Nilivyoyaona maendeleo ya Tanzania baada ya kuwa Ulaya kwa zaidi ya miaka minne

Ulaya siyo kwako hata uponde meisho wa siku utarudi huku kuchafu unakosema
 
Mkataa kwao mtumwa.. wewe unatuponda wakati ndege zinafululiza kuja bara na visiwani wazungu wanapagawa na bongo hii hii chafu..kila mtu ashinde mechi zake tulipo leo ni pazuri kuliko Jana..au nasema uongo ndugu zangu?
Aiseee juzi nilipita maeneo ya Mbagala pale karibu na kituo cha daladala cha Rangi tatu. Daaah huku barabarani hii mitaro ina maji yametuama mpaka yamekuwa meusiiii na yanatoa harufu mbaya kwelikweli, alafu jirani tu kuna mama ntilie, kuna watu wanauza matunda na wengine sijui mitumba na chipsi yanii nilishangaa mno.

Dar ni chafu chafu chafu inanukaaa.
 
Aisee nimeishia tu kuguna Yani unavyo ponda Kama sio kwenu ndio Mana katika story zako zako hujazungumzia hata nyumbani kwenu inamana hujafikia kwenu umeishia hotel nilivyo kuelewa Mimi ni kwamba unatusimulia Kama umefika ulaya we tuache na Tanzania yetu kaishi ulaya
Usitetee ujinga mkuu, Dar ni chafu na inatia kinyaa.. Mara nyingine bora hata tunaoishi mikoani.

Dar ni takataka na washamba tu mmejazana huko..
 
Mitaro hiyo ni michafu zaidi ya miaka kumi na maeneo hayo wapo watendaji wanakusanya ushuru na migambo wanatumwa kukamatwa wamachinga bila kujali kufanya usafi, kupanua eneo la kufanyia biashara ili kuepuka ajali huko askari wa trafiki wakihangaika kuongoza magari yasiyo na nafasi yoyote ya kupeana ili kupishana. Mbagala Rangi Tatu ni AIBU ya mwaka.
 
Duuu!! Acha ujinga tulipoachiwa na wakoloni wasomi na matajiri wale unspajua?. Ni wapi?

Wewe hapo umefanya nini kwenu. Tuanzie kumjengea babako?

Weka picha!!! Siyo unasema sema tuu!!

Kwani sisi lazima tuwe km ulaya? Dar yetu Bongo land haivunjwi na tutarudi tu kutoka huku tuliko ndo tulivo ukome kuisemasema!!!

Kwenu tu bado mnalalia nyumba za tembe!!! maskin bana? Umeotea kisafari unaleta za kuleta hapa

Mtuache. Mfugale si mchezo? Kigamboni weee!
 
Mitaro hiyo ni michafu zaidi ya miaka kumi na maeneo hayo wapo watendaji wanakusanya ushuru na migambo wanatumwa kukamatwa wamachinga bila kujali kufanya usafi, kupanua eneo la kufanyia biashara ili kuepuka ajali huko askari wa trafiki wakihangaika kuongoza magari yasiyo na nafasi yoyote ya kupeana ili kupishana. Mbagala Rangi Tatu ni AIBU ya mwaka.
Ni bora na wewe umeliona hili... aisee ile ni aibu sana, na kama wale wachuuzi wanatoa ushuru na hali iko vile wana haki ya kugoma kutoa
 
Umekaa miaka 4 tu ila dharau na kudhania miaka 4 yatosha TZ ifanane na Munich/London/Paris etc etc?!

Sasa huo ndio ulimbukeni.

Nawajuwa watu wamekaa 30+ huko so called the 1st 🌎 lakini hata uwaambie nini wanakwambia kweli huko wameendelea lakini nyumbani tunajitahidi, kila mwaka mambo mapya, hawakai hotel, ni aidha kwa wazazi, nyumba zao au apartments, na wanajichanganya nasi bila dharau au kujifanya ghafla wao wako kwenye class fulani.

Nashukuru umerudi huko ulikotoka (kama kweli), maana watz kama nyinyi mwatutia aibu sana mkifika huko.

Hujaongelea kama ulikuja kuwekeza, kusaidia wazazi na ndugu, yaonekana hata akili yako haijakomaa, endelea na ulimbukeni wako tuachie TZ yetu
 
Kwetu Mwanza. Nitapaongelea siku ingine. Lengo siyo kujionesha, ama kwamba napachukia nyumbani. TANZANIA NI KWETU. LENGO LANGU NI KWAMBA TUNATAKIWA KUJITATHMINI. KUDHANI TUMEFIKA KUNATUPOTOSHA.
Sio lazima kuishi kama wao inawezekana tunavyoishi kwa msongamano ni kivutio tosha kwa nchi nyingine kuiga wakidhani ndo utamaduni wetu

Tunakubali ni kweli tunamapungufu yetu lakini pamoja na yote bado tunaona sio sawa na tulipokua,ITOSHE KUSEMA TANZANIA NI YETU NA SISI NDO WATANZANIA WENYEWE KUA MZALENDO PENDA TAIFA LAKO
 
Umeongea ukweli mkuu,

Nchi zetu za kiafrica tuna janga kubwa la kukosa right leadership Hali iliyofanya tushindwe kusimamia mambo ya msingi km mipango miji na usafi

Ukiangalia nchi kama Tanzania leadership chain imepararaizi kila kitu mpaka rais au waziri mkuu aseme

Wabunge, madiwani, wenyeviti wa mtaa hawa wote ni kama hakuna wanalofanya kila kitu wameiachia serikali kuu ifanye

At least nchi km Rwanda wamejitahidi Sana Leo hii Rwanda ukienda Hadi vijijini ni kusafi si mchezo coz Hadi wenyeviti wa mtaa wanatimiza wajibu wao ipasavyo.
 
Back
Top Bottom