Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 29,446
- 40,432
Nilianza kimzaa mzaa, nikaanza kujiunga kwenye magrupu ya wafanya biashara, wajasiriamali, wanaofanya fedha za kimtandao n.k kutoka huko duniani.
Nimekuwa namwaga nondo nzito, za kibiashara za kimataifa na namna ya kufanya uwekezaji wa hapa na pale popote duniani n.k
Nimejikuta napata marafiki wengi kutoka Canada, Marekani, Uingereza, Romania, India, Pakistani, Bangladeshi, Norway n.k, na wote tunashea mawazo ya kibiashara na namna ya kufanya uwekezaji mdogo mdogo na mkubwa.
Kuna mwingine ameanzisha kampuni yake huko Ulaya, lakini bado iko changa ila amekuja kuniomba ushauri wa namna ya kufikisha malengo yake huko mbeleni.
Nimejikuta nacheka mwenyewe na kusema kimoyo moyo, kumbe sikuchezea hela ya ada ya wazazi wangu.
Vijana tuchangamke, tuachane na marafiki wa mazoea mazoea; tutafute marafiki wenye tija huko duniani, muhimu lugha iwe inapanda tu, na pia 'argument' zako ziwe zakisomi zenye 'standard' zinazotambulika kimataifa.
Leo ni hayo tu; mwenye akili apambane.
Nimekuwa namwaga nondo nzito, za kibiashara za kimataifa na namna ya kufanya uwekezaji wa hapa na pale popote duniani n.k
Nimejikuta napata marafiki wengi kutoka Canada, Marekani, Uingereza, Romania, India, Pakistani, Bangladeshi, Norway n.k, na wote tunashea mawazo ya kibiashara na namna ya kufanya uwekezaji mdogo mdogo na mkubwa.
Kuna mwingine ameanzisha kampuni yake huko Ulaya, lakini bado iko changa ila amekuja kuniomba ushauri wa namna ya kufikisha malengo yake huko mbeleni.
Nimejikuta nacheka mwenyewe na kusema kimoyo moyo, kumbe sikuchezea hela ya ada ya wazazi wangu.
Vijana tuchangamke, tuachane na marafiki wa mazoea mazoea; tutafute marafiki wenye tija huko duniani, muhimu lugha iwe inapanda tu, na pia 'argument' zako ziwe zakisomi zenye 'standard' zinazotambulika kimataifa.
Leo ni hayo tu; mwenye akili apambane.