafikia lengo lako.

Kuhusu cbe jaribu kupata ushauri kutoka kwao nafikiri itakuwa ni njia nzuri ya kuwa sure na kuokoa muda pia!!

Pole sana huna haja ya kukata tamaa na kupoteza matumaini kiasi hicho!!!!
Mungu akutangulie usifikie maamuzi ya kuutesa moyo wako!!!


asante sana kwa kunipa moyo,
nitakwenda jumatatu nikaonane nao.
Shukurani sana.
 
Huna haja ya kukata tamaa, nenda huko CBE utapata ushauri zaidi!
 
Kama umechukua form zijaze kisha rudisha kisha subiri majibu , usikate tamaa. tuma vyuo vingine pia.

ASANTE,
NI CHUO KIPI KINGINE KILICHOPO HAPA DAR
KINACHOTOA HIYO KOZI YA PROCUREMENT??,
Siwezi kwenda nje ya mkoa ksb nina mtoto mdogo,
siwezi kumwacha,ila kwa hapa DAR naweza kuhudhuria,
vipindi bila matatizo yoyote.
samahani kwa usumbufu.
 
Unajua mkuu si kwamba wanaofeli huwa ni vilaza, hasha. Kufaulu inategemea pia na utulivu wako unapofika chumba cha mtihani. Usikate tamaa kwani bado una 99% za kufaulu maisha. Evidence umeshaionesha kwa kutaka kusoma cbe.
Kuhusu cbe nenda kaongee nao, japo kuna uwezekano mkubwa wa kuanza ngazi ya cheti, ukifaulu unaenda diploma.

asante, kwa ushauri wako,
pia upo sahihi kabisa,
umakini wakati wa kufanya mtahani wowote ni muhimu.
 
NAHISI DUNIA IMENIGEUKA,
muda wangu wote,juhudi zangu zote,ndoto zangu zote,
maisha yangu yote naona kama ndiyo yamefikia mwisho.

Nilifanya mtihani wa kidato cha sita kama private candidates,
lakin NIMEFELI nina Dvn four (4) ya 18,GS-s,hst f, kisw -D,na eng f.
ndoto za kwenda chuo kikuu zimeyeyuka ghafla,
naona giza totolo mbele yangu,ila naamini kupitia,
hapa JF naamini wadogo zangu,wanangu,wajukuu zangu,
pamoja na wakubwa wenzangu mtanisaidia kimawazo nini cha kufanya.
mimi napenda sana nikasomee CBE mambo procurement kwa kuanzia na
diploma je ntaweza kufanikiwa kupata nafasi.Form nimeshachukua ila
sijarudisha,wasiwasi wangu je nitaweza kupata nafasi??.
matokeo ya form four yana hst-c,kiswa-c,eng-b,geo-d,
civic-d,. Yataweza kunisaidia kuingia diploma??.

Sitaki mkopo najilipia mwenyewe kwa sababu mimi siyo mwajiriwa,
nimejiajili mwenyewe na vibiashara vyangu vyenye uwezo wa kuniwezesha,
kumudu gharama zote kipindi chote cha masomo.
Sijapeleka jukwaa la elimu kwa sababu kule kuna wachangiaji wachache,
tofauti na huku ambako naamini nitapata mawazo mengi sana na yenye kunifaa.
Nawaomba muwe wa wazi tu,kama inawezekana sawa na kama haiwezekani niambieni pia. Ukweli wako ndiyo mafanikio yangu.

Samahani kwa maelezo marefu.

Unajua kufika chuo kikuu kuna njia nyingi sana mpendwa, kama lengo lako ni kufika chuo kikuu na kuendelea zaidi ya hapo basi jaribu njia mmbadala ambayo wengi ninaowafahamu mimi wamefanikiwa.

So long as una uwezo wa kujilipia ada as you said, na pia naona matokeo yako hapo una : D = ya kiswahili, na S- ya GS, basi naomba uni- PM ili tuweze kujadilina vema na kukupa ushauri wa njia ya kupita na hatimaye ndoto zako kuweza kutimia kuendelea na masomo zaidi.

Kuhusu CBE kuna competition sana siku hizi na hawachukui watu wengi so unaweza kuta -uka-apply then baadae ukakosa na ukakata tamaa ya kusoma tena.

NB: Hata kama kuna mdau mwingine mwenye tatizo kama la huyu ndugu, basi ani-PM immediately na kuona kama anaweza fanikiwa au kuchange field na baadaye kujiendeleza zaidi kwa field uipendayo.
 
pole mkuu,nimefurahi kwamba umri umeenda lakini bado una mikakati chanya ya kujiendeleza kimasomo, anyway kiukweli ukiwa na D-tano za form 4 unaruhusiwa kuchukua hiyo kozi yako(ingawa sasa ina compition kiaina) kwa ngazi ya cheti mwaka mmoja, ukifaulu vizuri una tena chance ya kuchukua diploma same field...na baada ya hapo unasongesha. Sasa wewe kwa matokeo ya form 4,tayari una C-2 na B-1 na D-2...so you are qualified for diploma field of 3 yrs. NB, depends on comptition..just try and check it out.
 
Mimi mpaka leo hii sijaelewa kabisa curriculum inayotumiwa katika elimu ya upili Tanzania. Hata text books zinazotumiwa sizijui. Jinsi hata wanavyosahihisha hiyo mitihani sielewi.

Kwa kifupi mfumo mzima wa elimu uko hovyo na shaghalabaghala kupita kipimo. Labda ni mimi ambaye sikuwa na pay attention darasani....but I think the whole educational system is so jacked up to prepare students to fail.
 
Unajua kufika chuo kikuu kuna njia nyingi sana mpendwa, kama lengo lako ni kufika chuo kikuu na kuendelea zaidi ya hapo basi jaribu njia mmbadala ambayo wengi ninaowafahamu mimi wamefanikiwa.

So long as una uwezo wa kujilipia ada as you said, na pia naona matokeo yako hapo una : D = ya kiswahili, na S- ya GS, basi naomba uni- PM ili tuweze kujadilina vema na kukupa ushauri wa njia ya kupita na hatimaye ndoto zako kuweza kutimia kuendelea na masomo zaidi.

Kuhusu CBE kuna competition sana siku hizi na hawachukui watu wengi so unaweza kuta -uka-apply then baadae ukakosa na ukakata tamaa ya kusoma tena.

NB: Hata kama kuna mdau mwingine mwenye tatizo kama la huyu ndugu, basi ani-PM immediately na kuona kama anaweza fanikiwa au kuchange field na baadaye kujiendeleza zaidi kwa field uipendayo.

ASANTE kwa ushauri wako,
ila jinsi ya kuanza kukuPM sifahamu, ila najua kureply PM tu,
naomba unipm halafu mimi nitareply.
samahani kwa kukusumbua.
 
pole mkuu,nimefurahi kwamba umri umeenda lakini bado una mikakati chanya ya kujiendeleza kimasomo, anyway kiukweli ukiwa na D-tano za form 4 unaruhusiwa kuchukua hiyo kozi yako(ingawa sasa ina compition kiaina) kwa ngazi ya cheti mwaka mmoja, ukifaulu vizuri una tena chance ya kuchukua diploma same field...na baada ya hapo unasongesha. Sasa wewe kwa matokeo ya form 4,tayari una C-2 na B-1 na D-2...so you are qualified for diploma field of 3 yrs. NB, depends on comptition..just try and check it out.

ASANTE SANA KWA MAONI YAKO,
nikienda kurudisha form jumatatu itabidi nikawaulize,
then nione ntajibiwa nini.
Nimeileta hapa jukwaani kabla sijarudisha form,
ili niweze kupata mawazo zaidi, kama huu wa kwako,
na mingine mingi zaidi.
asante sana.
 
Sasa wewe wa pm unataka malipo ya ziada?
kwanini usiwe muwazi kwa kuweka mawazo yako hapa tuyapime?

Unataka uandikiwe PM ilimawazoyako yaonekane yameenda shule kumbe ukiyaweka wazi yatakua ya kitoto.

Usitumie advantage ya watu wenye shida kuwalisha mawazo ambayo hayajachujwa.
 
Huna haja ya kukata tamaa, nenda huko CBE utapata ushauri zaidi!

asante katavi,
nimekuelewa ntaufanyia kazi ushauri wako.

naona hata Like nayo imetolewa nashindwa kubofya,
inabidi nijibu kwa njia hii tu.
asante.
 
Sasa wewe wa pm unataka malipo ya ziada?
kwanini usiwe muwazi kwa kuweka mawazo yako hapa tuyapime?

Unataka uandikiwe PM ilimawazoyako yaonekane yameenda shule kumbe ukiyaweka wazi yatakua ya kitoto.

Usitumie advantage ya watu wenye shida kuwalisha mawazo ambayo hayajachujwa.


Kaka jambazi ASANTE sana kwa mawazo yako,
hapo kwenye kukolezwa rangi napo pana maana sana tena sana,
ndiyo Tanzania yetu hii kila kitu watu wanageuza dili.

Lakin ningekuwa najua jinsi ya kuanza PM ningempm ili nimsikilize ushauri wake,
labda unaweza kunisaidia japo angeweka hapa labda ungeweza kuwasaidia wengi,
labda kuna wengine wenye tatizo kama langu japo hawajaweka wazi.
 
Mimi mpaka leo hii sijaelewa kabisa curriculum inayotumiwa katika elimu ya upili Tanzania. Hata text books zinazotumiwa sizijui. Jinsi hata wanavyosahihisha hiyo mitihani sielewi.

Kwa kifupi mfumo mzima wa elimu uko hovyo na shaghalabaghala kupita kipimo. Labda ni mimi ambaye sikuwa na pay attention darasani....but I think the whole educational system is so jacked up to prepare students to fail.

Ndiyo Tanzania yetu hii Nyani Ngabu,
Laiti wangekuwa jinsi wengine tunavyoumia kwa ,
kujituma angalau tujielimishwe ili tusiachwe nyuma na wasomi,
wenzetu wala wasingekuwa wanafanya mchezo na elimu.

Bado hatuna jinsi tutapambana hivyohivyo japo,
IMENIUMIZA KUPITA KIASI.
 
1.maisha siku zote yana changamoto.
2.changamoto zisikukatishe tamaa bali kukupa ari ya kusonga mbele.
3.nenda chuo cha uhasibu kurasini,mwone mkuu wa idara ya procurement mama mavis ni mtu mzima.utatoka unachekelea.
 
Pole sana ndugu
usikate tamaa yote maisha
wasiliana na saweboy akupatie njia mbadala
pamoja na michango mingine ya wadau
Mungu awe pamoja nawe
ninaamini siku moja utafika pale unapohitaji kuwa
 
Usijikite CBE tu pekee jaribu na vyuo vya ualimu pia, watu huwa wanadharau ualimu lakini unalipa sana, usikate tamaa. manake huko CBE utamaliza ajira pia matatizo.
 
Back
Top Bottom