Nimeachiwa mtoto ndani ya basi

Nimeachiwa mtoto ndani ya basi

kwa kuwa umeshatoa taarifa polisi basi yatosha,
kikubwa na cha muhimu mlee kwa uadilifu mkubwa na mungu ni mwema kwa hakika atakulipa ondoa shaka.
 
Huyo ndio first born wako
Hongera kwa kupata mtoto

Just for love
 
yaani ingekuwa mimi hizo taratibu za polisi nazifanya kwa security ila kimoyo moyo ningefurahi zaidi maana ile stage ya kuhangaika na nepi kashapita huyo, wee ni kulea tuu. Usilaumu sana wengine wanatafuta watoto hawapati
 
Hii mbona ni bahati mkuu, lea tu , ila nakushauri ukatoe ripoti kwenye vyombo husika (ustawi wa jamii kama sikosei). Ripoti pekee uliyotoa pale polisi sidhani kama inatosha!

Nimeupokea ushauri wako mkuu.
 
yaani ingekuwa mimi hizo taratibu za polisi nazifanya kwa security ila kimoyo moyo ningefurahi zaidi maana ile stage ya kuhangaika na nepi kashapita huyo, wee ni kulea tuu. Usilaumu sana wengine wanatafuta watoto hawapati

Nimekusoma mkuu.
 
Ndo inavyokuwaha. Wazazi waje wajitokeze baadae na ugomvi juu kumtaka mtoto.

Ki ukweli huwa sipendi kufanyia masikhara malezi ya mtoto
Kama ni mimi nimeachiwa mtoto wa aina hiyo na kisha akaja mtu anaejidai ni mama yake
Kwanza nakwenda kuripoti polisi maana naweza hata kumdhuru huyo anaejidai mama wa mtoto

Kenge kabisa hao wanaowatelekeza watoto wao
Waliwazaa wa nini?

Hebu wapokee kwanza hii dedication kutoka kwa huyu mkuu
Lucky Dube CHILDREN FROM THE STREETS - YouTube

images


"Children In The Streets"

Sitting by the door
One morning,
Looking at the children going to school man, then I thought about the ones in the street;
Moving up and down
No where to go,
No education,
No future.
Then I thought about their parents man, why do they suffer so much.
If they have parents why.
(if you really don't want no children why do you have them, why) [x2]

[Chorus]
We can fight and no one's hurt
We can stop children from the street. [x3]

It's a cold winter man, moving back cooler down khilo street man
His father is relaxing in the best bar in town asking them to fill his glass man.

His mother is kissing on another man.
If you really don't want no children, why do you have them.
If you can't care for them why...

[Chorus till fade]
 
Amicus Curiae,

Pole kwa shida yako, hata hivyo nadhani nina mtazamo tofauti,
Sishauri, umlee mtoto(si kwa nia mbaya) bali kwa nia njema tu.

1. Kumbuka uliacha vitambulisho na amawasiliano yako kwa ajiki ya kusaidia hili, lakini unadhani ni watu wema wote ndio watakao kuwa na mawasiliano hayo? Namaanisha , wanaweza kujitokeza wengi wenye kudai wanamfahamu mama wa mtoto na kumbe nia yao ni kumchukua mtoto .

2. Kwa kuacha utambulisho wako, na baadae kuondoka na mtoto miaka kadhaa baadae labda kutokana na mtoto kukua vyema au kupata mafanikio anaweza kujitokeza mama HALISI wa mtoto au tapeli, je utakataa?Utathibitisha?Mchakato wa kufanya vinasaba(DNA) nchi hii una ugumu wake unaujua? Zaidi ya yote hakuna uhakika wa vinasaba(DNA) yenyewe kutokana na Rushwa iliyopo.

3. Mipango yako binafsi, upokevu wa suala hilo kwa familia, mpenzi wako tayari kina ugumu, Vipi kuhusu ndugu wa girlfriend zako(pressuming utamuoa). Je, suala la kubaguliwa kuliko watoto wengine mtakaowapata, utaliepukaje?

Binafsi ningeshauri, kufanya mawasikiano na Ofisi ya Polisi kituo ulichoondokea mf. Ubungo n.k. na kupanga mkakati wa kumrejesha mtoto katika kituo cha kulelea watoto.

Lakini hapa pia nadhani kuna umuhimu wa kuangalia suala lingine la ulinzi, mfano uwepo wa Camera. Hii itapunguza wizi na matukio mabaya kama haya.
 
Last edited by a moderator:
Inasisimua na kutia huruma kwa mtoto ambaye ametelekezwa mikononi mwako... Nakushauri kaka mlee kama vile wakwako hadi hapo mama au ndugu wa mtoto watakapojitokeza ila nakusihi jitahidi kumfanyia ibada kupata kibali mbele za Mungu. Hatuwezi jua ametokea wapi.... Wengi wamesema ni baraka umeletewa, lakini pia kuna wakina Zinduna.

Mungu akubariki kwa moyo wa upendo ulio nao.
 
Hongera sana,Mungu akupe uweza wa kumlea vema,na baya lolote lisitokee...
 
Mlee tu kaka. Vipi shem hana noma lakini isije akamtesa tu huyo malaika wa mungu?
 
Ndg mleta mada MUNGU aendelee kukubariki kwa Huduma hiyo manake cwote wenye uTAYARI huo ukichukulia bado hujao! Ila kwa namna hii inafikia hatua watu watashindwa kusaidiana! Juzi ilibidi nimkwepe DADA 1 airport alipima Mzigo ukawa umezidi kanambia nimsaidie BEGI 1 nilimuangalia hadi kajishtukia Kiukweli tangu babu 1 apewe BEGI lenye BUNDUKI kwenye GARI asee ckotayari kumsaidia mtu hata km amecmamia uKUCHA kwakukosa nafasi yakukaa!
 
Ndg mleta mada MUNGU aendelee kukubariki kwa Huduma hiyo manake cwote wenye uTAYARI huo ukichukulia bado hujao! Ila kwa namna hii inafikia hatua watu watashindwa kusaidiana! Juzi ilibidi nimkwepe DADA 1 airport alipima Mzigo ukawa umezidi kanambia nimsaidie BEGI 1 nilimuangalia hadi kajishtukia Kiukweli tangu babu 1 apewe BEGI lenye BUNDUKI kwenye GARI asee ckotayari kumsaidia mtu hata km amecmamia uKUCHA kwakukosa nafasi yakukaa!

Ndio tunakoelekea huko mkuu, itafika kipindi tutashindwa kusaidiana.
 
Nilikuja dar kikazi kwa takribani siku 4, sasa jana nikawa narudi mkoani kwangu. Wkt nipo Ubungo nimekaa kwenye dar express akaja mama mmoja mtu mzima mweupe amebeba mtoto, akaketi pembeni yangu, nikamsalimia nikapiga kimya.


Akaniomba nimbebee mtoto akajisaidie, nikakubali. Muda ukawa unazidi kwenda yule mama harudi! hadi basi linajaa hajarudi, mara kakaja kadem kamoja kakaketi kwenye ile siti ya yule mama nikapigwa na butwaa! nikamueleza kwamba ile siti ina mtu, akanionyesha tiketi yake ikabidi nimuamini kwamba kweli ile ni siti yake

Wkt basi linataka kuondoka ikabidi nimpe taarifa konda, tukashuka na konda na baadhi ya abiria hadi kituo kdg cha polisi ubungo, polisi hawakuniamini sana, wakadhani nafanya usanii nilipotaka kumuacha pale mtoto, ikabidi nipige copy vitambulisho vyangu na niache mawasiliano yangu niondoke na mtoto.

Wamama ndani ya basi wakawa wanapokezana kukabeba na kukalisha, ni katoto ka kiume, ka-handsome, baba, mama na girlfriend wangu nao hawaniamini, wanadhani ni mwanangu! Dah!
Ndugu Amicus C, Narudi tena hii inapasua kichwa changu!! Mtoto wa miaka 2 ? Mama yake sii alishamlea na kuzoeana naye? Hukuweza kusoma nia yake au kusudiyo lake huyo mamamtu? WHY afanye hivyo? Aisee!! msuali ni mengi !!
Mkuu weplay your role.
 
Back
Top Bottom